Upotevu mkubwa wa pesa NECTA

Upotevu mkubwa wa pesa NECTA

usiniguse

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
1,725
Reaction score
1,194
Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi, kwanini nasema hivi?

Fikiria mitihani ya kidato cha 4 imeanza tarehe 2/11/2015 na mpaka sasa inaendelea kwa baadhi ya shule hasa zenye watahiniwa wa kujitegemea.

NECTA imelipa wasimamizi, wakuu wa shule na maaskari posho za siku zote za mitihani, hapa hakuna shida. Tatizo linakuja hapa; Ndani ya wiki mbili NECTA tena inaendesha mitihani ya kidato cha pili FTSEE na kulipa posho nyingine kwa kiwango kile kile kwa watu wengine tofauti na wakuu washule mara mbili.

Taarifa nilizonazo wilaya yenye shule chache za sekondari kwa kidato cha 4 bajeti ni karibia shilingi 90 milioni na kidato cha pili 60 milioni. Sasa kwa wilaya zenye shule nyingi na wanafunzi wengi ni shilingi ngapi? mara inchi nzima.

Hivi hawa NECTA wasingeweza kuiendesha hii mitihani kwa kwa kipindi kimoja na kuweza kuokoa mabilioni ya pesa ,kwani wangefanya semina moja, wasimamizi walewale na askari walewale,wakuu wa shule wangelipwa siku zilezile lakini sasa wanalipwa mara mbili halafu mitihani inakutana

 
Kwani mkuu wewe wakati unasoma mlifanya mtihani kipindi kimoja kama unavyotaka?
 
huwezi kuendesha hiyo mitihani kwa wakati mmoja,walimu ni wachache,askari pia ni wachache.elewa kuwa mwalimu aliyesimamia form four ndie huyo huyo anatakiwa kusimia form two,tahossa na kicoses.pia huyo huyo anatakiwa kusahisha mtihani wa tahossa,kicoses,form two na form four,unategemea atajigawaje? shule nyingi walishamaliza mitihani ya form four labda tu kwa zile zenye PC(private candidate) kama green acres,perfect vision na mbezi high ndio zinaenda muda mrefu mpaka tarehe 27 mwez huu,lakn shule zetu za kata na jumuiya ya wazazi(shule zinazomilikiwa na ccm kama tegeta high) hizi zimeshamaliza mitihani na ni chache sana ambazo hazijamaliza.
 
Mtoa mada nadhani kuna mambo hukuyachunguza
1. Shule nyingi za kata zina wastani wa vyumba vya madarasa 14 hadi 15.Ukivigawa kwa idadi ya wanatahiniwa 35 hadi 40 kwa kila chumba utagundua madarasa yote yatatumiwa kwa mitihani tu.Hiyo itafanya form 1 na 3 kukosa madarasa kwa kipindi chote cha mitihani.

2. Kwa wastani kwa shule moja idadi ya walimu kama 10 hivi hushiriki zoezi la usimamizi wa mitihani.Ikifanyika yote kama unavyotaka wewe ina maana idadi Mara mbili ya hiyo itashiriki kwenye usimamizi.Hapo ina maana form 1&3 watakosa walimu(hawatafundishwa).

3. Kuna masuala matatu ambayo huendeshwa kwa unyeti wa hali ya juu hasa katika mambo ya kiusalama...uchaguzi,mwenge na mitihani Taifa. Kuiweka mitihani yote pamoja inaleta hatari kiusimaizi na kiusalama maana manpower ni issue.

4. Usihofie gharama za uendeshaji kwa zoezi ambalo kwa unyeti wake likiharibika linagharimu zaidi na linaleta hasara zaidi.
 
Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi, kwanini nasema hivi?

Fikiria mitihani ya kidato cha 4 imeanza tarehe 2/11/2015 na mpaka sasa inaendelea kwa baadhi ya shule hasa zenye watahiniwa wa kujitegemea.

NECTA imelipa wasimamizi, wakuu wa shule na maaskari posho za siku zote za mitihani, hapa hakuna shida. Tatizo linakuja hapa; Ndani ya wiki mbili NECTA tena inaendesha mitihani ya kidato cha pili FTSEE na kulipa posho nyingine kwa kiwango kile kile kwa watu wengine tofauti na wakuu washule mara mbili.

