Urafiki wa Kagame na Magufuli umeanzia wapi?

Urafiki wa Kagame na Magufuli umeanzia wapi?

Bukyanagandi,
Kama unasema kabila la JPM linajulikana ni KABILA GANI?Mbona hulitaji?Umesema JPM anatoka Chato iliyokuwa mkoa wa Kagera na sasa Chato iko Geita baada ya mgawanyo wa mikoa na Wilaya!
Wasukuma wako Mwanza, Shinyanga na Mara kidogo lakini kwa Chato wengi ni Wahaya,Wanyambo,Wazinza na makabila yote haya yana ukaribu na kiasi cha kuoleana.

Hivi unaweza kujuua uhusiano ulipo kati ya Museveveni na Kabila?

Yes mkuu Makoye 2009, sasa kuhusu uhusiano kati ya M7 na Kabila hapo ujafafanua vizuri mkuu, unauliza uhusiano wa kindugu/damu au wa kisiasa? Kitu kingine unataka tumzungumzie Kabila yupi? Kabila Jr au Sr fafanua kidogo mkuu.

Kabla ujajibu - mimi ntazungumzia Kabila Sr, yeye alikuwa mfuasi wa itikadi za Lumumba na alikuwa anampinga Mobutu hivyo akanzisha vita vya msituni vyenye lengo la kumuondoa madarakani Mobutu, operation zake kivita azikufanikiwa sana kutokana na kutokuwa commited 100% na vita vya ukombozi, alikuwa interested na mambo ya starehe na wanawake - weakness hii ilimsikitisha sana Mpiganaji Che Guevara ambaye wakati huo alikuwa ni Waziri chini ya Fidel Castro huko Cuba, lakini aliamua kuacha kazi na kuja Africa kwa siri na wanajeshi wachache kwa nia ya kuja kumsaidia Kabila kuwapa mafunzo wapiganaji wa Kabila katika msitu wa Congo alishiriki vile vile katika mapambano ya kuvizia dhidi ya jeshi la Mobutu chini ya ushauri wa CIA.

Che Guevara alikaa miezi tisa kama nakumbuka vizuri, lakini attitude za Kabila 2wards armed struggle zilimkatisha tamaa, straw ya mwisho ilitokea wakati walipo safiri kuja Dar kutoka porini DRC, walikuja kuchukua mizigo fulani na fedha zilizo kuwa donated na socialist countries kusaidia katika masuala ya ukombozi.

Kabila na Che walipo wasili Dar wakitokea Kigoma kwa Train kwa usalama wao wakawa wanalala hoteli tofauti, walikaa kwa muda wakifatilia kilicho waleta baada ya kufanikiwa - baadae walipanga siku ya kukutana kwa kupanga mikakati yao, siku waliyo panga kukutana Che aliondoka Hotel aliyofikia kwenda kukutana na Kabali Hotelini kwake, Che anaingia barabarani na kuanza kuembea kwa miguu ghafla anakutana na Kabila ameshikiria usukani wa Mercedes Benz i.e anaendesha!!! Che alishikwa na butwaa mwenzake kumbe peza anaziunguza kwenye matanuzi, siku nyingine wakakubaliana wakutane Hoteli aliyo fikia Che Guavara, kesho yake Che kasubiri wee Kabila aonekani!! Che kakata shauri kumfuata Kabila Hotelini, Che kufika Chumba cha Kabila alikuta mlango ajafungwa kwa ufunguo Che kufungua mlango akamkuta Kabila akiwa na wanawake watatu (sikumbuki vizuri) sijui wanne kitandani - Che kafunga mlango kwa nguvu na kuondoka zake huku amekasirika kweli kweli, baada ya siku chache kupita Che akahamua kurudi kwenye Msitu wa Congo kuwafuata wanajeshi aliyo kuja nao kutoka Cuba wakarudi wote Dar na kuondoka kurudi Cuba kupitia iliyokuwa Ujerumani Mashariki.

Kwenye simulizi zake Che anasema kwamba Kabila awezi ku-organise a credible fighting force kama atajidai kwamba anaweza basi hiyo itakuwa sawa sawa na ndoto za mchana, akasema tatizo lake ni kuendekeza sana starehe kuliko kutaka kuwakomboa Wafrica wenzake. Kwa kifupi kabisa hayo ndio maoni ya Che kuhusu Kabila Sr.

