Daisy Llilies
JF-Expert Member
- Apr 19, 2019
- 1,017
- 2,154
CCM si chama chenye uadilifu katika matumizi ya pesa.
Nani anafahamu budget iliyotumika katika vita ya Kagera,
Tuliwahi kuhoji katika ukombozi wa bara la Afrika? Yote yalikuwa ni maamuzi ya mtu mmoja. Hata Chama kushika hatamu haikuwa ridhaa ya wananchi.
Afadhali ya Nyerere yalikuwa ni maamuzi ya kwa manufaa ya wengi. Ethics hapa inamuona hana hatia.
Awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa Waarabu walipewa mbuga ya Loliondo bila kupitishwa na bunge. Mrema alikamata dhahabu Airport ikiwa inakwenda Arabuni, alipohoji vizuri ndipo alipoambiwa cheo chake ni Waziri wa Ulinzi na hakuna cheo cha Makamu wa Waziri Mkuu kama alivyoaminishwa mwanzo.
Ya Mkapa yanajulikana kubinaifsisha miradi yote ya nchi na kuuziana na wazee wenzake.
Ya Kikwete ni mengi, kwa uchache ni GSM ndiyo washirika wake wakuu. Mzee anapesa chafu lakini uchumi aliyosomea pamoja na unafiki wa Waswahili wa Pwani vinamsaidia mumuone ni mtu wa kawaida. Yeye ndiye mfadhili wa Yanga kama hamfahamu hili.
Magufuli amewazidi wenzake wote. Wengi waliiba awamu ya pili ili wapate pesa ya cha juu ya pensheni lakini Rais Magufuli ameanza kuchota tangu mwaka wa kwanza wa kuwa madarakani.
Hawa na wanufaikaji wengine hawawezi kukubali CCM itoke madarakani. Watu kama Mzee Makamba, Lowasa, Rostam Aziz na wengineo.
Kibaya zaidi wakiwa madarakani hawazalishi ajira. Vijana wasio na ajira, wa wasomi na bodaboda ndiyo kete itakayotumiwa na wapinzani kuanzisha mabadiliko. CCM kubalini kukaa mezani na upinzani mfikie muafaka. Mabadiliko hayaepukiki.
Nani anafahamu budget iliyotumika katika vita ya Kagera,
Tuliwahi kuhoji katika ukombozi wa bara la Afrika? Yote yalikuwa ni maamuzi ya mtu mmoja. Hata Chama kushika hatamu haikuwa ridhaa ya wananchi.
Afadhali ya Nyerere yalikuwa ni maamuzi ya kwa manufaa ya wengi. Ethics hapa inamuona hana hatia.
Awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa Waarabu walipewa mbuga ya Loliondo bila kupitishwa na bunge. Mrema alikamata dhahabu Airport ikiwa inakwenda Arabuni, alipohoji vizuri ndipo alipoambiwa cheo chake ni Waziri wa Ulinzi na hakuna cheo cha Makamu wa Waziri Mkuu kama alivyoaminishwa mwanzo.
Ya Mkapa yanajulikana kubinaifsisha miradi yote ya nchi na kuuziana na wazee wenzake.
Ya Kikwete ni mengi, kwa uchache ni GSM ndiyo washirika wake wakuu. Mzee anapesa chafu lakini uchumi aliyosomea pamoja na unafiki wa Waswahili wa Pwani vinamsaidia mumuone ni mtu wa kawaida. Yeye ndiye mfadhili wa Yanga kama hamfahamu hili.
Magufuli amewazidi wenzake wote. Wengi waliiba awamu ya pili ili wapate pesa ya cha juu ya pensheni lakini Rais Magufuli ameanza kuchota tangu mwaka wa kwanza wa kuwa madarakani.
Hawa na wanufaikaji wengine hawawezi kukubali CCM itoke madarakani. Watu kama Mzee Makamba, Lowasa, Rostam Aziz na wengineo.
Kibaya zaidi wakiwa madarakani hawazalishi ajira. Vijana wasio na ajira, wa wasomi na bodaboda ndiyo kete itakayotumiwa na wapinzani kuanzisha mabadiliko. CCM kubalini kukaa mezani na upinzani mfikie muafaka. Mabadiliko hayaepukiki.