Unawezaje kujua kama unatumika kwenye uhusiano? Hizi hapa dalili

MAMESHO

JF-Expert Member
Jul 5, 2011
1,366
1,622
Hapa kutumika namaanisha kuwa kwenye uhusiano kwa sababu fulani ambapo unaona ni kama mtego ambao huwezi kujinasua na unahisi kuna jambo ambalo haliko sawa lakini unaona bora liende na siku zisogee. Hali hii inaweka akili yako kutokuwa sawa na pia unaathirika kisaikolojia. Hizi hapa ni baadhi ya dalili.

1. Furaha yako ya kuwa na mahusiano imegeuka kuwa hofu ya kuachwa. Unakuwa na mawazo na unaonyesha kuchoshwa na uhusiano uliopo.
2. Hali yako inategemea hali ya uhusiano ikoje wakati mwingine unajiskia chini sana na wakati mwingine huna uhakika kama umependa au unajipendekeza.
3. Unajiskia kuharibu kila jambo zuri linalotaka kutokea na hujui kwa nini unajiskia hivyo.
4. Mara nyingi unamuuliza mpenzio kama kila kitu kiko sawa unajiskia kuna kitu hakiko sawa lakini haujui ni kitu gani.
5. Mara nyingi unajilinda sana na unachoongea na unaona kama unachosema unaeleweka vibaya.
6. Umekuwa mpelelezi unakagua simu, unacheki email, akaunti za mitandaoni na kusikiliza kwa makini simu zake.
7. Unajitahidi sana umfurahishe mwenzi wako, unajibidisha sana awe na furaha lakini unaona kama hufanikikiwi hata kwa kiwango kidogo na hujui ufanyeje.
8. Unajiona hutoshi na huwezi kutimiza matazamio ya mwenzi wako.
9. Unajiona huwa unakosea kosea na huwa unaomba samahani mara nyingi.
10. Likitokea tatizo dogo unashikwa sana hasira na unaongea kwa sauti ya juu na hata kulia
11. Unatumia mbinu ambazo huzipendi na ni kinyume na maadili uliyokuzwa nayo ili kumfanya awe na furaha na kushikilia uhusiano.
12.kueleza mawazo yako au hisia kunaonekana kumezuilika na mara nyingi unakaa kimya hata ikiwa kuna jambo hulifurahii au hulipendi.
 
Sa
Saivi nimezoea kua kwenye mahusiano hewa wala siumii naenjoy tuu zile moment tamu..mengine namuachia Mungu.
Kwa kawaida mambo huwa yanaanza vizuri sana. Halafu unaona yanaanza kwenda kombo na unajaribu kuyarejesha yawe mazuri kama yalivyokuwa mwanzo unakutana na vizingiti unajaribu kuvivuka na kuimarisha uhusiano, unaogopa kujitoa, unaskia hofu na huna uhakika ufanye maamuzi gani unaamua kubaki umening'inia imani inashuka kabisa mara mambo yanaanza kuimarika lakini hayadumu unajikuta umerudi hali ngumu zaidi inakuwa ni mzunguko wa pili. Unajiuliza hivi kwa nini pale mwanzo sikufanya maamuzi? Unajilaumu unaona mwenye makosa ni wewe. Utasumbuka sana kama hukujua kuwa ulitumika tu ili kutimiza lengo la aliyekutumia
 
Pia kikubwa kinachosababisha wengine watumike ni kugopa kupoteza wanachopata, au kukosa walochoahidiwa. unashindwa kujua uende mbele au urudi nyuma.hapo unakuwa umenaswa.
 
Hapa kutumika namaanisha kuwa kwenye uhusiano kwa sababu fulani ambapo unaona ni kama mtego ambao huwezi kujinasua na unahisi kuna jambo ambalo haliko sawa lakini unaona bora liende na siku zisogee. Hali hii inaweka akili yako kutokuwa sawa na pia unaathirika kisaikolojia. Hizi hapa ni baadhi ya dalili.

1. Furaha yako ya kuwa na mahusiano imegeuka kuwa hofu ya kuachwa. Unakuwa na mawazo na unaonyesha kuchoshwa na uhusiano uliopo.
2. Hali yako inategemea hali ya uhusiano ikoje wakati mwingine unajiskia chini sana na wakati mwingine huna uhakika kama umependa au unajipendekeza.
3. Unajiskia kuharibu kila jambo zuri linalotaka kutokea na hujui kwa nini unajiskia hivyo.
4. Mara nyingi unamuuliza mpenzio kama kila kitu kiko sawa unajiskia kuna kitu hakiko sawa lakini haujui ni kitu gani.
5. Mara nyingi unajilinda sana na unachoongea na unaona kama unachosema unaeleweka vibaya.
6. Umekuwa mpelelezi unakagua simu, unacheki email, akaunti za mitandaoni na kusikiliza kwa makini simu zake.
7. Unajitahidi sana umfurahishe mwenzi wako, unajibidisha sana awe na furaha lakini unaona kama hufanikikiwi hata kwa kiwango kidogo na hujui ufanyeje.
8. Unajiona hutoshi na huwezi kutimiza matazamio ya mwenzi wako.
9. Unajiona huwa unakosea kosea na huwa unaomba samahani mara nyingi.
10. Likitokea tatizo dogo unashikwa sana hasira na unaongea kwa sauti ya juu na hata kulia
11. Unatumia mbinu ambazo huzipendi na ni kinyume na maadili uliyokuzwa nayo ili kumfanya awe na furaha na kushikilia uhusiano.
12.kueleza mawazo yako au hisia kunaonekana kumezuilika na mara nyingi unakaa kimya hata ikiwa kuna jambo hulifurahii au hulipendi.
Mkuu una akili Sana trust me
 
Sijui kwanini huu Uzi wa maana una comments chache..maneno machungu ila ndiyo dawa..ukifikia kwenye hali hiyo Bora ufanye yako tu.
 
Sijui kwanini huu Uzi wa maana una comments chache..maneno machungu ila ndiyo dawa..ukifikia kwenye hali hiyo Bora ufanye yako tu.
Ni kweli kabisa. Maamuzi hayo ndio yanaamua kama tuwe huru au tuamue kubaki utumwani. Kuhusu uzi watauona, watatafakari, watakuja kusema chochote.
 

WAKUU,
TUNAKUMBUSHANA TU KUWA,

MHESHIMIWA #HASHIM_RUNGWE_SPUNDA ND'O RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUPITIA TIKETI YA CHAUMMA, CHAMA KINACHOENDA KUSHIKA DOLA MWAKA HUU MWEZI WA KUMI.

 
Hapa kutumika namaanisha kuwa kwenye uhusiano kwa sababu fulani ambapo unaona ni kama mtego ambao huwezi kujinasua na unahisi kuna jambo ambalo haliko sawa lakini unaona bora liende na siku zisogee. Hali hii inaweka akili yako kutokuwa sawa na pia unaathirika kisaikolojia. Hizi hapa ni baadhi ya dalili.

1. Furaha yako ya kuwa na mahusiano imegeuka kuwa hofu ya kuachwa. Unakuwa na mawazo na unaonyesha kuchoshwa na uhusiano uliopo.
2. Hali yako inategemea hali ya uhusiano ikoje wakati mwingine unajiskia chini sana na wakati mwingine huna uhakika kama umependa au unajipendekeza.
3. Unajiskia kuharibu kila jambo zuri linalotaka kutokea na hujui kwa nini unajiskia hivyo.
4. Mara nyingi unamuuliza mpenzio kama kila kitu kiko sawa unajiskia kuna kitu hakiko sawa lakini haujui ni kitu gani.
5. Mara nyingi unajilinda sana na unachoongea na unaona kama unachosema unaeleweka vibaya.
6. Umekuwa mpelelezi unakagua simu, unacheki email, akaunti za mitandaoni na kusikiliza kwa makini simu zake.
7. Unajitahidi sana umfurahishe mwenzi wako, unajibidisha sana awe na furaha lakini unaona kama hufanikikiwi hata kwa kiwango kidogo na hujui ufanyeje.
8. Unajiona hutoshi na huwezi kutimiza matazamio ya mwenzi wako.
9. Unajiona huwa unakosea kosea na huwa unaomba samahani mara nyingi.
10. Likitokea tatizo dogo unashikwa sana hasira na unaongea kwa sauti ya juu na hata kulia
11. Unatumia mbinu ambazo huzipendi na ni kinyume na maadili uliyokuzwa nayo ili kumfanya awe na furaha na kushikilia uhusiano.
12.kueleza mawazo yako au hisia kunaonekana kumezuilika na mara nyingi unakaa kimya hata ikiwa kuna jambo hulifurahii au hulipendi.
Mkuu yani hapa umenigusa kabisa.Yote ulosema nayapitia kwasasa. Nipo kwenye mahusiano ambayo sina uhakika wa nilienae kama kweli ananipenda au ndo natumika na ubaya zaidi tupo mbali kwa mda wa mwaka sasa.Natumia nguvu kubwa kutokutaka kumkwaza na kumpoteza ila mwenzangu wala ata hajali na mawasiliano kwake ni shida.
 
Mkuu yani hapa umenigusa kabisa.Yote ulosema nayapitia kwasasa. Nipo kwenye mahusiano ambayo sina uhakika wa nilienae kama kweli ananipenda au ndo natumika na ubaya zaidi tupo mbali kwa mda wa mwaka sasa.Natumia nguvu kubwa kutokutaka kumkwaza na kumpoteza ila mwenzangu wala ata hajali na mawasiliano kwake ni shida.
Pole sna
 
Back
Top Bottom