Taarifa nilizonazo wilaya yenye shule chache za sekondari kwa kidato cha 4 bajeti ni karibia shilingi 90 milioni na kidato cha pili 60 milioni. Sasa kwa wilaya zenye shule nyingi na wanafunzi wengi ni shilingi ngapi? mara inchi nzima.

Hivi hawa NECTA wasingeweza kuiendesha hii mitihani kwa kwa kipindi kimoja na kuweza kuokoa mabilioni ya pesa ,kwani wangefanya semina moja, wasimamizi walewale na askari walewale,wakuu wa shule wangelipwa siku zilezile lakini sasa wanalipwa mara mbili halafu mitihani inakutana


Aisee hoja dhaifu sana...unadhani ni simple yaani shule 1 kuhandle mitihani zote kwa wastani wa darasa 1 kwa 35 students
 
Posssibles chukua likes zangu zote.hayo ndo majibu yake ,Mitihani ya necta sio gwaride wala halaiki
 
Mtoa mada nadhani kuna mambo hukuyachunguza
1. Shule nyingi za kata zina wastani wa vyumba vya madarasa 14 hadi 15.Ukivigawa kwa idadi ya wanatahiniwa 35 hadi 40 kwa kila chumba utagundua madarasa yote yatatumiwa kwa mitihani tu.Hiyo itafanya form 1 na 3 kukosa madarasa kwa kipindi chote cha mitihani.

2. Kwa wastani kwa shule moja idadi ya walimu kama 10 hivi hushiriki zoezi la usimamizi wa mitihani.Ikifanyika yote kama unavyotaka wewe ina maana idadi Mara mbili ya hiyo itashiriki kwenye usimamizi.Hapo ina maana form 1&3 watakosa walimu(hawatafundishwa).

3. Kuna masuala matatu ambayo huendeshwa kwa unyeti wa hali ya juu hasa katika mambo ya kiusalama...uchaguzi,mwenge na mitihani Taifa. Kuiweka mitihani yote pamoja inaleta hatari kiusimaizi na kiusalama maana manpower ni issue.

4. Usihofie gharama za uendeshaji kwa zoezi ambalo kwa unyeti wake likiharibika linagharimu zaidi na linaleta hasara zaidi.

safi sana mkuu,umefanya uchambuzi makini na wenye kueleweka.
 
umemjibu vizuri sana.

vilevile akumbuke kuwa hiyo mitihani inaendeshwa na Taasisi mbili Tofauti. NECTA wanasimamia Mitihani ya Kidato cha NNe wakati Ukaguzi kanda wanasimamia Mitihani ya Kidato cha Pili. Nadhani kwahoja huzo atakuwa ameelewa.
Mtoa mada nadhani kuna mambo hukuyachunguza
1. Shule nyingi za kata zina wastani wa vyumba vya madarasa 14 hadi 15.Ukivigawa kwa idadi ya wanatahiniwa 35 hadi 40 kwa kila chumba utagundua madarasa yote yatatumiwa kwa mitihani tu.Hiyo itafanya form 1 na 3 kukosa madarasa kwa kipindi chote cha mitihani.

2. Kwa wastani kwa shule moja idadi ya walimu kama 10 hivi hushiriki zoezi la usimamizi wa mitihani.Ikifanyika yote kama unavyotaka wewe ina maana idadi Mara mbili ya hiyo itashiriki kwenye usimamizi.Hapo ina maana form 1&3 watakosa walimu(hawatafundishwa).

3. Kuna masuala matatu ambayo huendeshwa kwa unyeti wa hali ya juu hasa katika mambo ya kiusalama...uchaguzi,mwenge na mitihani Taifa. Kuiweka mitihani yote pamoja inaleta hatari kiusimaizi na kiusalama maana manpower ni issue.

