Hatua ya lala salama ya Ligi Kuu Tanzania bara ilianza tarehe 15 - 01 - 2011 kwenye viwanja mbalimbali nchini kuwania ubingwa wa soka ambao kwa sasa unashikiliwa na Simba.
Timu 12 zinashiriki ligi hiyo kutoka mikoa ya Dar es Salaam yenye timu za Simba, Yanga, Azam, African Lyon, Pwani yenye timu za JKT Ruvu na Ruvu Shooting, Songea yenye timu ya Maji Maji, Mwanza yenye timu ya Toto Africa, Dodoma yenye timu ya Polisi Tanzania, Arusha yenye timu ya AFC, Morogoro yenye timu ya Mtibwa Sugar na Bukoba yenye timu ya Kagera Sugar.
Timu zilifanya usajili katika dirisha dogo, kuimarisha vikosi vyake hivyo huu ndio wakati wa kuangalia uwezo wa wachezaji waliosajiliwa na kuona wanavyo zisaidia timu zao kuchukua ubingwa au kuziokoa kushuka daraja.
Tutakuwa tunajulishana kila mara kinacho endelea kwenye ligi hii mhimu kabisa hapa Bara.