ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 43,060
- 49,748
Umoja wa Mataifa Ulitoa Waraka wa kukataza Matumizi ya Lugha za Kibaguzi "Hate Speech" Kwa Wanachama wake pindi wanapotaka kufikisha ujumbe wao wa kupinga au kujitafutia maslahi mbalimbali.
Sasa hapa Tanzania Toka Sakata la Makubaliano ya Serikali na DP World kuhusu uendeshaji wa Bandari kumetokea sintofahamu ya makundi mbalimbali ya wanaopinga na kukubali..
Lakini Kwa masikitiko Makubwa Jamaa wa Chadema wamekuwa wakitumia Lugha ya Ubaguzi na Chuki kufikisha maoni Yao hayo hasa Wakimlenga Rais "kwamba anauza Bandari Mali ya Tanganyika Kwa sababu yeye ni Mzanzibari",alianza Mbowe na Sasa imekuwa Kwa Wanachama wao wote si Lisu Wala Lema au mashabiki wao..
Hoja Iko hapa,Chadema wanaojinasibu kuwa na wanasheria wabobezi na watu wanaoheshimu utawala Bora wamekuwa wanafanya kosa Hilo Kwa Makusudi wakati wanafahamu fika ni kinyume na Maadili na tunu za Taifa hili na pia ni kinyume na Jumuiya ya Umoja wa Mataifa,na wanafanya hivi hadharani kwenye majukwaa na Kwa kutumia mitandao ya Kijamii.
Ndugu zangu amani ni kitu Cha msingi na adhimu kujengwa ila ni sekunde tuu kinaweza kupotea.Huko Rwanda,Burundi,DRC,South Sudan,Sierra Leon,Central Africa Republic,Miamar,Germany nk kulianza na Kauli za kueneza Chuki za kimaeneo,rangi,utaifa na baadae dini na ukabila vikaungana na kuzusha Moto mkubwa wa Mauaji..
Kumekuwa na wito wa watu na makundi kadhaa kutaka swala la Bandari lisitumike kueneza Chuki na Ubaguzi ila wao wameendelea na Serikali imekaa kimya.
Swali,Je huwezi fikisha ujumbe wako bila kutumia Chuki ukaeleweka? Na kama Kuna vyombo vya Utoajia Haki na kesi Iko Mahakamani Kwa nini Chadema Kwa kutumia Wanachama wao akiwemo Dr.Slaa Wanaendeleza chuki?
My Take
Naomba sana Mh.Rais asikae kimya maana yeye ndie aliapa kulinda Amani ya Tanzania,kuwaacha watu kama Hawa wanaeneza Chuki Kwa visingizio vya Demokrasia na uhuru wa kutoa maoni haikubaliki.
Uhuru na Demokrasia usiofuata maadili ni hatari kwa Ustawi nastakabali wa Taifa na Jumuiya ya Mataifa Kwa Ujumla..
Vyama vinavyohubiri chuki na Ubaguzi tuvikatae.
Sasa hapa Tanzania Toka Sakata la Makubaliano ya Serikali na DP World kuhusu uendeshaji wa Bandari kumetokea sintofahamu ya makundi mbalimbali ya wanaopinga na kukubali..
Lakini Kwa masikitiko Makubwa Jamaa wa Chadema wamekuwa wakitumia Lugha ya Ubaguzi na Chuki kufikisha maoni Yao hayo hasa Wakimlenga Rais "kwamba anauza Bandari Mali ya Tanganyika Kwa sababu yeye ni Mzanzibari",alianza Mbowe na Sasa imekuwa Kwa Wanachama wao wote si Lisu Wala Lema au mashabiki wao..
Hoja Iko hapa,Chadema wanaojinasibu kuwa na wanasheria wabobezi na watu wanaoheshimu utawala Bora wamekuwa wanafanya kosa Hilo Kwa Makusudi wakati wanafahamu fika ni kinyume na Maadili na tunu za Taifa hili na pia ni kinyume na Jumuiya ya Umoja wa Mataifa,na wanafanya hivi hadharani kwenye majukwaa na Kwa kutumia mitandao ya Kijamii.
Ndugu zangu amani ni kitu Cha msingi na adhimu kujengwa ila ni sekunde tuu kinaweza kupotea.Huko Rwanda,Burundi,DRC,South Sudan,Sierra Leon,Central Africa Republic,Miamar,Germany nk kulianza na Kauli za kueneza Chuki za kimaeneo,rangi,utaifa na baadae dini na ukabila vikaungana na kuzusha Moto mkubwa wa Mauaji..
Kumekuwa na wito wa watu na makundi kadhaa kutaka swala la Bandari lisitumike kueneza Chuki na Ubaguzi ila wao wameendelea na Serikali imekaa kimya.
Swali,Je huwezi fikisha ujumbe wako bila kutumia Chuki ukaeleweka? Na kama Kuna vyombo vya Utoajia Haki na kesi Iko Mahakamani Kwa nini Chadema Kwa kutumia Wanachama wao akiwemo Dr.Slaa Wanaendeleza chuki?
My Take
Naomba sana Mh.Rais asikae kimya maana yeye ndie aliapa kulinda Amani ya Tanzania,kuwaacha watu kama Hawa wanaeneza Chuki Kwa visingizio vya Demokrasia na uhuru wa kutoa maoni haikubaliki.
Uhuru na Demokrasia usiofuata maadili ni hatari kwa Ustawi nastakabali wa Taifa na Jumuiya ya Mataifa Kwa Ujumla..
Vyama vinavyohubiri chuki na Ubaguzi tuvikatae.