Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Moja ya vitu ambavyo vimefanywa kwa vitendo katika kipindi hiki cha Kwanza cha utawala wa JK ni kuhakikisha kuwa Dodoma University inajengwa na kuanza kuchukua wanafunzi kwa ajiri ya masomo ya juu. Nimesikia inakadiriwa kuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi karibu 40,000 kwa wakati mmoja.Litakuwa jambo la manufaa makubwa kama chuo hiki kikiweza kukamilika katika muda na kutoa nafasi ambazo bado zinasumbua za kuwaendeleza watanzania kitaaluma katika fani mbalimbali. Kuna maandalizi yoyote mengine ya kuviwezesha hivi vyuo kuwa na contribution kubwa nchi yetu apart from majengo yanayojengwa? Nini tunaweza kufanya ambacho pengine hatufanyi ili kuviboresha vyuo vyetu viwe vizuri zaidi?