Unyama ndani ya Bongo Action Movie

JMipicha

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
704
1,069
Habari wanaJF

Mimi ni actor chipukizi wa bongo action movie na kutokana na sanaa kushuka nimeona tuje kivingine tena kutokana pia na movie kukosa ubunifu na kila siku movie za mapenzi na uchawi nimeona nitengeneze short film ambayo ni hii hapa click link upate kuiona YouTube na pia ningependa kuskia MAONI kutoka kwenu ili tuzidi kukuza Sanaa ya Bongo.



ASANTENI SANA :
 
Acting nzuri japo art ya mapigano ni moderate. Najua vifaa vya production vimewaangusha kutokana na mtaji hapo ukute kamera ilikuwa moja tuu.

Asante brother yeah camera ya simu tumetumia na KUEDIT kwa simu
 
Action, ongezeni mazoezi na technique za mapigano ziwe unique mkuu. Mfano Agent Bavo ukicheki mapigano yake kuna uniqueness fulani na yote ni kwasababu ya utimamu katika mazoezi. Jipikeni haswa na mbuni technique bora za kusapraizi watu.

Meseji kaka. Bongo tunafeli kwenye kutengeneza script zenye kugusa uhalisia wa maisha yetu ya kitanzania. Hizi script za mabifu kuanza sababu za utapeli au kuibiwa au mzazi kuuliwa na majambazi zimepitwa na wakati na ni nyingi. Na script siyo lazima uangaishe kichwa sana. Kuwa mpenzi wa kutazama movie za wenzetu kwa sana kisha beba idea na ufanye editing.

Mengine kama video quality na technical parts zingine kwakuwa ni mwanzo siwezi walaumu sana japo mmejitahidi.

Action movie, jifue uwe fiti na mwepesi na technique za kutosha. Kwa wataalamu wa ngumi tukiangalia action tu tukaona ya kawaida na ubunifu umekuwa mdogo wengi huwa tuna ignore.


Yote niliyoongea ni maneno. Pigeni kazi wazee mwanzo changamoto nyingi. Kikubwa ubunifu kila kukicha ni muhimu na.msitidhike na uwezo mlionao
 
Mmejitahid lakini binafsi naona clip hiyo ime lost touch na uhalisia hatuna connection na hao characters hatujui ni wana background ipi,(i am wrong kama kuna episodes za nyuma ambazo sijaziona labda zilikuwa zinaelezea characters) kama hamna ujue ni tatizo hilo, hata kama nishort movie unaweza uka establish personality ya characters wako hata kwa ufupi, binafsi naona strangers wanapigana tu hata huyo aliekuwa shot sipati ile hisia maana simjui namuona tu, unavyotengeneza jaribu kuunganisha hisia za movie na watazamaji. Hata kama ni action movie sio watu ndio wawe wanapigana tu for silly reasons, hapana establish kisa kizuri

Movie iwe na uhalisia usifanye kitu kwa vile kinaonekana Cool kwenye screen ila hakimake sense, hapana weka action ambayo binadamu angekuwa kwenye hii situation angefanya kama hiko kipande anashoot bila kuangalia sijaona kama kina uhitaji wa kufanya hivyo ili aonekane cool kama kwenye favourite action movie fulan unayoipenda...hapana nahis ungeweza weka hata”anamuangalia anamuuliza kwanini umefanya hivi? Maybe “angejibu jambo na sisi tungeelewa zaid agenda inayoendelea” labda akawa anabeg kuomba msamaha asiuawe kwamba katumwa maybe au nn, tunapata na hata perception ya uyo jamaa mtekaji, kuweka series ya crazy actions ambazo hazileti manaa si ubora wa movie ya action.

Nmeandika mengi kidg nahis Inatosha najua movie yako sio kiwango cha juu sana upo unaaza kama ulivyosema unaomba comments umepata za wadau hapo, muhimu ni ukifanya jambo hata kama ni dogo fanya kiukweli, mapungufu madogo madogo ndio yanashusha thamani kazi hata unaonekana incompetent, usiache hata kakosa kadogo jaribu kukimbizia perfection najua hautofikia kuwa perfect sema utakuwa umefanya kazi nzuri ya kiwango bora.

Kila la kheri
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom