Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Mtikisiko wa Harmonize kujitoa WASAFI haukuwa mdogo japo japo kila upande ulijitahidi ku play low
Kuna sababu haziwekwi wazi sana lakini kuna moja ambayo ndio inaweza kuwa chanzo.. Na hii ni pale Harmonize alipoamua kuingiza siasa kwenye biashara pengine bila kushirikisha uongozi na viongozi wake kwa kupindua baadhi ya mashairi ya wimbo wake na kusifia wanasiasa
Wimbo asilia ni utunzi wake binafsi lakini gharama za kurekodi nk zilifanywa na WASAFI. Kwahiyo haikuwa sahihi kufanya lolote bila kushirikisha uongozi wa WASAFI ambao waliona hatari iliyopo ya kuchanganya SIASA na BIASHARA.
Pamoja na sababu nyingine zote hatimaye Harmonize alijitoa WASAFI lakini akiwa tayari ameshajitengeneza kwa utambulisho wake wa KONDE BOY.
Inapotokea ajali kishindo cha mwangwi wa sauti hufika mbali lakini walioko karibu hushuhudia majeruhi, vifo na uharibifu baada ya vumbi kutulia. Ni katikati ya Harmonize kujitoa WASAFI akapima upepo kwa kuachia UNO. Kazi yake ya kwanza akiwa nje ya WASAFI
Kwa haraka sana bosi wake wa zamani naye akaachia BABA LAO ili kuuthibitishia umma kwamba yeye bado yuko juu.
Nyimbo zote mbili zina kutambiana ndani yake na mafumbo na kwakuwa hazikuwa na maandalizi ya kutosha zimechuja haraka mno na katika hili Diamond ndio kapoteza zaidi kuliko Harmonize
Kwanza nyimbo zote mbili ni copy n paste. Harmonize anashutumiwa ku copy toka Kenya lakini Diamond iko wazi kabisa ka-copy wimbo alioshirikishwa Kongo DRC uliofanya vizuri sana. Alipokosea pakubwa Diamond ni kuangukia mtego uleule wa kuchanganya BIASHARA na SIASA, kwenye wimbo wake huo kawasifia wanasiasa tena wa upande mmoja
Diamond bila kufahamu na pengine panic ya Harmonize kujitoa WASAFI na kutoa wimbo fasta huku akitajwa kama mbunge mtarajiwa kwa njia moja kulimuumiza sana Diamond naye akaamua kusifia lakini kwa kufanya hivi kapoteza SEHEMU kubwa ya mashabiki wake
Msanii hapaswi kuwa na upande kwenye mambo ya wanasiasa, Mwanasiasa hana rafiki wa kudumu bali ana maslahi ya kudumu. Msanii anapoamua kuipa kisogo hadhira inayompenda kwa dhati na kuamua kuwageukia wanasiasa..Huyo siku zake zinahesabika.
All in all impact ya jambo hili itaonekana miezi michache ijayo kwa kila upande mwaka 2020 unaweza kuwa mchungu ama mtamu kwa wawili hawa.
Kuna sababu haziwekwi wazi sana lakini kuna moja ambayo ndio inaweza kuwa chanzo.. Na hii ni pale Harmonize alipoamua kuingiza siasa kwenye biashara pengine bila kushirikisha uongozi na viongozi wake kwa kupindua baadhi ya mashairi ya wimbo wake na kusifia wanasiasa
Wimbo asilia ni utunzi wake binafsi lakini gharama za kurekodi nk zilifanywa na WASAFI. Kwahiyo haikuwa sahihi kufanya lolote bila kushirikisha uongozi wa WASAFI ambao waliona hatari iliyopo ya kuchanganya SIASA na BIASHARA.
Pamoja na sababu nyingine zote hatimaye Harmonize alijitoa WASAFI lakini akiwa tayari ameshajitengeneza kwa utambulisho wake wa KONDE BOY.
Inapotokea ajali kishindo cha mwangwi wa sauti hufika mbali lakini walioko karibu hushuhudia majeruhi, vifo na uharibifu baada ya vumbi kutulia. Ni katikati ya Harmonize kujitoa WASAFI akapima upepo kwa kuachia UNO. Kazi yake ya kwanza akiwa nje ya WASAFI
Kwa haraka sana bosi wake wa zamani naye akaachia BABA LAO ili kuuthibitishia umma kwamba yeye bado yuko juu.
Nyimbo zote mbili zina kutambiana ndani yake na mafumbo na kwakuwa hazikuwa na maandalizi ya kutosha zimechuja haraka mno na katika hili Diamond ndio kapoteza zaidi kuliko Harmonize
Kwanza nyimbo zote mbili ni copy n paste. Harmonize anashutumiwa ku copy toka Kenya lakini Diamond iko wazi kabisa ka-copy wimbo alioshirikishwa Kongo DRC uliofanya vizuri sana. Alipokosea pakubwa Diamond ni kuangukia mtego uleule wa kuchanganya BIASHARA na SIASA, kwenye wimbo wake huo kawasifia wanasiasa tena wa upande mmoja
Diamond bila kufahamu na pengine panic ya Harmonize kujitoa WASAFI na kutoa wimbo fasta huku akitajwa kama mbunge mtarajiwa kwa njia moja kulimuumiza sana Diamond naye akaamua kusifia lakini kwa kufanya hivi kapoteza SEHEMU kubwa ya mashabiki wake
Msanii hapaswi kuwa na upande kwenye mambo ya wanasiasa, Mwanasiasa hana rafiki wa kudumu bali ana maslahi ya kudumu. Msanii anapoamua kuipa kisogo hadhira inayompenda kwa dhati na kuamua kuwageukia wanasiasa..Huyo siku zake zinahesabika.
All in all impact ya jambo hili itaonekana miezi michache ijayo kwa kila upande mwaka 2020 unaweza kuwa mchungu ama mtamu kwa wawili hawa.