Intellect
Member
- Apr 1, 2011
- 34
- 20
​Moja kati ya kero ambazo zimeutia dosari kubwa Muungano wa Jamuhuri ya Tanzania ni juu ya Mamlaka ya Mapato TRA.
Leo hii tumeshuhudia kamata kamata ya daladala na gari zote za biashara kwa kodi ya TRA, ambayo ni laki unusu kwa mwaka, sasa wiki hii ambayo ndio ilikuwa deadline ya kulipa kodi hiyo tangu january 2012 imesababisha kero kubwa kwa wakazi wa mkoa wa Mjini Magharibi kwa kukosekana kwa usafiri wa daladala barabarani. Wamiliki hawajalipa kodi hiyo ya TRA, kwa madai kwamba kodi zishakuwa nyingi, ZRB, insurance, Road license na sasa TRA utadhani gari ni mpya na atakayelipa baada ya tarehe 1 april atatakiwa kulipa faini ya 30,000/-Tsh
Hiki kimekua kilio cha muda mrefu na hapaonekani kuwepo jitihada mahususi ya kuondokana na kero hii hivyo wazanzibari wanaona ni bora Muungano uvunjwe ili kodi hii iondoke sambamba na kero nyingine nyingi!
Hiki kimekua kilio cha muda mrefu na hapaonekani kuwepo jitihada mahususi ya kuondokana na kero hii hivyo wazanzibari wanaona ni bora Muungano uvunjwe ili kodi hii iondoke sambamba na kero nyingine nyingi!