Upinzani tafuteni majadiliano na CCM, wanaogopa madudu waliyoyafanya upinzani ukiwa madarakani yataanikwa wazi

Daisy Llilies

JF-Expert Member
Apr 19, 2019
1,017
2,154
CCM si chama chenye uadilifu katika matumizi ya pesa.
Nani anafahamu budget iliyotumika katika vita ya Kagera,
Tuliwahi kuhoji katika ukombozi wa bara la Afrika? Yote yalikuwa ni maamuzi ya mtu mmoja. Hata Chama kushika hatamu haikuwa ridhaa ya wananchi.

Afadhali ya Nyerere yalikuwa ni maamuzi ya kwa manufaa ya wengi. Ethics hapa inamuona hana hatia.

Awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa Waarabu walipewa mbuga ya Loliondo bila kupitishwa na bunge. Mrema alikamata dhahabu Airport ikiwa inakwenda Arabuni, alipohoji vizuri ndipo alipoambiwa cheo chake ni Waziri wa Ulinzi na hakuna cheo cha Makamu wa Waziri Mkuu kama alivyoaminishwa mwanzo.

Ya Mkapa yanajulikana kubinaifsisha miradi yote ya nchi na kuuziana na wazee wenzake.

Ya Kikwete ni mengi, kwa uchache ni GSM ndiyo washirika wake wakuu. Mzee anapesa chafu lakini uchumi aliyosomea pamoja na unafiki wa Waswahili wa Pwani vinamsaidia mumuone ni mtu wa kawaida. Yeye ndiye mfadhili wa Yanga kama hamfahamu hili.

Magufuli amewazidi wenzake wote. Wengi waliiba awamu ya pili ili wapate pesa ya cha juu ya pensheni lakini Rais Magufuli ameanza kuchota tangu mwaka wa kwanza wa kuwa madarakani.

Hawa na wanufaikaji wengine hawawezi kukubali CCM itoke madarakani. Watu kama Mzee Makamba, Lowasa, Rostam Aziz na wengineo.

Kibaya zaidi wakiwa madarakani hawazalishi ajira. Vijana wasio na ajira, wa wasomi na bodaboda ndiyo kete itakayotumiwa na wapinzani kuanzisha mabadiliko. CCM kubalini kukaa mezani na upinzani mfikie muafaka. Mabadiliko hayaepukiki.
 
Wanaompimga Rais Magufuli Ni mafisadi na wauza madawa ya kulevya na wenye vyeti feki

Sisi Watanzania tunampenda Magufuli nyie wachache mnajiangaisha
Umekariri hilo jibu lakini wengi wanaompinga ni wasomi wasio na ajira, bodaboda anaeambiwa Trillioni 1.5 imepotea hazina bila ya maelezo atampenda Magufuli kweli?
 
Umekariri hilo jibu lakini wengi wanaompinga ni wasomi wasio na ajira, bodaboda anaeambiwa Trillioni 1.5 imepotea hazina bila ya maelezo atampenda Magufuli kweli?
Sasa bodaboda anaijua hio Trilioni 1.5? Tena unamwambia ya serkali. Hivi unawajua Watanzania wewe? Au unawasikiaga tu? Kwa taarfa yako mwananchi wakawaida hajui hizo mambo wala hana mda nazo.

Wanaoteseka ni ma much know tu, na wanaotaka kula bila kuvuja jasho.
 
CCM si chama chenye uadilifu katika matumizi ya pesa.
Nani anafahamu budget iliyotumika katika vita ya Kagera,
Tuliwahi kuhoji katika ukombozi wa bara la Afrika? Yote yalikuwa ni maamuzi ya mtu mmoja. Hata Chama kushika hatamu haikuwa ridhaa ya wananchi.

Afadhali ya Nyerere yalikuwa ni maamuzi ya kwa manufaa ya wengi. Ethics hapa inamuona hana hatia.

Awamu ya pili chini ya Mzee Ruksa Waarabu walipewa mbuga ya Loliondo bila kupitishwa na bunge. Mrema alikamata dhahabu Airport ikiwa inakwenda Arabuni, alipohoji vizuri ndipo alipoambiwa cheo chake ni Waziri wa Ulinzi na hakuna cheo cha Makamu wa Waziri Mkuu kama alivyoaminishwa mwanzo.

