Upinzani wa Tanzania umewafanya watanzania kushiriki ‘utoto wao wa kisiasa’,hii ni fedheha na aibu kwa watanzania

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Apr 10, 2019
2,590
4,601
Bado ubongo wangu unatafakari mengi sana juu ya upinzani wa Tanzania ambao umefikia mahali kuonekana ni chombo cha kuhamasisha ajenda za siri ambazo watanzania hawakubaliani nazo. Sura ya kwanza ya upinzani watanzania tuliujua kama wa maandamano na migomo lakini miaka hii michache ya Rais Magufuli umetusaidia kuujua upinzani katika sura ya pili ambayo hatukubahatika kuijua hapo kabla. Sura ya pili ya upinzani ambayo INABEZA, INALAUMU, INAPINGA kila jitihada chanya za serikali ya nchi hii.

Nikiendelea kutafakari Zaidi najikuta katika wimbi zito la kufikiri, kuwaza na kuwazua ni nini wapinzani wanataka serikali ifanye kwa ajili ya watanzani ? watanzania tulio wengi tunaona matokeo ya maamuzi tuliyofanya mwaka 2015 ya kumchagua Rais Magufuli kuwa Rais wetu , ni maamuzi yenye tija, ya hekima na busara nyingi. Rais ambaye anatekeleza aliyoahidi na anafanya yale wapinzani waliyokuwa wanayasema ni fahari kubwa watanzania.

Katika hili la kupinga na kubeza kila kitu, upinzani umekuwa tatizo kwa watanzania kusonga mbele. Ni hakika kabisa mpinzani wa kweli kutoka CHADEMA alikuwa ni Dkt.Slaa tu kwa sababu ameamua kuachana na utoto wa kisiasa wa CHADEMA wa kupinga yale aliyokuwa anayaamini na kuamua kuwa upande ule ambao unayafanya kwa vitendo nao ni CCM.

Aibu gani hii? Fedheha ya namna gani hii kwa watanzania? Hakika watanzania kuendelea kukumbatia upinzani huu usio na malengo ni kujirudisha nyuma enzi za ujima na ukabaila , enzi ambazo maendeleo yalikuwa hafifu. Watanzania wa sasa wanataka maendeleo ya kasi ya viwanda, kilimo, elimu, miundombinu , afya na uvuvi na kiongozi tuliyenaye sasa anajua mahitaji ya watanzania na anajitahidi kufanikisha kuyatimiza hata kama si kwa asilimia 100 ila kwa kiwango alichofikia tunaweza kusema maendeleo ya Tanzania yapo juu.

Kwa nini watanzania waendelee kushiriki utoto wa kisiasa wakati dira na muelekeo wa maendeleo chini ya Rais Magufuli ni mzuri na wenye nuru kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Utoto wa kisiasa wa upinzani uliwatumbukiza watanzania kwenye siasa za matukio na purukushani badala ya siasa za utendaji ambazo kwa hakika awamu hii ya tano umezianika wazi.
 
Akili zako zinakusaidia kuvukia barabara Tu hivi umeshawahi kujiuliza tokea vyama vingi vimeanzishwa 1992 Hadi leo ni wabunge na madiwani wangapi wa upinzani wamechaguliwa?..
Wewe mlamba miguu hujui lolote Ila raisi wenu,katibu wenu wa chama wanajua kuwa siku watakayoruhusu tume huru ya uchaguzi basi kaburi Lao tutawafukia rasmi

Badilisheni katiba iliyopo alafu tuipitishe Ile katiba pendekezwa ya jaji warioba utaona kitachowakuta!!!!
 
Bado ubongo wangu unatafakari mengi sana juu ya upinzani wa Tanzania ambao umefikia mahali kuonekana ni chombo cha kuhamasisha ajenda za siri ambazo watanzania hawakubaliani nazo. Sura ya kwanza ya upinzani watanzania tuliujua kama wa maandamano na migomo lakini miaka hii michache ya Rais Magufuli umetusaidia kuujua upinzani katika sura ya pili ambayo hatukubahatika kuijua hapo kabla. Sura ya pili ya upinzani ambayo INABEZA, INALAUMU, INAPINGA kila jitihada chanya za serikali ya nchi hii.

Bahati mbaya sana sijuhi umjezaliw alini ila tokea siku ya kwanza demokrasia iliporuhusiwa nchi hii, MACCM yamekuwa yakijitahidi kuu Brand like that, kikubwa ni kuwa MACCM yameshindwa vibaya sana kwenye hilo.
 
Umejiona umeandika kwelikweli..!