Sasa tuje uhusiano wa M7 na Kabila - again sijui unazungumzia Kabila yupi Sr au Jr - kama ni Kabila Sr - huyo aliwahi kuishi Uganda na familia yake under assumed name akiwa anaendeleza harakati zake za ukombozi huku akifanya biashara, sasa sijui walikuwa na ukaribu gani na M7 zaidi ya kupanga mbinu za kumuondoa madarakani Mobutu kwa kupigana vita kamili wakishirikiana na jeshi la PK, lakini wakati wanapanga hayo Kabila na familia yake alikwisha hamia Dar kwa miaka mingi akijiita Mfipa kwa jina ya O'Mutwale of course O'Mutwale ni Kiganda/Kinyankole/Kihaya kama sikosei.

M7 na Kabila Sr hawana undugu wowote walikuwa ni ma comrade in arm basi i.e wenye lengo moja kuingia madarakani kwa kutumia mtutu wa bunduki na walifanikiwa.

Tukienda mbali kidogo ni hivi: M7 ni Munyankole mwenye damu ya Kihima kama alivyo Mh.Kagame - wakati Kabila alikuwa Mkongomani wa mashariki ya Congo wenye asili ya kabila la Kimanyema kama walivyo baadhi ya wenyeji wa Kigoma, hivyo sidhani kama Kabila Sr ana damu ya Kihima hata kidogo.

Linapo kuja suala la
Kabila Jr (Rais wa sasa DRC) huyo is a different story iliyo ghubikwa na utata mtupu!!!. Nadhani nime eleweka mkuu.
 
tupe pia uhusiano wa mbowe na lowassa, maana kipindi cha jk mbowe na lowassa walikuwa maadui, urafiki wao umeanzajeanzaje

Countrywide,
This is an inept and non-sense question!
Hapa tunazungumzia uhusiano wa Marais wawili toka nchi mbili tafauti! Sasa unapohoji uhusiano wa ndugu 2 ambao ni Watanzania inatisha na inaskitisha!
Hii ni uthibitisho wa kile Serikali ya Kidikteta ya Rais JPM inataka kuanza kuwabagua Watanzania kwa MISINGI YA KIVYAMA AU UPINZANI!
Tumeshuhudia mpaka sasa jinsi Bunge letu limeanza kugeuzwa kuwa ni chombo cha CCM na Serikali yake KUWA ZIBITI WAPINZANI/UKAWA kwa vile tu wana mawazo tofauti na Serikali ya CCM kwa madai wanapinga serikali ya CCM!

Kwa sasa Serikali ya CCM chini ya JPM inataka kuigeuza Tanzania kuwa ni nchi ya Utawala wa CHAMA KIMOJA CHA CCM! Kwa serikali ya JPM na serikali yake WAPINZANI NI MAADUI wa serikali yake! Hii ni zana ovu na potofu na isipozibitiwa mapema inaenda kutengeneza uadui utakaoweza kusababisha janga na machafuko ndani ya Tanzania!
JPM ameshaanza kulewa madaraka na amesahau kuwa aliapa kuilinda na kuitetea KATIBA YA NCHI badala yake ameanza kuisigina!
KITENDO CHA KUTAKA KUZUIA MIKUTANO YA NJE NA NDANI YA VYAMA PINZANI NI UCHOCHEZI NA UCHOKOZI KWA UPINZANI AMBAO UNA WATANZANIA MILIONI 6 NYUMA YAO WALIOPIGIA KURA KUONYESHA IMANI YA KUONGOZWA NAO!

Magufuli lazima ashauriwe kuwa kuzuia mikutano ya Wapinzani ni kugandamiza haki,uhuru na demokrasia ya Watanzania milioni 6 waliokubali kuongozwa na UKAWA!

JPM anapaswa ajue kuwa Upinzani uliruhusiwa na Katiba mwaka 1992 wakti wa uhai wa Baba wa Taifa Nyerere(RIP)ambaye kwa hekima na busara alizojaliwa na Mungu alikubali MAWAZO YA WACHACHE WALIOTAKA MFUMO WA VYAMA VINGI ZIDI YA WENGI WALIOTAKA KUENDELEA NA MFUMO WA CHAMA KIMOJA!
Nashangaa kuna watu wanataka kumfananisha JPM na JKN sijui kwa sifa ipi hasa?Baba wa Taifa hakuchukia upinzani kama anavyofanya JPM kwa sasa hata kidogo! Anachofanya JPM ni dhambi ya UBAGUZI kwa kuwabagua wapinzani. Maneno ya Baba wa Taifa kuhusu ubaguzi ni kwamba hii ni dhambi mbaya sana sawa na kula nyama ya mtu ukionja huwezi kuacha! Hivo dhambi hii ya Ubaguzi anayoifanya JPM itamtafuna yeye na CCM yake ni swala la muda tu.
 
