Upinzani unadumazwa na CHADEMA

Upinzani unadumazwa na CHADEMA

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,733
Reaction score
4,928
Wananchi wanapenda mabadiliko sana ila vyama vinavyojiita vya upinzani Nchini hususani Chadema kimekuwa kikizorotesha sana uhai upinzani.

Ushahidi wa haya unayoyasema upo wazi kabisa:-
1. CHADEMA ndiyo waliomkera Dr Wilbroad Slaa kiongozi ambaye alipaswa kuzalisha vijana wengi kwa kuwafundisha historia ya siasa za kipinzani za kistaarabu.

2. Chama hiki licha ya kuwa chama kikuu cha kipinzani Nchini hakina succession planning inayoeleweka kwa mfano mwaka 2015 kiliamua kuona wagombea wake wa ndani hawafai na kuazima mgombea kutoka CCM.

Hii inaonesha kuna watu wanaaminiwa na Wananchi wawawakilishe ila wanachokifanya hao wawakilishi siyo uwakilishi unaotakiwa.
Nadhani leo tarehe 4/12/2018 tumemsikiliza Mheshimiwa Waziri Mkuu Mstaafu amesema nini kuhusu CDM halafu tuunganishe nukta.
 
Succession plan ya CCM ni ipi? Magufuli? CCM ilipanga kweli aawe Rais anayefuata, au Bashiru awe KM? Polepole awe K/Mwenezi? hao wote ni ngekewa by Mdee's voice!You must be carzy!
 
succession plan ya CCM ni ipi? maagufuli? CCM ilipanga kweli aawe rais anayefuata, au Bashiru awe KM? Polepole awe K/Mwenezi? hao wote ni ngekewa by Mdee's voice!You must be carzy!
Unalinganisha strategy au kipi hapo? na ukitaka kujiona vizuri unakumbuka CCM ilikuwa na wagombea wangapi? linganisha na CHADEMA uone maajabu.
 
Acheni unafiki kuweni wakweli, ukweli ni uhuru kwani niliyoyaandika ni uongo? tulia kijana
 
Kama kisingizio chako ni CHADEMA ninamashaka na uelewa wako ndani ya siasa ya Tanzania! Ni juzi tu Tar 24 Nov. ndo uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika na bado lawama unapeleka kwa CHADEMA!!

Kwa nini usiwalaumu Serikal na Tume ya Uchaguzi labda na vyombo vya usalama?
 
Kama kisingizio chako ni CHADEMA ninamashaka na uelewa wako ndani ya siasa ya TZ! Ni juzi tu Tar 24 Nov. ndo uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika na bado lawama unapeleka kwa CHADEMA!!

Kwa nini usiwalaumu Serikal na Tume ya Uchaguzi labda na vyombo vya usalama?
Nikuulize hivi upinzani imeanza kwenye uchaguzi wa juzi au? Twende taratibu misingi ya upinzani CHADEMA ni more than weak
 
Nikuulize hivi upinzani imeanza kwenye uchaguzi wa juzi au? Twende taratibu misingi ya upinzani CDM ni more than weak
Haujaanza juzi! then hujui vyama kama CHADEMA kila uchaguzi ilikuwa ikizidi kuongeza nafasi? Je, waliowakata wagombea wa Upinzani hata waliorudisha fomu ni Viongozi wa CHADEMA?.
Na kungekuwa na tume huru ya uchaguzi kuna vyama vingine vingebaki na jembe tu kwa bendera zao! Nyundo haitumiki sana shambani/vijijini
 
Haujaanza juzi! then hujui vyama kama CHADEMA kila uchaguzi ilikuwa ikizidi kuongeza nafasi? Je, waliowakata wagombea wa Upinzani hata waliorudisha fomu ni Viongozi wa CHADEMA?.
Na kungekuwa na tume huru ya uchaguzi kuna vyama vingine vingebaki na jembe tu kwa bendera zao! Nyundo haitumiki sana shambani/vijijini
Mbona hatutaki self criticism unataka kusema hakuna sababu zozote za ndani ya Cdm zinazozorotesha upinzan au?.
 
Kama kisingizio chako ni CHADEMA ninamashaka na uelewa wako ndani ya siasa ya TZ! Ni juzi tu Tar 24 Nov. ndo uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika na bado lawama unapeleka kwa CHADEMA!!

Kwa nini usiwalaumu Serikal na Tume ya Uchaguzi labda na vyombo vya usalama?
Hayo ni mainga ya lumumba yako kwenye propaganda mfu.
 
Km huna cha kuandika kaa kimya. Kwa mwenye akili timamu anajua upinzani unadumazwa na nani. Inamaana Chadema ndo wameisambaratisha CUF? Mijitu mingine buana!
Yani wewe hujui kuwa CUF chanzo cha kusambaratika ni Chadema?

2015 CUF na chadema viliungana na kutengeneza umoja wa ukawa Lipumba alikuwa hana shida kumuachia Slaa kiti cha kugombea uraisi

Gafla Mbowe akamkaribisha Lowasa katika kikao cha kumpitisha Lowasa kama mgombea uraisi Lipumba alikataa kuhudhuria

Mbowe akaongea na Sefu na Sefu akahudhuria wakampitisha Lowasa kama mgombea wa ukawa
Kwa kuwa makubaliano ya ukawa Mbowe ameyakiuka na pia Mbowe akamshawishi Sefu amsaliti Lipumba kwa kuhudhuria kikao ambacho yeye Lipumba kama mwenyekiti alikikana na wakapitisha maamuzi yao ndipo Lipumba akaona ni bora ajiengue akae pembeni awache na tamaa zao za kisiasa

Hapo mgogoro wa ndani ya CUF ndio ulipo anzia yaliotokea baada ya hapo ni matokeo tu
 
Wananchi waliopevuka kama wewe wanaoweza kuliona hilo wanalo jukumu la kuwaelimisha wananchi. Lakini pia sheria/katiba inaruhusu kuanzishwa vyama vingine.
 
Unatudhalilisha wala Kitimoto aisee. Hatunaga hoja za namna hiyo.
 
Back
Top Bottom