Updates za Corona Tanzania

Watu 200 kwa siku? Hebu muulize mwandishi tena
 
Hapa mjini kahama nako kuna tetesi ya mtu kukutwa na corrona, ila haijathibishwa vipimo vyapelekwa maabara muhimbili.
Kwa hali ya sasa inawezekana wengi tunamaambukizi ila muda tu haujatimia kuanza kuonyesha dalili.

Vipi nasikia msemaji wetu wa simba (Hajji Manara)nae kaupata huko Spain hii ina ukweli wadau?
 
Serikali imefanya uzembe, kuruhusu safari na kutofunga mipaka.
Na yule Mama naona alijijua ana corona akaamua aje kutuletea huku.
Et unajiweka karantini mwenyewe? ?
Alijua.
1. kwanini alisafiri kipindi hiki
2.kwann Serikali ilimpa kibari

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeona juzi Muhimbili watu wanapanga foleni kunawa mikono kwa maji na sabauni. Nikajiuliza kwa foleni zilizopangwa hapo, akitokea mgonjwa mmoja akapiga chafya au kukohoa wataambukizwa wangapi? Kama Muhimbili wenye dhamana ya kulinda afya hawako makini kiasi hicho, vipi wanasiasa na viongozi wengine wa kisiasa?

Tutasikia tu kauli za tumejidhatiti kupambana na CORONA ila ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa hatujalichukulia suala hili kwa uzito unaostahili. Namba 1 jana alisema amegundua amefanya kosa kusimama njiani hali iliyowafanya watu wakakusanyika na kuleta hatari ya maambukizi.

MUHIMU. Nawa mikono kadiri ya utakavyoweza, epuka msongamano na jitahidi usiguse mdomo, pua au macho. Kuvaa musk mbwembwe maana kwa ukata wetu, mtu atavaa musk moja mwezi mzima lakini pia itapelekea upungufu wa musk kwa wataalamu wa afya ambao wanazihitaji zaidi kuliko sisi raia ambao hatuhudumii wagonjwa moja kwa moja.
Kama umeambukizwa corona, vaa musk ili kuepuka kuambukiza wengine. Mpende jirani yako kwa kumlinda asipate corona.
 
Hii nayo ni habari ya kutuletea hapa ?.

Tatizo la Watanganyika hampendi kusoma

Jitahidi upende kusoma mkuu, itakusaidia

kuondokana na mihemko isiyofaaa

.


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…