Upi ni ukweli juu ya penzi hili?

Upi ni ukweli juu ya penzi hili?

g stable

Member
Joined
May 8, 2013
Posts
34
Reaction score
14
Mwanamke kaenda chuo akakata mawasiliano na mshkaji wakati walikuwa ni wapenzi, akaja akarudi baadaye huku akiomba msamaha kwa tukio la kunyamaza jamaa akamsamehe dada akadai anashida amebiwa nauli jamaa akamtumia laki kutoka Mwanza kuja Dar.

Baadaye jamaa anampenda demu kuliko chochote bi dada akaja akadai simu yake imechkuliwa na kaka yake kibabe hivyo mawasiliano yatafeli jamaaa akawa aware kuwa bi dada hana simu hivyo wakawa wanawasiliana kwa no nyingine ambayo bi dada alimpa akidai ni simu ya jirani yake.

Baadaye jamaa akapata safari ya kikazi akamwambia nakuja Dar kesho napenda nikuone nitakuwa kwa siku 4 demu akadai poa atamuona ajabu mpaka mshikaji karudi Chuga hawajaonana na yule dada, toka siku hiyo yule dada ajafanya jitihada za kumcheki mshkaj wakati ana no zake zote 3 na e mail.

Ajabu simu ya huyo dada huwa inaita ukipiga ila haipokelewi sasa jamaa anahoji simu haiishi chaji? Kama brother ake anayo huwa anaichagi ikiisha?

Ni miezi 3 sasa hawana mawasiliano demu ni wa chuo 21 aged je ni kweli hana no ya mshikaji wake awe anawasiliana?

Au ndo mapenzi yashakufa na hiyo ya kaka kuchukua simu ni hoja tu?

Wakuu embu ioneni hii ishu kimawazo.

Jamaa stil anataka ampige chini kwani ashakaa naye miaka 3 lakini anadai anampenda.

Je aendelee au apige chini?
 
Sasa ataendelea vip wakati penzi lilishaota mbawa? Kama jamaa kusoma hawezi ina maana hata picha haoni kuwa teyari ashakuwa shamba la bibi?
Hapo bibie atamvuna tu kwa sana.
 
Ndio yameisha ivyo wewe kaka tu ndio hujielewi
 
mwanamke kaenda chuo akakata mawasiliano na mshkaji wakati walikuwa ni wapenzi, akaja akarudi baadaye huku akiomba msamaha kwa tukio la kunyamaza jamaa akamsamehe dada akadai anashida amebiwa nauli jamaa akamtumia laki kutoka mwanza kuja dar baadaye jamaa anampenda demu kuliko chochote bi dada akaja akadai simu yake imechkuliwa na kaka yake kibabe hivyo mawasiliano yatafeli jamaaa akawa aware kuw bi dada hanasimu hivyo wakawa wanawasiliana kwa no nyingine ambayo bi dada alimpa akidai ni simu ya jiran yake baadaye jamaa akapata safar ya kikaz akamwambia nakuja dar kesho napenda nikuone nitakuwa kwa siku 4 demu akadai poa atamuona ajabu mpaka mshkaj karudi chuga hawajaonana na yule dada, toka siku hiyo yule dada ajafanya jitihada za kumcheki mshkaj wakat ana no zake zote 3 na e mail, ajabu simu ya huyo dada huwa inaita ukipiga ila haipokelewi sasa jamaa anahoji simu haiishi chaji? Kama brother ake anayo huwa anaichagi ikiisha? Ni miezi 3 sasa hawana mawasiliano demu ni wa chuo 21 aged je ni kweli hana no ya mshkaj wake awe anawasiliana? Au ndo mapenzi yashakufa na hiyo ya kaka kuchkua simu ni hoja tu? Wakuu embu ioneni hii ishu kimawazo. Jamaa stil anataka ampige chini kwani ashakaa naye miaka 3 lakini anadai anampenda je aendelee au apige chini.

Jamaa ana ona manyoya halafu anauliza kuku yuko wapi?
 
^^
Kuna watu watu wana mioyo ya kupenda hadi raha!!
Mawingu huoni,,hadi mvua inakunyeshea unasema sio yenyewe?
Mwambie aamke huo uzezeta sasa.
^^
 
ok!
we ulimshaurije?.. maana naona mimosh tu hapa!
mazima
 
As far as I can see...hakuna mapenzi hapo...
Ni watu wazima wawili ambao wameamua watumiane in the of love...
 
Back
Top Bottom