Yes mkuu Makoye 2009, sasa kuhusu uhusiano kati ya M7 na Kabila hapo ujafafanua vizuri mkuu, unauliza uhusiano wa kindugu/damu au wa kisiasa? Kitu kingine unataka tumzungumzie Kabila yupi? Kabila Jr au Sr fafanua kidogo mkuu.

Kabla ujajibu - mimi ntazungumzia Kabila Sr, yeye alikuwa mfuasi wa itikadi za Lumumba na alikuwa anampinga Mobutu hivyo akanzisha vita vya msituni vyenye lengo la kumuondoa madarakani Mobutu, operation zake kivita azikufanikiwa sana kutokana na kutokuwa commited 100% na vita vya ukombozi, alikuwa interested na mambo ya starehe na wanawake - weakness hii ilimsikitisha sana Mpiganaji Che Guevara ambaye wakati huo alikuwa ni Waziri chini ya Fidel Castro huko Cuba, lakini aliamua kuacha kazi na kuja Africa kwa siri na wanajeshi wachache kwa nia ya kuja kumsaidia Kabila kuwapa mafunzo wapiganaji wa Kabila katika msitu wa Congo alishiriki vile vile katika mapambano ya kuvizia dhidi ya jeshi la Mobutu chini ya ushauri wa CIA.

Che Guevara alikaa miezi tisa kama nakumbuka vizuri, lakini attitude za Kabila 2wards armed struggle zilimkatisha tamaa, straw ya mwisho ilitokea wakati walipo safiri kuja Dar kutoka porini DRC, walikuja kuchukua mizigo fulani na fedha zilizo kuwa donated na socialist countries kusaidia katika masuala ya ukombozi.

Kabila na Che walipo wasili Dar wakitokea Kigoma kwa Train kwa usalama wao wakawa wanalala hoteli tofauti, walikaa kwa muda wakifatilia kilicho waleta baada ya kufanikiwa - baadae walipanga siku ya kukutana kwa kupanga mikakati yao, siku waliyo panga kukutana Che aliondoka Hotel aliyofikia kwenda kukutana na Kabali Hotelini kwake, Che anaingia barabarani na kuanza kuembea kwa miguu ghafla anakutana na Kabila ameshikiria usukani wa Mercedes Benz i.e anaendesha!!! Che alishikwa na butwaa mwenzake kumbe peza anaziunguza kwenye matanuzi, siku nyingine wakakubaliana wakutane Hoteli aliyo fikia Che Guavara, kesho yake Che kasubiri wee Kabila aonekani!! Che kakata shauri kumfuata Kabila Hotelini, Che kufika Chumba cha Kabila alikuta mlango ajafungwa kwa ufunguo Che kufungua mlango akamkuta Kabila akiwa na wanawake watatu (sikumbuki vizuri) sijui wanne kitandani - Che kafunga mlango kwa nguvu na kuondoka zake huku amekasirika kweli kweli, baada ya siku chache kupita Che akahamua kurudi kwenye Msitu wa Congo kuwafuata wanajeshi aliyo kuja nao kutoka Cuba wakarudi wote Dar na kuondoka kurudi Cuba kupitia iliyokuwa Ujerumani Mashariki.

Kwenye simulizi zake Che anasema kwamba Kabila awezi ku-organise a credible fighting force kama atajidai kwamba anaweza basi hiyo itakuwa sawa sawa na ndoto za mchana, akasema tatizo lake ni kuendekeza sana starehe kuliko kutaka kuwakomboa Wafrica wenzake. Kwa kifupi kabisa hayo ndio maoni ya Che kuhusu Kabila Sr.

