Kikweli upweke unatesa sana watu wengi hawaelewi tu,
hata ujichanganye vipi na watu, mwisho wa siku utaingia ndani peke yako na upweke utakuvaa...
Fanya mazoezi pale unaporudi nyumbani kama huwezi jishughulishe na kitu chochote hata kufanya usafi ndani kwako.
Sali, ikijiweka karibu na Mola wako itakusaidia,
Soma vitabu hasa vya dini itakujenga kiimani na kujiona hauko peke yako,
Usipende sana kusikiliza nyimbo za huzuni, zinaongeza hali ya kijihisi mpweke.
Kama mpenzi wa movie, pendelea kuangalia movies za kuchekesha, kucheka kunaleta ahueni katika nafsi.
Pia waweza fanya matembezi ya jioni hata kwenda kula dinner mahali kuliko kula peke yako, kuona watu huko nje kutakufanya ukirudi nyumbani ufikirie matukio kadhaa uliyoyaona na kusahau upweke wako,
Jiunge na sites flani za kutafuta marafiki, huko utakutana na watu tofauti tofauti, mtashare stories na kusahau upweke wako.