Wanajamvi habarini za miangaiko!
Bila kupoteza muda, mada iko hivi. Wakati niko chuoni actually kulingana na mishe zangu nilikuwa naingia kwenye vipindi vya jioni baada ya kazi.
Sasa kuna somo ambalo nilichelewa sana kuhudhuria vipindi vyake kama wiki tatu mfululizo ila siku yangu ya kwanza kuingia nilijitahidi kuwa mchangiaji kwenye discussions ili hata ikitokea nimekosa kuhudhuria siku nyingine mwalimu asinimind sana maana umachinga ulizidi.
Sasa kipindi kilichofuatia nilipata udhuru kikazi nikasafiri hivyo sikuhudhuria kipindi cha mwalimu huyu. Alikuwa dada mzuri na very smart upstairs kwa kweli.
Niliporudi darasani, wanafunzi wenzangu wote waliniambia nimchukue mwalimu mazima maana si kawaida alivyoniulizia. Sasa alipoingia yeye darasani hakuonyesha dalili yoyote ya kunishobokea ila baada ya pale tulipata likizo. Hapo ndo siku moja nashangaa mtu ananipigia akajitambulisha kuwa yeye ni mwalimu wangu na angependa twende movie kama sitojali.
Kwa kuwa nilishapata habari mapema nilikubali. Na siku hiyo ndo ilikuwa mwanzo wa safari ya mahusiano na mwalimu wangu.
Nikiri kwamba sikutaka kuwa na mahusiano naye ila nilipiga mahesabu ya madhara ya kutokukubali ombi lake hususani kwenye matokeo yangu ya mitihani niliogopa kufelishwa kwa kosa hilo.
Baada ya kumaliza chuo nilimpiga chini lakini
Vipi wewe Ungefanyaje?