Upotoshaji Wikipedia Juu ya Nyerere?

Inashangaza sana Nyerere huyo huyo ndiye Rais pekee wa Tanzania aliyetoa hukumu ya kunyongwa kwa mtu mmoja tu Mwamwindi wa Iringa alimuua Kileluu aliyekuwa mkuu wa mkoa huo na akawaacha kwa mamia bila kuwanyonga japo walihukumiwa kunyongwa na Mahakama.
 
mbona wakoloni hawajaandika wikipedia waliuua wangapi Afrika?

Nyerere kama alikuwa mbaya sana mbona alifanya harakati kubwa kuzikomboa nchi za kusini mwa Afrika ambako Waafika mamilioni waliuuawa wakati wa vita vya ukombozi?
 
Angalia Sasa ...Mnaenda kubishania Kwenye Wikipedia sasa...wabongo msijue kitu sijui Bongo Lala Gani ? Aloenda edit na kuanza kuuliza Maswali, kule Hakuulizwi maswali ni Majibu...acheni ushamba ukijua kitu wakati mwingine hata Mnakaa Kimya nayo ikatosha, sasa mtawa misleadin hata wengine wasiojua chochote

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Nyerere kama alikuwa mbaya sana mbona alifanya harakati kubwa kuzikomboa nchi za kusini mwa Afrika ambako Waafika mamilioni waliuuawa wakati wa vita vya ukombozi?
Labda Waingereza waliokuwa wakimuongoza na kumuendesha walimwambia kuwa ndio njia pekee ya kutoka.
 
Historia itabaki kuwa ni historia tu, hata kama ikipindishwa nayo itakuwa siku moja kuwa historia iliyopindishwa!. Hiyo ndiyo sheria ya historia!
 
ukweli unauma.....

Nyelele arikuwa mtu mzuli sana, wakati wa Nyelele aliimalisha sana hari ya watu wake kierimu na rishe bola, vyakura kama mahalage

mchere, sukali, virikuwa vikipatikana kira kona ya Jamhuli ya Tanzania

Watanzania hawahitaji mitandao kujua wakati gani sukari,mchele,unga ulikuwa haupatikani mpaka watu wapange foleni baada ya kupata kibali cha balozi wa nuymba kumi,wanafaham ni wakati gani kumiliki Tv,Fridge lilikuwa kosa la jinai,wanakumbuka ni wakati gani unakamatwa kwa kuvaa nguo nzuri kwa kigezo eti zimetoka nje,wanakumbuka utawala upi ilikuwa kujitafutia kifo kukosoa watawala, historia iliyopindishwa kwa kalam itanyooshwa kwa simulizi za mdomo
 
Nyerere wa Wikipedia atabaki kuwa wa hukohuko. Nyerere wa WATANZANIA, tulieishi naye, tukafanyakazi naye, tukamsoma, tukamsikiliza, akafariki, tukamzika atabaki kama tulivyomwona na kumfahamu.
Hivyo hukumjua Nyerere wewe! na ulikuwa humsikilizi Nyerere kwa sababu hotuba zake, barua zake kwenda kwa viongozi wa nje na nini afanye vyote hivi alikuwa akipangiwa na raia wa Kiingereza Joan Wicken mwenye asili ya Kiyahudi.
Joan Wicken alikuwa akiitumikia na kulipwa na Serikali ya Uingereza "kumshauri" Nyerere tokea kabla ya Uhuru mpaka kufa kwa Nyerere, ni great thinker wewe fanya utafiti kidogo kuhusu huyu mwanamke Joan Wicken na Nyerere.
Wakati ulipokuwa ukiimba "zidumu fikra za Mwenyekiti" ujue kuwa ulikuwa ukiimba zidumu fikra za Joan! Umetiwa changa la macho mkuu! pole.
 
ukweli unauma.....

Nyelele arikuwa mtu mzuli sana, wakati wa Nyelele aliimalisha sana hari ya watu wake kierimu na rishe bola, vyakura kama mahalage

mchere, sukali, virikuwa vikipatikana kira kona ya Jamhuli ya Tanzania

Hebu check kwenye red unafanya makusudi au ndio uelewa wako wa kiswahili?
 
Siwezi kukuzuia kufikiri na kuandika hivi na hasa kama unaongozwa na chuki, jazba, husda, fitna, DINI, ..., Nyerere wetu alikuwa muwazi sana katika utendaji wake kazi. Hakucheka na aliyemchukia. Hakuwa mnafiki kwa yeyote. Hotuba zake nyingi alizungumza kwa kichwa na akili yake. Alisimamie kwelikweli lile aliloamini ni SAHIHI na ni kwa manufaa ya WATANZANIA.
 

Ukitaka kumuongelea Nyerere lazima uwe na kichwa kigumu kama jiwe...ndio jamaa zangu wanapojifunzia shabaha ingawa so far hakuna aliyemgusa kwa kukosa umakini.
 

ala kumbe zilikuwa fikra za kizungu!
 
Kwa hiyo Joan Wicken aliyekuwa akilipwa na Waingereza ndiye aliyemshauri Nyerere miaka ya Sitini kuvunja mahusiano ya kibalozi na Uingereza kwa vile Uingereza ilikuwa inamsapoti Ian Smith wa Rhodesia (Zimbabwe)? Kweli tunapenda kutengeneza uongo kuwa ukweli.
 


CAN YOU Mention those PRISONER's? It sometimes Propaganda... NO ONE WAS Imprisoned by NYERERE in 1962

He was not even ruling the country as the PM was Rashid Kawawa; He took Over Afterwards as the Republic President
Hii ni kweli kabisa wala haina marekebisho kuna kina Chipaka,Zuberi Mtemvu kina Chifu Mareale kina Fundikira,Abdulrahman Babu,wengine wengi walikimbia nchi kama kina Kambona wengine walifukuzwa jeshini na kuzuiwa nyumbani kama kina Bob Nasser(Nasari).Mahfudhi wengine wakapewa kazi nyingine uraiani lakini kwa masharti kama kina Capt.Mushi huyu mwenye malori mengi mfadhili wa Simba jina simkumbuki alikuwa meneja kampuni ya KAMATA na wengine wengi sana siwakumbuki majina yao,wako waliofia gerezani kwa mateso,lakini hayo hayazungumzwi,hiyo ndiyo taswira ya Mwl.Nyerere kwa upande wa pili,tusipende kuongelea mazuri tu,hata mabaya yapo mengi tena ya kutisha.
 
Chakaza,
Anayekutukana hakuchagulii tusi. Kale kamama ka kizungu kalikuwa kaadilifu na kachapakazi sana tu. Mwalimu alibaki nako kwa ajili ya sifa hizo tu na kwa kweli hakukosea.
 
Nyerere wa Wikipedia atabaki kuwa wa hukohuko. Nyerere wa WATANZANIA, tulieishi naye, tukafanyakazi naye, tukamsoma, tukamsikiliza, akafariki, tukamzika atabaki kama tulivyomwona na kumfahamu.

Na ukweli hauwezi kuchakachuliwa na wajanja wajanja wachache
 
Hizo ni propaganda za Wikipedia! By the way Wiki is not a reliable source it is just a ****!
Wawataje angalau watu wawili waliopotezwa na Nyerere
 

I see.
Tatizo ni kuwa kuna watu hapa, kuongea na kusambaza uongo si dhambi katika dini yao. Kwa hiyo andikeni mnavyotaka, danganyeni, mnavyoweza, lakini ukweli kuhusu Nyerere upo na utabaki. Alikuwa kiongozi bora. Dunia nzima tunajua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…