Kwanza nenda shule ukajifunze kuandika jambo na kulipa shape ya kueleweka kwa wasomi na waelewa,nashukuru umesema una uelewa mdogo,lakini ndani ya CHADEMA kuna waelewa wengi tena chuo kikuu,jitahidi wakati mwingine waone wakusaidie ku-shape stori yako then leta humu.Humu kuna Great Thinkers kibao sasa unapokuja na uelewa wako mdogo unazidi kujiaibisha pamoja na kwamba una jambo muhimu!
La pili sikiliza wewe Dogo mwenye uelewa Mdogo,hakuna ubishi kwamba Chadema inakubalika Arusha,na hakuna Ubishi kwamba Chadema haiongozi Arusha,hilo liko wazi na kwa watu wenye akili kubwa na uelewa kama sisi tunalitambua hilo,isipokuwa tatizo ni kwamba hakuna amani Arusha.
Kwa maelezo yangu hapo juu na kwa nguvu iliyonayo CHADEMA mjini Arusha nilitegemea sana kupata matokeo chanya na viongozi wake walipaswa kutumia mwanya huo kuliweka jiji la Arusha katika ramani nzuri kwa sababu kuna faida nyingi kwenye jiji hilo na moja kubwa ni kwamba ni jiji linaloingilika sana na wageni kutoka nje ya nchi,sasa wangetumia kuweka kila kitu sawa ikiwa ni pamoja na siasa zake zinazoongozwa na Chadema ili wageni wapate la kusema.
Kibaya sana na kinachonishangaza ni kiwamba kila vurugu na mauaji ya watu ni lazima zitokee kwenye mkutano wa chadema,ok.yawezekana ni wapinzani wao CCM ndio wanaowafanyia hivyo ili waonekane wana vurugu,lakini kwa sababu kuna watu wengi ndani ya Chadema ni Great Thinker walipaswa kubadili mbinu na kutumia mbinu nyingine katika kufanya siasa zao.
Leo hii hata wageni wanaobahatika kuingia Arusha na kushuhudia matukio hayo,wanaondoka na sura kwamba Chadema ndio wakiorofi.nasema sipendi,sipendi sipendi kabisa.