Mshauri basi Magufuli arudishe mfumo wa chama kimoja ili huu "utoto" uishe!
 
Kama si waoga ruhusu mikutano na uhuru wa habari uone ukweli!!
Mmeuwa uchumi biashara bei za mazao hovyo, hakuna la maana.
Watu kupotea kupigwa risasi kuuwawa kwenu ni kawaida, hamna aibu.
Acha ukatili sio asili ya Tanzania!!
 
Asante kwa kushangaa kwanini watanzania wanaendelea kuupenda upinzani!Endelea kutafakari na kushangaa!
 
Acha kutoa rushwa kununua wabunge na madiwani!!
Mnafunika kichwa mchangani kama mbuni kiwiliwili kiko nje hakuna siri ndg mfanyayo yote yako wazi!!
 
Upinzani wa Tanzania ufumuliwe. Unahitaji watu wapya, akili mpya na maono mapya. Hii itachukua si chini ya miaka 10.
 
Upinzani wa Tanzania umewafanya watanzania kushiriki ‘utoto wao wa kisiasa’,hii ni fedheha na aibu kwa watanzania
Usiwe na wasi wasi, ongezeni tu spidi na juhudi katika kuteka, kutesa, kutwanga risasi an kupoteza wanaowakosoa. Muda is mrefu mtabaki peke yenu na hapo ndipo mtagundua umuhimu wa upinzani!
 
Bado ubongo wangu unatafakari mengi sana juu ya upinzani wa Tanzania ambao umefikia mahali kuonekana ni chombo cha kuhamasisha ajenda za siri ambazo watanzania hawakubaliani nazo. Sura ya kwanza ya upinzani watanzania tuliujua kama wa maandamano na migomo lakini miaka hii michache ya Rais Magufuli umetusaidia kuujua upinzani katika sura ya pili ambayo hatukubahatika kuijua hapo kabla. Sura ya pili ya upinzani ambayo INABEZA, INALAUMU, INAPINGA kila jitihada chanya za serikali ya nchi hii.

Nikiendelea kutafakari Zaidi najikuta katika wimbi zito la kufikiri, kuwaza na kuwazua ni nini wapinzani wanataka serikali ifanye kwa ajili ya watanzani ? watanzania tulio wengi tunaona matokeo ya maamuzi tuliyofanya mwaka 2015 ya kumchagua Rais Magufuli kuwa Rais wetu , ni maamuzi yenye tija, ya hekima na busara nyingi. Rais ambaye anatekeleza aliyoahidi na anafanya yale wapinzani waliyokuwa wanayasema ni fahari kubwa watanzania.

Katika hili la kupinga na kubeza kila kitu, upinzani umekuwa tatizo kwa watanzania kusonga mbele. Ni hakika kabisa mpinzani wa kweli kutoka CHADEMA alikuwa ni Dkt.Slaa tu kwa sababu ameamua kuachana na utoto wa kisiasa wa CHADEMA wa kupinga yale aliyokuwa anayaamini na kuamua kuwa upande ule ambao unayafanya kwa vitendo nao ni CCM.

Aibu gani hii? Fedheha ya namna gani hii kwa watanzania? Hakika watanzania kuendelea kukumbatia upinzani huu usio na malengo ni kujirudisha nyuma enzi za ujima na ukabaila , enzi ambazo maendeleo yalikuwa hafifu. Watanzania wa sasa wanataka maendeleo ya kasi ya viwanda, kilimo, elimu, miundombinu , afya na uvuvi na kiongozi tuliyenaye sasa anajua mahitaji ya watanzania na anajitahidi kufanikisha kuyatimiza hata kama si kwa asilimia 100 ila kwa kiwango alichofikia tunaweza kusema maendeleo ya Tanzania yapo juu.

Kwa nini watanzania waendelee kushiriki utoto wa kisiasa wakati dira na muelekeo wa maendeleo chini ya Rais Magufuli ni mzuri na wenye nuru kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Utoto wa kisiasa wa upinzani uliwatumbukiza watanzania kwenye siasa za matukio na purukushani badala ya siasa za utendaji ambazo kwa hakika awamu hii ya tano umezianika wazi.
Ulipaswa wewe ndio ujishangae kwa nini una akili tofauti na wenye akili timamu?
Jee ni ujinga? au ushabiki? Au vyote pamoja?
 
Unaandika chapisho refu lakini huna uandishi mzuri, na hata propaganda zako haziendani.
 