Sasa tuje uhusiano wa M7 na Kabila - again sijui unazungumzia Kabila yupi Sr au Jr - kama ni Kabila Sr - huyo aliwahi kuishi Uganda na familia yake under assumed name akiwa anaendeleza harakati zake za ukombozi huku akifanya biashara, sasa sijui walikuwa na ukaribu gani na M7 zaidi ya kupanga mbinu za kumuondoa madarakani Mobutu kwa kupigana vita kamili wakishirikiana na jeshi la PK, lakini wakati wanapanga hayo Kabila na familia yake alikwisha hamia Dar kwa miaka mingi akijiita Mfipa kwa jina ya O'Mutwale of course O'Mutwale ni Kiganda/Kinyankole/Kihaya kama sikosei.

M7 na Kabila Sr hawana undugu wowote walikuwa ni ma comrade in arm basi i.e wenye lengo moja kuingia madarakani kwa kutumia mtutu wa bunduki na walifanikiwa.

Tukienda mbali kidogo ni hivi: M7 ni Munyankole mwenye damu ya Kihima kama alivyo Mh.Kagame - wakati Kabila alikuwa Mkongomani wa mashariki ya Congo wenye asili ya kabila la Kimanyema kama walivyo baadhi ya wenyeji wa Kigoma, hivyo sidhani kama Kabila Sr ana damu ya Kihima hata kidogo.

Linapo kuja suala la
Kabila Jr (Rais wa sasa DRC) huyo is a different story iliyo ghubikwa na utata mtupu!!!. Nadhani nime eleweka mkuu.

Kiongozi Bukyanagandi,
Lazima tujue kuwa hizi nchi zetu za Kiafrika hasa ambazo zinapakana au ambaxo kwa namna moja au nyingine zilisaidiwa na Tanzania aidha kwenye maswala ya Armed struggle au ukombozi toka kwa mkolone au kuziondoa serikali za kidikteta kama ilvotokea Uganda wakti wa Nduli Amin, kulitokea mwingiliano wa kijamii wa Tanzania na mataifa hayo.Tanzania ilikuwa ni Hub ya vuguvugu la Ukombozi wa Mwafrika!
Ukifika huko Mazimbu Morogoro zilizokuwa kambi za waliokuwa wapigania Uhuru wa SA utakuta kuna elements za Kizulu na Kixhosa.
Ukienda huko Mtwara walipokuwa wanakaa wapigania Uhuru wa Mocambique kina marehemu Samora Machel hutakosa Wamekonde waliozaa na Wanamsumbiji,Wa angola n.k.
Ninachotaka kusema ni kwamba wote kina Museveni,Kabila Sr&Jr,Kagame,Samora Machel(RIP),Nelson Mandela(RIP),Robert Mugabe,n.k ni watu na mataifa yao ambao kwa vipindi fulani wamewahi kuishi Tanzania na kuwa na mahsiano ya kidugu kwa kuoa na kuoleana, hivo haya si mambo ya kushangaza hata kidogo!
 
Makoye post yako na comments zako zinakuondolea credibility ya kuwa mchambuz wa hili suala. Kwa kifupi AMASALA GAKO GALE NA MAKOYE KITE ELINA LYAKO.
 
Kwa hiyo magufuli ni nusu mtusi/chotara?
ila yaweza kuwa kweli maana kapua cha mheshimiwa kamechongoka sana kama wale waimba kwaya wa ambassadors
 
"Nahitimisha kwa kusema kuwa yawezekana kabisa tukianza kufuatilia babu wa babu wa babu wa John Pombe yawezekana ametokea hukohuko......!!!"

Nadhani ungesema hivi, tukianza kufuatilia babu wa babu wa babu wa Paul Kagame yawezekana ametokea kanda ya ziwa.
 
Wadau naomba mnisaidie kwanini raisi wetu amechagua mfumo wa uongozi wa Kagame nchini Rwanda? Nimeangalia imani ya Magufuli kwamba anaamini katika mtu badala ya mfumo,hii inatokana na sababu zifuatazo ambazo kwazo utwala wa Kagame unazizingatia sana