4. Usihofie gharama za uendeshaji kwa zoezi ambalo kwa unyeti wake likiharibika linagharimu zaidi na linaleta hasara zaidi.
 
wengi wamekupa majibu sahihi hasa suala ya man power na vyumba vya kufanyika kazi. Hata Hivyo utambuwe kuwa Mitihani hiyo haisimamiwi na NECTA yote. NECTA wanasimamia mtihani wa Kidato cha Nne wakati Ukaguzi Kanda wanasimamia Mtihani wa Kidato cha Pili.
Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi, kwanini nasema hivi?

Fikiria mitihani ya kidato cha 4 imeanza tarehe 2/11/2015 na mpaka sasa inaendelea kwa baadhi ya shule hasa zenye watahiniwa wa kujitegemea.

NECTA imelipa wasimamizi, wakuu wa shule na maaskari posho za siku zote za mitihani, hapa hakuna shida. Tatizo linakuja hapa; Ndani ya wiki mbili NECTA tena inaendesha mitihani ya kidato cha pili FTSEE na kulipa posho nyingine kwa kiwango kile kile kwa watu wengine tofauti na wakuu washule mara mbili.

Taarifa nilizonazo wilaya yenye shule chache za sekondari kwa kidato cha 4 bajeti ni karibia shilingi 90 milioni na kidato cha pili 60 milioni. Sasa kwa wilaya zenye shule nyingi na wanafunzi wengi ni shilingi ngapi? mara inchi nzima.

Hivi hawa NECTA wasingeweza kuiendesha hii mitihani kwa kwa kipindi kimoja na kuweza kuokoa mabilioni ya pesa ,kwani wangefanya semina moja, wasimamizi walewale na askari walewale,wakuu wa shule wangelipwa siku zilezile lakini sasa wanalipwa mara mbili halafu mitihani inakutana

 
Haiwezekani kuendesha mituhani tote kwa pamoja coz shule nyingi miundo mbinu yake haiko vizuri nikiwa na maana ya samani, vyumba vya kufanyia mitihan hiyo nk. Hvyo wanachokifanya necta ni sahihi. Na km unaona Elimu ni ghali basis jaribu ujinga
 
wengi wamekupa majibu sahihi hasa suala ya man power na vyumba vya kufanyika kazi. Hata Hivyo utambuwe kuwa Mitihani hiyo haisimamiwi na NECTA yote. NECTA wanasimamia mtihani wa Kidato cha Nne wakati Ukaguzi Kanda wanasimamia Mtihani wa Kidato cha Pili.
Kiongozi nikusahihishe kidogo kama hutojali. Kuanzia mwaka huu 2015 mitihani yote ya Taifa (kuanzia ya darasa la nne mpaka kidato cha 6) imewekwa chini ya usimamizi wa NECTA. Sababu kuu ni kwamba NECTA ndio yenye wajibu na mamlaka ya kutahini wanafunzi......Wizara ya elimu kwa kushirikiana na TAMISEMI imebaki na jukumu la kuandaa wanafunzi na mazingira ya kufundishia....ukaguzi wamebaki na majukumu ya kukagua mwenenndo wa utoaji elimu na mazingira yake......TIE imebaki na majukumu yake ya evaluations na ukuzaji mitaala.

Na kwahiyo utaona hata mitihani ya Form 2 mwaka huu imetungwa na NECTA na itasahihishwa kitaifa kwenye vyuo na taasisi mbalimbali baadhi ni Ndanda, Uyole, Mandaka n.k. na watatumia wiki 2 tu.
Usahihishaji wa kidato cha nne nao uanfanyika kama ilivyokuwa kabla na utaenda sambamba na wa kidato cha pili isipokuwa wao watatumia vyuo tofauti na watachukua zaidi ya wiki 2 kumaliza kazi.
 
umemjibu vizuri sana.

vilevile akumbuke kuwa hiyo mitihani inaendeshwa na Taasisi mbili Tofauti. NECTA wanasimamia Mitihani ya Kidato cha NNe wakati Ukaguzi kanda wanasimamia Mitihani ya Kidato cha Pili. Nadhani kwahoja huzo atakuwa ameelewa.

Mitihani yote ni NECTA, hyo ya ukaguzi haipo .
 
Back
Top Bottom