Upelelezi wazidi kukwamisha kesi ya Kitilya na wenzake

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Upelelezi wazidi kukwamisha kesi ya Kitilya na wenzake

Upelelezi wa kesi inayomkabili Kamishna Mkuu Mstaafu wa TRA, Harry Kitilya, mshindi wa Mashindano ya Urembo (Miss Tanzania), mwaka 1996, Shose Sinare na Sioi Solomon katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamili.
Dar es Salaam.Upelelezi wa kesi inayomkabili Kamishna Mkuu Mstaafu wa TRA, Harry Kitilya, mshindi wa Mashindano ya Urembo (Miss Tanzania), mwaka 1996, Shose Sinare na Sioi Solomon katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Hellen Moshi aliyaeleza hayo leo kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Hata hivyo Hakimu Nongwa aliutaka upande wa mashtaka Juni 2, 2017 kueleza upelelezi umefikia katika hatua ipi.

Katika kesi hiyo washtakiwa hao wanadaiwa kutenda makosa kati ya Machi 2013 na Septemba 2015 wakati wa mchakato wa mkopo wa dola za Marekani 550 milioni kwa Serikali ya Tanzania kutoka Benki ya Standard Uingereza.

Wanadaiwa kula njama na kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, Kwa upande wa mshtakiwa.




Chanzo: Mwananchi
 
Hahahaah!Sioi eti ana vaa tai halafu anakwenda kunyea ndoo,ndio nini sasa,anatuonyesha yupo vizuri tu au
 
Hahahaah!Sioi eti ana vaa tai halafu anakwenda kunyea ndoo,ndio nini sasa,anatuonyesha yupo vizuri tu au
Mkuu kesi haijaisha upelelezi ndio utabaini nani hasa kaiba na nani ni guilty na hukumu watapewa hivyo sio vzuri katika hatia ya sasa kuanza kejeli mtu au kumtusi mtu ilihali bado hujajua nani aliyepiga hizo hela hta wa upande wa serikalini coz its obvious hao watatu siamini walipiga dili kubwa hivyo bila "watu flani kujua" ni mahakama tu itaeleza hilo sasa haya ya kukejeli yanatoka wapi..... we unafurahia binadama mwenzio kunyea ndoo ???
 
Mim nilijua imeshaafutwa hiyo kesi kumbe bado tu ipo
Shitaka lisilo na dhamana la UHUJUMU UCHUMI liliondolewa hivyo dhamana ikawa wazi na hapo serikali/upande wa mashtaka ikaweka pingamizi hivyo shtaka likarudishwa tena!!! Ndio maana bado wako ndani
 
Mkuu kesi haijaisha upelelezi ndio utabaini nani hasa kaiba na nani ni guilty na hukumu watapewa hivyo sio vzuri katika hatia ya sasa kuanza kejeli mtu au kumtusi mtu ilihali bado hujajua nani aliyepiga hizo hela hta wa upande wa serikalini coz its obvious hao watatu siamini walipiga dili kubwa hivyo bila "watu flani kujua" ni mahakama tu itaeleza hilo sasa haya ya kukejeli yanatoka wapi..... we unafurahia binadama mwenzio kunyea ndoo ???
Mie nimesema tu kuvaa tai halafu unarudi keko maana yake nini?
Halafu hata wakiongezwa wengine lakini hao watatu ndio wahusika wakuu.Huyo sio alikuwa mwanasheria aliesaini huku akijua si halali,hilo zee ndio hela iliingizwa kwenye kamapuni yake na huyo kidosho anatuhumiwa kuwa mtu wa kati
 
Hako kamis watakuwa vigogo walikagegeda kwanza alafu wakakapa bobge la deal kakaishia kuwa kaizi, dah....
 
Mie nimesema tu kuvaa tai halafu unarudi keko maana yake nini?
Halafu hata wakiongezwa wengine lakini hao watatu ndio wahusika wakuu.Huyo sio alikuwa mwanasheria aliesaini huku akijua si halali,hilo zee ndio hela iliingizwa kwenye kamapuni yake na huyo kidosho anatuhumiwa kuwa mtu wa kati
Sasa ulitaka avaaje kwenda mahakamani?? Yaani unakejeli tena hku unacheka kisa unajua anajisaidia kwenye ndoo !!! Mkuu yasikupate jela sio mahala salana awekwe wa ccm au chadema jela sio nzuri ssa kushabikia huku bado hujajua kma ni mhalifu or not sio maturity kabisa!!!

Anyway nape na masha walikuwa kma wwe ila sahvi wamenyooka
 
Back
Top Bottom