laii
JF-Expert Member
- Oct 10, 2016
- 834
- 1,060
Kwenye hii Dunia ya sasa, ni watu wachache sana watakupenda jinsi ulivyo, ni watu wachache watajua mapungufu (ujinga) wako na kuendelea kukupenda jinsi ulivyo, ukipata mtu au watu wa aina hii washikilie sana, waombee sana.
Ni watu wachache wataichukulia shida yako kama yao, kuna watu wapo radhi kukopa ili kukusaidia katika matatizo yako, wako radhi kuhairisha walichopanga kufanya ili kutatua changamoto zako, hakika ukimpata mtu wa aina hii mshikilie sana na muombee sana Kwa Mungu.
Ukiwa nao usiongee kupitiliza utajikuta umeongea hadi mambo yatakayomkera, chagua maneno ya kuongea na wakati sahihi ya kuyaongea, usilielie shida wala kuomba omba hela iwe kukupa bure au kumkopakopa, usijieleze sana kwake kuhusu changamoto zako na familia kwa ujumla, mkishaongea mara moja mwache, mara nyingi watu wa aina hii husukumwa na Upendo walio nao kusaidia na si mara ngapi umemwambia shida zako. Jitahidi kuficha madhaifu yako mbele yake, acha ayaone au ayasikie.
Dunia ya leo imejaa watu wanaojipenda wenyewe Wenye kujali vitu kuliko utu, akishiba yeye inatosha haangalii wengine, ni watu ambao wako radhi kuuzima uhai wa kiumbe chochote Kwa ajili ya mali. Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hiyo hapo juu mshikilie sana, na wewe pia ujitoe Kwa watu ambao unaweza kuwasaidia na kurejesha tabasamu lao.
Mungu Awabariki Na Kuwalinda, Kwa Jina La Baba na La Mwana na La Roho Mtakatifu. Amina.
Ni watu wachache wataichukulia shida yako kama yao, kuna watu wapo radhi kukopa ili kukusaidia katika matatizo yako, wako radhi kuhairisha walichopanga kufanya ili kutatua changamoto zako, hakika ukimpata mtu wa aina hii mshikilie sana na muombee sana Kwa Mungu.
Ukiwa nao usiongee kupitiliza utajikuta umeongea hadi mambo yatakayomkera, chagua maneno ya kuongea na wakati sahihi ya kuyaongea, usilielie shida wala kuomba omba hela iwe kukupa bure au kumkopakopa, usijieleze sana kwake kuhusu changamoto zako na familia kwa ujumla, mkishaongea mara moja mwache, mara nyingi watu wa aina hii husukumwa na Upendo walio nao kusaidia na si mara ngapi umemwambia shida zako. Jitahidi kuficha madhaifu yako mbele yake, acha ayaone au ayasikie.
Dunia ya leo imejaa watu wanaojipenda wenyewe Wenye kujali vitu kuliko utu, akishiba yeye inatosha haangalii wengine, ni watu ambao wako radhi kuuzima uhai wa kiumbe chochote Kwa ajili ya mali. Kwa hiyo ukipata mtu wa aina hiyo hapo juu mshikilie sana, na wewe pia ujitoe Kwa watu ambao unaweza kuwasaidia na kurejesha tabasamu lao.
Mungu Awabariki Na Kuwalinda, Kwa Jina La Baba na La Mwana na La Roho Mtakatifu. Amina.