Akili zako zinakusaidia kuvukia barabara Tu hivi umeshawahi kujiuliza tokea vyama vingi vimeanzishwa 1992 Hadi leo ni wabunge na madiwani wangapi wa upinzani wamechaguliwa?..
Wewe mlamba miguu hujui lolote Ila raisi wenu,katibu wenu wa chama wanajua kuwa siku watakayoruhusu tume huru ya uchaguzi basi kaburi Lao tutawafukia rasmi

Badilisheni katiba iliyopo alafu tuipitishe Ile katiba pendekezwa ya jaji warioba utaona kitachowakuta!!!!
Hiyo ilikuwa ni wakati ule siyo sasa! Ni wakati ule Dr. Silaa bado ni katibu wenu. Kabla hamjajidhalilisha na kumuweka Bw. Lowasa kuwa mgombea wenu. Sasa hivi tume ya uchaguzi ibadilishwe kama mnavyotaka au katiba ije kwa muundo wa ile ya Warioba, hakuna mtakacho faidi. Maana hamuungwi mkono kama zamani. Hamna sera za kutufanya tuwakubali. Na hasa wakati huu ambapo mnaona muokozi wa jahazi lenu ni Bw. Membe au Bw. Lissu.
 
Bado ubongo wangu unatafakari mengi sana juu ya upinzani wa Tanzania ambao umefikia mahali kuonekana ni chombo cha kuhamasisha ajenda za siri ambazo watanzania hawakubaliani nazo. Sura ya kwanza ya upinzani watanzania tuliujua kama wa maandamano na migomo lakini miaka hii michache ya Rais Magufuli umetusaidia kuujua upinzani katika sura ya pili ambayo hatukubahatika kuijua hapo kabla. Sura ya pili ya upinzani ambayo INABEZA, INALAUMU, INAPINGA kila jitihada chanya za serikali ya nchi hii.

Nikiendelea kutafakari Zaidi najikuta katika wimbi zito la kufikiri, kuwaza na kuwazua ni nini wapinzani wanataka serikali ifanye kwa ajili ya watanzani ? watanzania tulio wengi tunaona matokeo ya maamuzi tuliyofanya mwaka 2015 ya kumchagua Rais Magufuli kuwa Rais wetu , ni maamuzi yenye tija, ya hekima na busara nyingi. Rais ambaye anatekeleza aliyoahidi na anafanya yale wapinzani waliyokuwa wanayasema ni fahari kubwa watanzania.

Katika hili la kupinga na kubeza kila kitu, upinzani umekuwa tatizo kwa watanzania kusonga mbele. Ni hakika kabisa mpinzani wa kweli kutoka CHADEMA alikuwa ni Dkt.Slaa tu kwa sababu ameamua kuachana na utoto wa kisiasa wa CHADEMA wa kupinga yale aliyokuwa anayaamini na kuamua kuwa upande ule ambao unayafanya kwa vitendo nao ni CCM.

Aibu gani hii? Fedheha ya namna gani hii kwa watanzania? Hakika watanzania kuendelea kukumbatia upinzani huu usio na malengo ni kujirudisha nyuma enzi za ujima na ukabaila , enzi ambazo maendeleo yalikuwa hafifu. Watanzania wa sasa wanataka maendeleo ya kasi ya viwanda, kilimo, elimu, miundombinu , afya na uvuvi na kiongozi tuliyenaye sasa anajua mahitaji ya watanzania na anajitahidi kufanikisha kuyatimiza hata kama si kwa asilimia 100 ila kwa kiwango alichofikia tunaweza kusema maendeleo ya Tanzania yapo juu.

Kwa nini watanzania waendelee kushiriki utoto wa kisiasa wakati dira na muelekeo wa maendeleo chini ya Rais Magufuli ni mzuri na wenye nuru kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Utoto wa kisiasa wa upinzani uliwatumbukiza watanzania kwenye siasa za matukio na purukushani badala ya siasa za utendaji ambazo kwa hakika awamu hii ya tano umezianika wazi.
Rubbish
 
Hiyo ilikuwa ni wakati ule siyo sasa! Ni wakati ule Dr. Silaa bado ni katibu wenu. Kabla hamjajidhalilisha na kumuweka Bw. Lowasa kuwa mgombea wenu. Sasa hivi tume ya uchaguzi ibadilishwe kama mnavyotaka au katiba ije kwa muundo wa ile ya Warioba, hakuna mtakacho faidi. Maana hamuungwi mkono kama zamani. Hamna sera za kutufanya tuwakubali. Na hasa wakati huu ambapo mnaona muokozi wa jahazi lenu ni Bw. Membe au Bw. Lissu.
Hata kujenga hoja hujui bado,huu utumbo wako hata wanaccm wenzio watakushangaa jinsi ulivyokuwa mweupe kichwani.
 
Back
Top Bottom