Upandaji wa miti aina ya pain

Dec 8, 2013
94
10
Haya jamani 2014 ndo hiyo. Timiza malengo yako ya upandaji miti ili uboreshe mazingira na ukuze uchumi wako na uchumi wa nchi kwa ujumla. Miche ya miti aina ya pain inapatikana kwa Badian kinwiko aliyeko wilayani Mufindi, Iringa, kwa bei ya sh.100@mche. Kwa wakazi wa Mufindi na maeneo jirani mnakaribishwa. Kama una swali tupia hapahapa au email hii badiankinwiko@gmail.com
 
Haya jamani 2014 ndo hiyo. Timiza malengo yako ya upandaji miti ili uboreshe mazingira na ukuze uchumi wako na uchumi wa nchi kwa ujumla. Miche ya miti aina ya pain inapatikana kwa Badian kinwiko aliyeko wilayani Mufindi, Iringa, kwa bei ya sh.100@mche. Kwa wakazi wa Mufindi na maeneo jirani mnakaribishwa. Kama una swali tupia hapahapa au email hii badiankinwiko@gmail.com

Huwa wanatoa maelezo mkuu, hiyo miti ina manufaa gani, ukuaji wake hata na kapicha kidogo mkuu!
 
PAIN ndiyo miti gani?

Bila shaka anamaanisha "pine" ambayo ikitamkwa kwa kiingereza inasikika kwa kiswahili kama "paini"

Kiswahili cha PINE ni "msonobari"

Tuvumiliane tu ndugu yangu. Ndio maana kuna watu wanasema "elementi" wakimaanisha "helmet"; "rejeta" wakimaanisha "radiator"; "dip" wakimaanisha "beep"... na mengine mengi.
 
Pain(pine) ni mti wa mbao, ambao hukua kwa muda wa miaka 8-10 tangu kupandwa shambani, ndipo hupasuliwa na kutoa mbao zenye ukubwa wa inchi 2kwa 8, 2kwa6(2 by 6 inch) na kushuka mpaka 2 kwa 4(2 by 4). Na ni miti inayotoa mbao zenye matumizi mengi na wateja wake ni wengi sana ikishapandwa shambani.
 
Back
Top Bottom