Ni upotoshaji wa kiwango cha juu na sijui kwa nini watu mnaendelea kuijadili kwa sababu mwaka 1962 Julius Nyerere hakuwa madarakani.
Alijiuzuru u-Prime Minister January 22, 1962 yaani siku 22 tu baada ya kuuanza mwaka, akabaki kama mbunge tu hadi aliapishwa kuwa Rais wa Tanganyika December 09, 1962 yaani zikiwa zimebaki siku 23 kabla ya kuumaliza mwaka.
Hivyo, jumla ya siku alizokuwa madarakani mwaka huo ni 22+23=45. Hivyo (45/365)x100%=9.59%. Hivyo alitumia asilimia 9.59% tu ya muda wa mwaka huo kuwa madarakani.
Kuhusu Wikipedia, binafsi nimeiamini sana siku za mwanzo, lakini baada ya mimi kuweza ku-edit post kadhaa kwenye wikipedia nikaondoa imani ya kuitegemea sana kwani kama mimi nimeweza basi kila mmoja anaweza hata anayesema uongo.
Kinachosaidid kwenye Wikipedia ni kwamba uongo ni rahisi kutambulika na kurekebishwa haraka. Lakini mimi binafsi tangu wakati huo, Wikipedia naiweka kama second priority na ndiyo maana ninategemea sana vitabu na publications nyingi maana huko mtu anakuwa responsible na anachoandika.