Uondoaji chuki sehem 1

Mufiyakicheko

JF-Expert Member
Mar 24, 2011
892
86
Aina zote za chuki lazima zisahauliwe, iwe chuki ya kitaifa au chuki ya kidini kadiri ya watu watakavyo shikilia kwenye chuki hatutakuwa na amani duniani vita vyote tulivyokuwa navyo katika siku za nyuma, umwagaji damu vimekuwa vikitokea sababu ya Chuki ya aina fulani watu wamegombana juu ya nchi yao au dini yao wakileta maangamizi duniani na mauwaji kwa mamilioni ya binadamu wenzao.

Ikiwa chuki hii na uadui ni kwa sababu ya dini (fikiri kwamba) dini lazima iwe chanzo cha upatano, la sivyo haina faida na ikiwa chuki hii ni chuki ya kitaifa (fikili kwamba)binadamu wote ni wa taifa moja wote wamechipuka kutoka kwenye mti wa adam na adam ni mzizi wa mti mmoja na mataifa yote haya ni kama matawi ambapo watu mmoja mmoja ni kama majani mauwa na matunda ya mti huo.

Uanzishaji wa mataifa mbalimbali na baadaye umwagaji wadamu maangamizi ya binadamu vinatokana na ujinga wa binadamu na nia za ubinafsi. Chuki za taifa na taifa ni sababu ya ujinga kabisa uso wa dunia nchi moja ya asili kila mwanadamu anaweza kuishi mahali popote katika dunia mipaka hii na njia za milango ya kuingia na kutoka vimefanywa na binadamu katika kuumbwa mipaka haikuwepo bara ra (Removal of Prejudice)sehemu 2 inaendelea
 
Back
Top Bottom