Unawakumbuka nguli hawa wa soka?

hapa ndio ukisikia no comment ndio hiyo zetu azam tu siunajua tena wazaliwa wasiku hizi sijui kina kayuni sijui huyu nani huyu mwameja wala sina time nao sie zetu ngassa na kina bocco ndio baadae watakuwa kina Pazi, Mkwasa..
 
Nakumbuka mzee, wakt nilikuwa standard three au four pale mpakani primary school, manzese dsm. Baazi ya wachezaji walikuwa hawa:

Beya Simmba
Mao Mkami
Hussein Masha
Paul Rwechungura
Madata Rubigisa
Deo Njoore
Rajabu Risasi

Wengi wa wachezaji walihamia simba ya dar. Je mnamkumbuka yule mtangazaji wa rtd aliyekuwa mwanza, utapenda akitangaza mechi ya pamba na simba au pamba na yanga.


Kaka kwa kweli upo juu kuna huyo kwenye red jamaa alikuwa noumer...nadhani pia alikuwepo Juma Amir kama sikosei...David Mwakalebela hakuwa kwenye hicho kikosi kabla ya kwenda yanga? Kipa wao alikuwa anaitwa nani?
 
kulikua na nyanda mmoja toka kanda ya ziwa KICHOCHI LEMBA[biashara shinyanga] duh alikua na mbwembwe sana langoni,kweli kila zama na enzi zake.
 
kulikua na nyanda mmoja toka kanda ya ziwa KICHOCHI LEMBA[biashara shinyanga] duh alikua na mbwembwe sana langoni,kweli kila zama na enzi zake.

Alikuwa RTC Kagera, akipiga kapelo kama alivyokuwa Manyika Petre wa Yanga.
 
Musimsahau Hussein Tindwa, aliekufa kiwanjani siku simba ilipocheza na Raccah Rovers ya Nigeria, hapo ilikuwa baada ya Simba kuipiga Mufulira Wandereres goli tano bila, kumbuka mechi ya mwanza iliochezwa uwanja wa taifa simba ilipigwa nne bila, huo ulikuwa ni mwaka 1978 sijui wangapi wanakumbuka hii

Tunakumbuka ila ilikuwa 1979, baada ya vita ya Uganda. Simba ilikuwa; Mahadhi, Kajole, Daudi Salum, Filbert Rubibira, Husein Tindwa, Nico Njohole, George(Best) Kulagwa, Abass Kuka, Thuwein Ally, somebody Mabaso, labda na Kikwa sikumbuki. Mwaka ule pia Pan Africa walicheza kombe la washindi na AS Vita ya Zaire sasa DRC. Kassim Manara akafunga magoli mawili ya hali ya juu. Vita walifunga moja kupitia kwa LOFOMBO. Kwenda Zaire AS Vita wakafunga goli la utata wakapata faida ya goli la ugenini tulilalamika AFC na kudai mkanda uonyeshwe sijui nini tulishindwa. Pan ilikuwa Pondamali, Jaffar Abdurahman, Mohamed Mkweche, Leodgard Tenga, Jela Mtagwa, Mohamed Rishard(Adolph), Godian Mapango, Muhaji Muki, Kitwana Manara, Sunday Manara, Kassim Manara. Nafikiri hii ilikuwa rekodi ya wanafamilia watatu kucheza mechi moja ya kimataifa, Sunday akitokea USA kupitia KIA na kuingia uwanjani baada ya timu kukaguliwa. Hata hivyo, kitwana aliharibu akarudisha mpira uliokuwa unaenda wavuni kwa tick tak ya Kassim Manara vinginevyo Kassim angepiga hat trick. Mwaka uliofuata 1980 ndiyo tulifuzu fainali za afrika kupitia goli la Peter Tino.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom