JEKI
JF-Expert Member
- Aug 16, 2013
- 4,845
- 2,966
Kama mtakumbuka wiki ilopita ndo nimepeleka barua ukweni japo palitokea lapsha kidogo, wengi mmenishambulia na kunitisha nimekosa mke, dua la kuku.
Barua imejibiwa twende kupanga mahali, japo mke mtarajiwa kanitonya wamejiandaa kunibana kwenye mahali iwe kama faini, wanataka wanikamue milioni 3.
Kama ilivyo kawaida nimeamua kujipanga tena kwa kuandaa majembe ambayo yamefuzu katika nyanja nzima za bargaining, jana nikaongea na jembe moja ambalo ni uncle langu.
Jembe langu likaniambia maneno haya, "uncle ondoa shaka, nitafanya maajabu, nitawashangaza pale watakapopokea mahali ndogo kuliko kawaida, kwanza nitawaanzia mbali kama vile hatutaki. Halafu kwa ustadi wa hali ya juu kabisa tutapanda nao katika reducing balance, ikibidi tutapanda nao kwa elfu tano tano, huku tukiwapa maneno matamu, mwisho watachoka na tutajikuta tunaishia kwenye laki 3 au 4.....".
Niombeeni wakuu niikamilishe hii hatua tena bila jazba kama siku ya barua, nimejifunza na nimepokea ushauri wenu japo katika hatua hii lazima pia niibuke ili kuokoa jahazi kama litakuwa linazama.
Barua imejibiwa twende kupanga mahali, japo mke mtarajiwa kanitonya wamejiandaa kunibana kwenye mahali iwe kama faini, wanataka wanikamue milioni 3.
Kama ilivyo kawaida nimeamua kujipanga tena kwa kuandaa majembe ambayo yamefuzu katika nyanja nzima za bargaining, jana nikaongea na jembe moja ambalo ni uncle langu.
Jembe langu likaniambia maneno haya, "uncle ondoa shaka, nitafanya maajabu, nitawashangaza pale watakapopokea mahali ndogo kuliko kawaida, kwanza nitawaanzia mbali kama vile hatutaki. Halafu kwa ustadi wa hali ya juu kabisa tutapanda nao katika reducing balance, ikibidi tutapanda nao kwa elfu tano tano, huku tukiwapa maneno matamu, mwisho watachoka na tutajikuta tunaishia kwenye laki 3 au 4.....".
Niombeeni wakuu niikamilishe hii hatua tena bila jazba kama siku ya barua, nimejifunza na nimepokea ushauri wenu japo katika hatua hii lazima pia niibuke ili kuokoa jahazi kama litakuwa linazama.