Upareni hadi Moshi enzi hizo

Upareni hadi Moshi enzi hizo

Kulikuwa na lingine linaitwa Vuma la kwenda Ugweno.
Ha vaathu va vughweno..

Ila ni miaka ya zamani sana nadhani miaka ya 80's huko
 
Je uliwahi kuipanda hiyo basi -''Sirori Teina Horo'' Maana yake Sisimizi hana hasira. Mimi nilisimuliwa tu sikuwahi kuiona ila dada na kaka zangu waliwahi kusafiri nayo.

View attachment 345158

Haaaaaaah, umenikumbusha mbali aisee, magari ya RELWE hayo....yaani likiwa kilomita nne kule vijijini mnasubiri usafiri unasikia mlio wake, nadhani yalikuwa LEYLAND. Sisi tulikuwa tunayaita POSTA...nikiwa kinda nauli ilikuwa senti 45...kulikuwa na second class wanakaa watu sita hivi.
 
Kwanza sisi wa enzi hizo tunajua hakukuwa na mabasi ya East African Railways bus kwa vitongoji i.e. Kutoka Usangi (Vuasu) kwenda Moshi. Haya mabasi yalikuwa long route kama vile Dar Arusha to Nairobi..... Dar Mbeya., Dar Dodoma na Dodoma Arusha/ Moshi na pia Bukoba Mwanza wakati meli haifanyi kazi.
utakuwa umeongea ukweli maana hayo maandishi yenyewe yamewekwa kwenye picha
 
Miaka y 1980+ kulikuwa na basi linaitwa Kimbara-Usangi to Arusha.
 
Hii picha feki, hayo maandishi ya sirori yamewekwa na hayo ya usangi moshi pia, yameandika juu ya picha
Ni kweli hata mimi naona hivyo na lipo la zaidi. Hilo bus lina rangi na alama na namba za kampuni ya reli afrika mashariki (enzi hizo).Kwa tanzania mabus haya yalihudumia barabara za arusha mpaka mbeya kupitia dodoma na iringa.Hakuna bus la railway lililokuwa likihudumia njia ya usangi mpaka moshi.
 
Kwa sasa ukiwa na kichwa cha bata mzinga,utalishwa matangopori sana kwa hizi habari za mitandaoni.
 
SIRORI sio sisimizi wewe mtoa post: SIRORI ni nyuki wadogo wale ambao sio wakali na wanatengeneza asali ambayo wataalamu wanasema ni nzuri na sometimes inatumika kama dawa. (asali ya nyuki wadogo)
SIRORI TEINA HORO means nyuki wadogo hawana hasira

CHIKIRA;
Mi nakutiyo; Nahavache, we uu mwathu kweri. Msijitwalie utukufu kwa lugha za wengine jamani. Ila, thwali langu ni, Mbona ni la shirika letu tukufu East Africa Railway?? Ni mabasi yalikuwa very very famous. Enzi hizo 1968!! Karakana kuu ikiwa Dodoma?
 
CHIKIRA;
Mi nakutiyo; Nahavache, we uu mwathu kweri. Msijitwalie utukufu kwa lugha za wengine jamani. Ila, thwali langu ni, Mbona ni la shirika letu tukufu East Africa Railway?? Ni mabasi yalikuwa very very famous. Enzi hizo 1968!! Karakana kuu ikiwa Dodoma?
washinjiadhe?
 
Leyland Albion. Wakati huo ilikuwa nadra mno bus kupata ajali. Kulikuwa na madereva wawili tena watu wa makamo. Ndani ya Bus kulikuwa na first class kama ndege. Viti vya aina moja lakini mmetenganishwa tu na kiukuta fulani. Wanafunzi walikuwa wanasafiri kwa kutumia warrant. Dotcom hapo ni gizani tu!
 
Back
Top Bottom