Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Katika kuungana na dunia kusherehekea Siku ya Mama Duniani Jumapili hii Mei 11, 2025, klabu ya AC Milan imeendeleza utaratibu wa wachezaji wake kuvaa jezi zenye majina ya Mama zao mgongoni badala ya majina yao kama ilivyozoeleka.
Wachezaji wa AC Milan kwa mara nyingine walivaa jezi hizo dhidi ya Bologna jana wakishinda mabao 3-1 kama ilivyokuwa msimu uliopita kwenye mchezo dhidi ya Cagliari walioshinda kwa mabao 5-1.
AC Milan wamelazimika kuvaa jezi hizo jana Mei 09, kwa sababu hawatakuwa na mchezo wa ligi Mei 11, ambapo ndio maadhimisho ya siku hiyo Ulaya na kwingineko duniani.
Wameweka utaratibu mzuri wa kuadhimisha siku ya kina Mama duniani. Klabu zingine zifuate utaratibu kama huu.
Wachezaji wa AC Milan kwa mara nyingine walivaa jezi hizo dhidi ya Bologna jana wakishinda mabao 3-1 kama ilivyokuwa msimu uliopita kwenye mchezo dhidi ya Cagliari walioshinda kwa mabao 5-1.
AC Milan wamelazimika kuvaa jezi hizo jana Mei 09, kwa sababu hawatakuwa na mchezo wa ligi Mei 11, ambapo ndio maadhimisho ya siku hiyo Ulaya na kwingineko duniani.
Wameweka utaratibu mzuri wa kuadhimisha siku ya kina Mama duniani. Klabu zingine zifuate utaratibu kama huu.