Uovu wa shetani ni upi kwa mujibu wa maandiko?

1. Wakati Mungu anamuumba Lucifer, alijua au hakujua kwamba atakuja kumuasi?

2. Kama binadamu hakutakiwa kujua jema wala baya, angekua na tofauti gani na roboti?

3. Kama binadamu aliumbwa akiwa hajui jema wala baya, angejuaje kwamba kutokumtii Mungu ni vibaya ili asile tunda alilokatazwa?
Mungu anajua yote (Omniscient). Alijua kuna malaika watamwasi, aliwaacha maana hakutaka kuingilia utashi wa viumbe wake kutokana na upendo mkuu alio nao. Pia alijua ni nini atakachokifanya baada ya uasi huo. Ndio maana akaandaa njia ya UKOMBOZI iliyo katika Kristo Yesu Bwana.

Mungu alitaka tusijue jema na baya kwa sababu hakutaka tujiongoze wenyewe (katika nafsi) yaani kujitegemea. Alitaka tuishi kama malaika na viumbe wengine walioko mbinguni. Alitaka tuongozwe na roho, sio akili ambao Iko kwenye nafsi. Akili ya mwanadamu haina uwezo wa kumuongoza mtu kuyafanya mapenzi ya Mungu. Ndio maana mtu anajua kutenda jambo fulani ni makosa mbele za Mungu ila analitenda. Maana yake akili yake kujua jambo hilo ni dhambi haijamsaidia chochote. (ndio maana atahukumiwa)
 
Ukitumia akili utagundua shetani na Mungu ni story tu , jiulize Mungu kaumbaje vitu vyenye mapungufu then mwisho wa siku anakasirika mwenyewe.

Mbona wewe unapanga kuzaa mtoto mwenyewe na bado unakuja kukasirika akifanya tofauti na unavyotaka?
 
Mungu hakuumba shetani. Mungu alimuumba malaika akaasi.

roho ya uasi ilitokea ndani ya moyo wake mwenyewe ! ni kama wewe uamue kumwasi Mungu, utakuwa umeamua wewe! hali ya kuasi hutokea ndani ya moyo wa mhusika.

Mungu hakuumba viumbe wake waendeshwe kama mashine.
Wakati Mungu anamuumba huyo malaika ambaye ni shetani, alikua anafahamu kuwa ipo siku huyo malaika atamuasi na kugeuka kuwa shetani?
 
Mbona wewe unapanga kuzaa mtoto mwenyewe na bado unakuja kukasirika akifanya tofauti na unavyotaka?
Kwasababu sisi sio Mungu!

Hivi wewe ungekua na uwezo wa kuumba kitu kisicho na mapungufu ungechagua kuumba kitu chenye mapungufu huku ukijua kabisa mbeleni kitakuja kukuudhi na kukukasirisha? Halafu eti baadae uje uandae mpango wa kukikomboa halafu utake kitu hicho kikusifu na kukushukuru kwa ukombozi..

Yaani ni sawa na wewe ujenge nyumba halafu uezekee mabati yaliyotobokatoboka, huku ukijua kabisa kwamba mvua ikinyesha utavujiwa. Halafu ukivujiwa uanze kukasirika..
 
Mungu alitaka tusijue jema na baya kwa sababu hakutaka tujiongoze wenyewe (katika nafsi) yaani kujitegemea. Alitaka tuishi kama malaika na viumbe wengine walioko mbinguni.
Kwahiyo unamaanisha malaika na viumbe walioko mbinguni hawajui jema wala baya?

Na pia, kama Mungu hakutaka tujiongoze wenyewe sindio maana yake tungeishi kama maroboti?

Mbona kama maelezo yako yanajichanganya..?
 
Kwahiyo unamaanisha malaika na viumbe walioko mbinguni hawajui jema wala baya?

Na pia, kama Mungu hakutaka tujiongoze wenyewe sindio maana yake tungeishi kama maroboti?

Mbona kama maelezo yako yanajichanganya..?
Malaika hawajui jema wala baya. Wao huwa wana kazi ya kuyatimiza mapenzi ya Mungu.

Mungu alitaka tuwe na ushirika naye katika kila jambo. tusijiongoze wenyewe. tushirikiane naye katika kuishi.
 
Ukifikiria vizuri utaona hata Mungu mwenyewe ana sifa kama za shetani.

"Barua zako zinakuhubiria ushindi, kutangaza vita wakati mtutu wenyewe hushiki" Dizasta Vina -hatia VI
 
Tegua kitendawili
Wayahudi Bible yao wameandika Adamu na Eva waliumbwa kwenye Mwili mmoja yaan upande wa kushoto Eva upande wa kulia Adamu

Wakawa hawawezi kuonana ndio Mungu alipoona Adamu anapata tabu akawapeleka Mloganzila kisha MOI akawafanyia upasuaji wa kwanza duniani ndio wakatoka wawili huku Adamu na huku Eva

Sasa balaa linakuja swali

Km Mungu alitaka Adamu na Eva waishie kwenye bustani ya Hedeni kulikua na umuhimu gani kumruhusu Shetani aingie bustanini na kuwafarakanisha wawili wale waliokua mwili mmoja kula tunda la katikati likawanogea mpaka wakafurushwa bustanini?
 
Back
Top Bottom