Sipo
JF-Expert Member
- Jul 25, 2008
- 2,139
- 91
Mwili wa kichanga waopolewa ******
Kamanda wa mkoa wa kipolisi Kinondoni, Mark Kalunguyeye, amesema tukio hilo limetokea mishale ya saa 4:00 asubuhi nyumbani kwa Bi. Asha Said, 60, pale Mwananyama Kisiwani.
Akasema waili wa kichanga hicho unadaiwa kuwa ulitupwa katika shimo hilo la choo na mwanamke ambaye hajafahamika.
Kamanda Kalunguyeye amesema mwili huo wa motto uliopolewa toka ****** na askari wa kikosi cha Zimamoto na uokoaji cha Jijini.
Akasema mwili mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Mwananyamala na hadi sasa Polisi wanaendelea kumsaka mwanamke aliyefanya kitendo hicho cha kinyama ili aweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria
Chanzo: Alasiri 27/08/09
www.ippmedia.com