Ya Mkapa yanajulikana kubinaifsisha miradi yote ya nchi na kuuziana na wazee wenzake.

Ya Kikwete ni mengi, kwa uchache ni GSM ndiyo washirika wake wakuu. Mzee anapesa chafu lakini uchumi aliyosomea pamoja na unafiki wa Waswahili wa Pwani vinamsaidia mumuone ni mtu wa kawaida. Yeye ndiye mfadhili wa Yanga kama hamfahamu hili.

Magufuli amewazidi wenzake wote. Wengi waliiba awamu ya pili ili wapate pesa ya cha juu ya pensheni lakini Rais Magufuli ameanza kuchota tangu mwaka wa kwanza wa kuwa madarakani.

Hawa na wanufaikaji wengine hawawezi kukubali CCM itoke madarakani. Watu kama Mzee Makamba, Lowasa, Rostam Aziz na wengineo.

Kibaya zaidi wakiwa madarakani hawazalishi ajira. Vijana wasio na ajira, wa wasomi na bodaboda ndiyo kete itakayotumiwa na wapinzani kuanzisha mabadiliko. CCM kubalini kukaa mezani na upinzani mfikie muafaka. Mabadiliko hayaepukiki.
Mkuu nisamehe sijasoma uzi wako maana heading tu imeniput off,so naomba nikuulize swali,hivi ccm wanagopa kutoka madarakani kutokana na maovu waliyoyafanya dhidi ya chadema au dhidi ya watanzania,na Kama ni dhidi ya watanzania why Chadema ndo iwe na jukumu la kuongea na ccm badala ya watanzania wanaotendewa uovu? Elimu wanayopewa watanzania inanipaga wasiwasi sana but nisamehe bure
 
Mkuu nisamehe sijasoma uzi wako maana heading tu imeniput off,so naomba nikuulize swali,hivi ccm wanagopa kutoka madarakani kutokana na maovu waliyoyafanya dhidi ya chadema au dhidi ya watanzania,na Kama ni dhidi ya watanzania why Chadema ndo iwe na jukumu la kuongea na ccm badala ya watanzania wanaotendewa uovu? Elimu wanayopewa watanzania inanipaga wasiwasi sana but nisamehe bure
Nionavyo mleta mada ametaja Upinzani hakuitaja Chadema, ungesoma ungemuelewa
 
Hata yule mkuu wa mkoa mwenye vyeti feki anampinga Rais Magufuli?
Angekuwa hampingi angekuwa amejiuzuru siku nyingi maana chuki ngingi imechangiwa na huyu lakini hawezi kufanywa lolote kwa sababu anajua mengi mabaya ya wakubwa zake. Kwa hali ilivyo wataendelea kuvumiliana mpaka kupingwa na chuki kwa wote kutawarudisha kijijini ambako wataanza kuulizana zile 10% vipi? Chukua chako mapema!
Hata yule mkuu wa mkoa mwenye vyeti feki anampinga Rais Magufuli?
 
Umekariri hilo jibu lakini wengi wanaompinga ni wasomi wasio na ajira, bodaboda anaeambiwa Trillioni 1.5 imepotea hazina bila ya maelezo atampenda Magufuli kweli?
Wanaomchukia magufuli pia ni wale waliozowea short cut to successful.

Waliozowa kuishi DARESALAAM kiujanja ujanja,.
Wajasilasiasa na wengineo kama wewe.
 
Msome tena utaona ile kitu mbaya alifanya na kukata mzizi wa fitina.

Between 1992 and 1996, Rawlings eased control over the judiciary and civil society, allowing a more independent Supreme Court and the publication of independent newspapers. Opposition parties operated outside of parliament and held rallies and press conferences.
 
Between 1992 and 1996, Rawlings eased control over the judiciary and civil society, allowing a more independent Supreme Court and the publication of independent newspapers. Opposition parties operated outside of parliament and held rallies and press conferences.
Ni kweli alifanya yote hayo lakini alichimbua makaburi na wakuwashughulikia (kinyama) watangulizi wake. Kulindana kukaisha. Si advocate mtu afanye kwa style hiyo lakini kuna muda nawaza tu je kulindana kutaisha lini?
 
Back
Top Bottom