Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,210
- 829,203
Wengi tunapoongelea neno KINGA tunapeleka mawazo yetu moja kwa moja kwenye mipira ya kufanyia ngono yaani kondomu. Lakini wengine watadhani ni kinga dhidi ya maradhi ama kinga dhidi ya ajali barabarani na wezi majumbani huku wachache wakiwaza kinga dhidi ya watoto nknk. Akitokea mmoja akazungumzia kinga ya kiroho huyo itabidi umwangalie mara mbili kwakuwa si kawaida na si mazoea.
Tumekuzwa kwenye kuulinda mwili, kulinda vile vinavyoonekana, tunauhudumia mwili wa nyama uwe na siha njema, sura ivutie, nywele zivutie, nguo zikubali, tunaunywesha na kuulisha mwili wa nyama uharibikao na kusahau kabisa msingi wa kinachoufanya huo mwili uhudumiao uuhudumie.
Mwili dhaifu usio na kinga imara ni rahisi sana kushambuliwa na magonjwa mbalimbali, kuna watu haipiti mwezi kaugua hiki ama kile. Hawa automatically miili yao haina kinga thabiti. Ni watu wa spana mkononi kama gari bovu trip moja kazini, trip moja kwa fundi
Sasa mwili huohuo unaoweza kuwa na afya na siha njema usioshambuliwa na magonjwa ya mara kwa mara unaweza kuwa na upungufu mkubwa wa kinga za kiroho.
Pigo lolote likirushwa humpata yeye kama sio jini makhaba, basi ni zongo, kama sio zongo basi ni mapepo, kama sio mapepo basi ni chochote kibaya cha roho chafu kitampata.
Mtu mwenye upungufu wa kinga za kiroho mambo yake hayaendi kwenye stark, hayanyooki, hayasimami sawasawa, kama ni ajira inakuwa ngumu kupata, na akiipata hachelewi kuacha kuharibu ama kufukuzwa.. Kama ni biashara nuksi tupu, kama ni mahusiano balaa tupu, hakuna atakaloshika likakaa sawa.
Kuna vitu husababisha upungufu wa kinga za kiroho. Mungu (kwa wale waamini na waaminio) huleta duniani kiumbe kamili chenye kinga zote(usichanganye na wale watoto wa kichawi na majini) Lakini katikati ya harakati za maisha watu hupoteza ama kupunguza kinga zao kwa kwenda kwa waganga wa kienyeji, kuhangaika bila kuwa na msimamo wa kiimani, kufanyiwa mambo mabaya ma jirani ndugu ama rafiki.
Habari za kusafishwa nyota ama kupewa Pete za bahati ni vitu vibaya kabisa kiroho.
Habari za kuhangaika kwa waganga wa kienyeji ni kuzidi kujichafua kiroho na kujiharibia kabisa.. Yani mwili wako unakuwa kama punching bag, kila mtu anajaribu hapo.
Kutangatanga kiimani, mara huku mara kule unahangaisha bure roho yako na kuichosha sana mwisho inakuwa dhaifu kabisa
Jijengee msingi imara wa kinga ya kiroho kwa kubaki na imani moja bila kujali unaamini katika nini.
Pambana na hali yako kwa njia chanya. Kila mmoja wetu ana changamoto nyingi sana za maisha. Epuka nguvu hasi yoyote kwa manufaa binafsi. Unajiharibia.
Epuka epuka epuka kujihusisha na mambo ya giza huko huendi kutengeneza bali kujimaliza. Unafuu wake ni wa muda mfupi sana.
Wengi wanaohagaika leo wenye upungufu wa kinga za kiroho angalia historia zao wengi wamepitia hayo hapo juu. Simama na Mungu wako ujenge kinga imara ya kiroho.
Tumekuzwa kwenye kuulinda mwili, kulinda vile vinavyoonekana, tunauhudumia mwili wa nyama uwe na siha njema, sura ivutie, nywele zivutie, nguo zikubali, tunaunywesha na kuulisha mwili wa nyama uharibikao na kusahau kabisa msingi wa kinachoufanya huo mwili uhudumiao uuhudumie.
Mwili dhaifu usio na kinga imara ni rahisi sana kushambuliwa na magonjwa mbalimbali, kuna watu haipiti mwezi kaugua hiki ama kile. Hawa automatically miili yao haina kinga thabiti. Ni watu wa spana mkononi kama gari bovu trip moja kazini, trip moja kwa fundi
Sasa mwili huohuo unaoweza kuwa na afya na siha njema usioshambuliwa na magonjwa ya mara kwa mara unaweza kuwa na upungufu mkubwa wa kinga za kiroho.
Pigo lolote likirushwa humpata yeye kama sio jini makhaba, basi ni zongo, kama sio zongo basi ni mapepo, kama sio mapepo basi ni chochote kibaya cha roho chafu kitampata.
Mtu mwenye upungufu wa kinga za kiroho mambo yake hayaendi kwenye stark, hayanyooki, hayasimami sawasawa, kama ni ajira inakuwa ngumu kupata, na akiipata hachelewi kuacha kuharibu ama kufukuzwa.. Kama ni biashara nuksi tupu, kama ni mahusiano balaa tupu, hakuna atakaloshika likakaa sawa.
Kuna vitu husababisha upungufu wa kinga za kiroho. Mungu (kwa wale waamini na waaminio) huleta duniani kiumbe kamili chenye kinga zote(usichanganye na wale watoto wa kichawi na majini) Lakini katikati ya harakati za maisha watu hupoteza ama kupunguza kinga zao kwa kwenda kwa waganga wa kienyeji, kuhangaika bila kuwa na msimamo wa kiimani, kufanyiwa mambo mabaya ma jirani ndugu ama rafiki.
Habari za kusafishwa nyota ama kupewa Pete za bahati ni vitu vibaya kabisa kiroho.
Habari za kuhangaika kwa waganga wa kienyeji ni kuzidi kujichafua kiroho na kujiharibia kabisa.. Yani mwili wako unakuwa kama punching bag, kila mtu anajaribu hapo.
Kutangatanga kiimani, mara huku mara kule unahangaisha bure roho yako na kuichosha sana mwisho inakuwa dhaifu kabisa
Jijengee msingi imara wa kinga ya kiroho kwa kubaki na imani moja bila kujali unaamini katika nini.
Pambana na hali yako kwa njia chanya. Kila mmoja wetu ana changamoto nyingi sana za maisha. Epuka nguvu hasi yoyote kwa manufaa binafsi. Unajiharibia.
Epuka epuka epuka kujihusisha na mambo ya giza huko huendi kutengeneza bali kujimaliza. Unafuu wake ni wa muda mfupi sana.
Wengi wanaohagaika leo wenye upungufu wa kinga za kiroho angalia historia zao wengi wamepitia hayo hapo juu. Simama na Mungu wako ujenge kinga imara ya kiroho.