1.Haoni umuhimu wa mhimili huru wa bunge,kwani hakuifuata bajeti iliyopitishwa na bungr2016/17 na mara kwa mara ameingilia shughuli za bunge
2. Haoni umuhimu wa katiba,kwani mpaka sasa hajaruhusu mchakato wa katiba mpya kuendelea na utawala wake hauheshimu misingi ya katiba
3.Haoni umuhimu wa kutoa uwanja mpana wa demokrasia nchini.Pia hana shida na mapatano,majadiliano,na maafikiano ya vyama kuhusu mambo mbalimbaliyanayoikumba nchi.Mfano alikataa kupatanishwa na viongozi wa dini ktk suala la ukuta
4.Amejinasibu kuwa yeye ni mtawala asiyepangiwa cha kufanya na mtu yeyote na kwamba yeye ndie anayeamua chochote kwa wakati wowote atatakapojisikia inafaa

Sifa hizo zote ndizo alizonazo Kagame na hazijamsaidia kurudisha heshima ya Rwanda kimataifa.Huwezi linganisha sifa ya kuwa Mtanzania na kuwa Mrwanda kimataifa
Swali ;Je raisi anataka kuiporomosha hadhi ya Tanzania kama taifa lenye usalama na amani
Je, raisi anataka Tanzania iwe ni miongoni mwa nchi zenye migogoro ya kiutawala kama Rwanda na Burundi na hivyo kuingia kwenye migogoro na nchi wahisani wa maendeleo?
Kwanini raisi asijifunze kutoka nchi zenye maendeleo kisiasa na kiuchumi kama Kenya,Nigeria na nyinginezo aundio atasema tusimchagulie marafiki anaopaswa kuiga kutoka kwao?

Je kwanini
 
Ili upate majibu mazuri, tufafanulie hiyo conclusion kuwa Kagame ni role model wake umeitoa wapi? Kutaka watu wajadili mihemko yako binafsi sio fair.
 
Nimefuatilia sana hotuba za PK na kuona kwamba, jamaa anajitahidi sana kuuficha ubabe wake usionekane kwenye kauli zake. Tofauti na JM ambaye ubabe wake haufichiki kwa maneno yenye kauli tatanishi na vitendo.

Nini maoni yako?
 
We ni mnyarwanda?
Hiyo ni kwa sababu hakuna wa kuzirepot kauli hizo,

Vyombo vya habari vinaandika anachohariri yeye
 
Kuna tetesi kuwa Magufuli na Kagame hawakukutana barabarani uhusiano wao inasemekana waweze kuwa ni udugu wa damu!

Kwa asili Magufuli Pombe Joseph ni mtu anayetoka Kanda ya Ziwa maeneo yanayopakana kabisa na nchi za Rwanda, Burundi na Uganda. Katika mikoa hii ya Kigoma, Kagera kuna mwingiliano wa makabila ya ya Wahaya, Waha, Warundi, Wanyarwanda, Waganda, Wasukuma,Wazinza na Wanyambo.

Mpaka JPM ameingia kwenye Urais bado kabila lake rasmi haliko wazi. Kuna watu wanasema Magufuli ni Msukuma, wengine waasema ni Mzinza, wengine wanasema ni Mhaya au mchanganyiko wa Kisukuma na Kizinza!!!

Lakini kwa kasi ambayo Magufuli ameionyesha ya kuwa karibu sana na Rais Paul Kagame wa Rwanda imeanza kuleta hofu. Kuna uwezekano mkubwa wa Magufuli kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na wa kifamilia na Kagame. maana haingii akilini Rais huyu huyu Paul Kagame alikuwa na uadui na Rais mstahafu Kikwete kiasi cha kutishia amani ya nchi hizi mbili lakini leo imekuwa ni kinyume chake!! Kuna nini hapa?

Uwezekano wa Magufuli na Kagame kuwa na udugu uliotokana na mwuingiliano wa makabila ya mipaka ya Tanzania, Rwanda na Burundi ni mkubwa sana. Miaka ya nyuma kwenye 1960s na 1970s kulikuwa na wimbi kubwa sana la Warundi na Wanyarwanda waliokuwa wakija mikoa ya Mwanza, Kagera, Shinyanga kwa kazi za kilimo cha Pamba na kuchunga ng'ombe na pia katika mikoa ya Morogoro na Tanga kwa ajili ya Kilimo cha Mkonge na Miwa.

Mwingiliano huu ulifanya baadhi ya Warundi na Wasukuma kuoleana na hivo kuwa na damu mchanganyiko wa makabila haya. Nahitimisha kwa kusema kuwa yawezekana kabisa tukianza kufuatilia babu wa babu wa babu wa John Pombe yawezekana ametokea hukohuko......!!!
😂😂😂
 
Back
Top Bottom