Abuhunna
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 409
- 233
Mtoa mada nadhani kuna mambo hukuyachunguza
1. Shule nyingi za kata zina wastani wa vyumba vya madarasa 14 hadi 15.Ukivigawa kwa idadi ya wanatahiniwa 35 hadi 40 kwa kila chumba utagundua madarasa yote yatatumiwa kwa mitihani tu.Hiyo itafanya form 1 na 3 kukosa madarasa kwa kipindi chote cha mitihani.
2. Kwa wastani kwa shule moja idadi ya walimu kama 10 hivi hushiriki zoezi la usimamizi wa mitihani.Ikifanyika yote kama unavyotaka wewe ina maana idadi Mara mbili ya hiyo itashiriki kwenye usimamizi.Hapo ina maana form 1&3 watakosa walimu(hawatafundishwa).
3. Kuna masuala matatu ambayo huendeshwa kwa unyeti wa hali ya juu hasa katika mambo ya kiusalama...uchaguzi,mwenge na mitihani Taifa. Kuiweka mitihani yote pamoja inaleta hatari kiusimaizi na kiusalama maana manpower ni issue.
4. Usihofie gharama za uendeshaji kwa zoezi ambalo kwa unyeti wake likiharibika linagharimu zaidi na linaleta hasara zaidi.
Umemjibu, litafakari jambo kabla ya kukurupuka