Kwa mtizamo wangu, kuwa na mtazamo kinyume na unavyofikir sio uvivu wa kufikiru. Watu wanadhani lowasa ndio fisadi na wengine wote wasafi. Lakini tunaona, huyu lowasa ameondolewa miaka nane iliyipita, na bado tumeuona ufisadi wa kutisha. Mfumo wetu wa kiserikali ndio unaotengeneza mazingira rafiki ya ufisadi. Sidhani kama kwenye tz hii kuna mtu ambaye ana mamlaka, kuanzia wenyevit wa vijiji mpaka juu ambaye ambaye alicho nacho alikipata kwa halali, na hiyo ni pamoja na wewe na mimi. Shida uoo katika mfumo wa serikali, kwa sababu mtu hafanyi ufisadi kwa jina lake, bali kwa cheo chake. Kwa hiyo ni rahis rais kwa cheo chake akalazimisga jambo, na kwa sababu hao anaowaagiza ni wateule wake, itabidi wafanye kulinda kibarua chake. Vivyo hivyo wazri mkuu, mawaziri, wakurugenzi, wakuu wa taasisi, wakurugenzi wa hamashauri ambao nao hawapo nyuma kuchakachua, kila mmoja kwa uwigo wa mamlaka yake, wamefanya hayo. Nijuavyo mimi, jambo lolote linaoopekwa bungeni, ni lazima lijadiriwe kwanza na baraza la mawaziri. Na hata bunge letu nalo linekaa kuupalilia ufisadi, kwa sababu miradi yote ya kifisadi ilipitihwa humo ili kutekelezwa, na tunaona hongo wanayopewa naserikali, pale kunapokuwa na uzito(rjea jairo), na kwa sababu mfumo unasababishwa na katiba, na ccm haiwezi kutoa katiba ambayo itawadhibit, na kumbuka kuwa shera na katiba hii ipo kwa ajili ya kutudhibiti sisi, ukionekana unainua shingo na kuulizia wakudhibit, haipo kwa ajili ya kuwadhibiti wao, ili kuwaweka kwenye nidhamu ta utawala, na kwa sababu ccm haiwezi kuleta katiba itakayowaondolea udhbiti wao juu ya watu, tunatakiwa tuitoe kwanza, na ndipo tuanze katiba ya kuwadhibiti, ambayo itawafanya wezi walipie wizi wao. Hakuna mwizi hata mmoja aliyefungwa, akina mramba walifungwa kwa matumizi mabaya ya madaraka, na ambayo nadhani pia, serikali yote, kama baraza la mawaziri walikubaliana.