Dogo G
JF-Expert Member
- Jul 6, 2018
- 1,052
- 440
Wandugu habari,
Juzi nilileta taarifa kuhusiana na mwanajeshi wa jwtZ kupewa kichapo kikali na vijana wa bodaboda punde baada ya kumdhulumu yule kijana 1500 tu ambayo ilikuwa ni kwaajili ya malipo ya huyo boda kwa hiyo huduma.
Sasa jana inasemekana kiongozi wa kambi ya mafinga mwenye cheo cha luteni(jina halijafahamika) alikwenda kituo cha polisi mafinga kwaajili ya kuzungumza na mkuu wa polisi mafinga(OCD) ambapo pia alimshukuru kamanda huyo kwa kuwa police waliwahi mapema kumuokoa huyo kijana kwasababu bila hivyo angekuwa ni hayati.
Katika mazungumzo hayo,inasemekana yule luteni amefedheheka sana na kitendo kilichotendwa na askari wake kwa kufanya utovu wa nidhamu kudhulumu shillingi 1500 kwa raia kwani kwa namna moja anachafua sifa ya jeshi la wananchi(JWTZ) lakini amesema askari huyo ambaye ni private atahojiwa zaidi hali yake kimwili ikitengemaa kwani bado yupo nyumbani akiugulia na uchunguzi unafanyika ikibainika kosa ni lake sheria za kiuaskari zitafwatwa.
Source:ebony
MY TAKE:sasa nimeamini hii awamu nyingine na zama zimebadilika,mimi nilifikiri wangekwenda kulipiza kisasi kwa bodaboda wote badala yake kaenda police kisheria Zaidi ndio kwanza anasema anafanya UCHUNGUZI.kweli sasa uonevu umekwisha
Juzi nilileta taarifa kuhusiana na mwanajeshi wa jwtZ kupewa kichapo kikali na vijana wa bodaboda punde baada ya kumdhulumu yule kijana 1500 tu ambayo ilikuwa ni kwaajili ya malipo ya huyo boda kwa hiyo huduma.
Sasa jana inasemekana kiongozi wa kambi ya mafinga mwenye cheo cha luteni(jina halijafahamika) alikwenda kituo cha polisi mafinga kwaajili ya kuzungumza na mkuu wa polisi mafinga(OCD) ambapo pia alimshukuru kamanda huyo kwa kuwa police waliwahi mapema kumuokoa huyo kijana kwasababu bila hivyo angekuwa ni hayati.
Katika mazungumzo hayo,inasemekana yule luteni amefedheheka sana na kitendo kilichotendwa na askari wake kwa kufanya utovu wa nidhamu kudhulumu shillingi 1500 kwa raia kwani kwa namna moja anachafua sifa ya jeshi la wananchi(JWTZ) lakini amesema askari huyo ambaye ni private atahojiwa zaidi hali yake kimwili ikitengemaa kwani bado yupo nyumbani akiugulia na uchunguzi unafanyika ikibainika kosa ni lake sheria za kiuaskari zitafwatwa.
Source:ebony
MY TAKE:sasa nimeamini hii awamu nyingine na zama zimebadilika,mimi nilifikiri wangekwenda kulipiza kisasi kwa bodaboda wote badala yake kaenda police kisheria Zaidi ndio kwanza anasema anafanya UCHUNGUZI.kweli sasa uonevu umekwisha