Upendo ni nini?

Alfred88

Senior Member
Jul 25, 2016
125
59
Tunapozungumzia upendo, ni hisia zinazotoka moyoni mwa mtu. Mtu anaposema "Nakupenda kutoka moyoni" hana maana kuwa moyo ndio unaokupenda bali hisia zake za moyoni zipo kwajili yako. Unajikuta umempenda mtu pasipo kujitambua wewe mwenyewe, lakini pia kuna upendo wa dhati(kweli) na upendo wa ulaghai(uongo/kinafki).

Sio wote watakao sema neno nakupenda basi ni wakweli bali yakupasa kuchunguza hisia za huyo mtu kwanza kabla huja amini. Usipende kufosi mapemzi sababu utaumia maisha yako yote kwa kile utakachofanyiwa. Ule msemo wa ""penda unapopendwa"" sikweli. Uliza kwanza moyo wako nini unataka na si kukurupuka.
 
Tatizo ni wewe unapopenda hupendwi na yeye anapenda mwingine na mwingine anapenda mwingine huko. basi vuruguvurugu mtindo mmoja.
 
practically upendo ni mgumu, unatakiwa kuwapenda watu wote,hata wanaokufanyia mabaya ambako ndiko kuna changamoto
 
Back
Top Bottom