ARISTOTLE79
JF-Expert Member
- Apr 27, 2015
- 451
- 137
Picha ya kwanza na upara wangu naituma nikipokea dawa
Ya pili baada ya wiki4 ili washuhudie Kama Kuna mabadiliko
Ya pili baada ya wiki4 ili washuhudie Kama Kuna mabadiliko
Wabongo ndio maana wengine tumeumbwa na ngozi nyeusi lakini tunaamua kutumia madawa eti tuwe weupe, aliyekwambia kuwa weusi ni laana ni nani!?
Hivyo hivyo aliyekwambia kuwa kuwa na kipara ni ulemavu au laana ni nani!?
Umemjaribu mwanao tu umesharuka hewani utuuzie dawa! Makubwa haya.
Sasa makuje swali dume......TBS na hii menzie TFDA naolewa hii bishara yako ya nywele mpya?
Picha ya kwanza na upara wangu naituma nikipokea dawa
Ya pili baada ya wiki4 ili washuhudie Kama Kuna mabadiliko
Haya maelezo yanatia shaka sana.
Mama nikutakie biashara njema na nina imani utapata wateja wengi. ILA kwenye hizi picha umezipiga kijanja janja.
Ni mtu mmja ndio, ila picha ya juu umepiga kwenye paji la uso ila hii ya chimi umepiga utosini. Ndio maana watu wanakuwa na wasiwasi.
Nipo dodoma Napaje hiyo ya bure ili NIJE KUWAAMINISHA WASIOAMINI
Watu wabishi jf sijapata kuona sasa kama alipiga ya kwanza akiwa na kipara baada ya nywele kuota atafananeje na ya kwanza?
Pia sehemu amepiga tofauti kabisa
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
* Dada weka bei ya dawa ila nina swali huyo dawa inazingatia umri kama mtu ana miaka 50+ nywele zitaota?
Swali la pili,je ni kweli kuna dawa za kuongeza uume na hazina madhara?
Cc masaidada
Dodoma upo kwa Bi Rukia - 0653249898 barabara ya saba kwenye mix.
Bi Rukia ni mjasiriamali yeye kaununuwa na anasambaza ili nae ajipatie faida, kwa hiyo sidhani kama atakupa bure, na siwezi kuwalazimisha wajasiriamali watoe bure, bure ninautoa kwangu tu.
kumaliza mzizi wa fitna...unauzaje dawa yako?...sh ngapi na ni kwa kipimo kipi au gani?
Pich hizo zimepigwa sehemu tofauti na camera tofauti na wakati tofauti, na moja ni nje na nyingine ni ndani ya nyumba, hata miji ilizopigwa hizo picha ni tofauti.
Na hizo picha hazijapigwa ki professional kwa ajili ya advertising. Hizo ni picha zilizopigwa kawaida tu kwa ajili ya kumbukumbu.
Huyo ni mwanangu na ni mtu mmoja na sina haja ya kudanganya, nidanganye ili iweje?
Bei ngapi
Nina ushauri kwako kidogo kama utaona wafaa....waonaje ukibadili hizo picha ulizoweka hapo juu uweke zinazofanana...au uweke hizo ulizomtumia jamaa kwa PM....maana naona watu wanajikita kwenye kuhisi wanaibiwa kutokana na mwonekano wa picha badala ya kujikita kwenye huduma unayotoa..
Mie sikufahamu na naamini unachosema
Kila la kheri kwenye kuhudumia watu
Ni TZS 3,500 kwa pakti ya gram 100 ambayo unaweza kuitumia kwa wiki tatu hadi nne.
Nimejaribu kuweka kwenye PM nimeshindwa, sina ujuzi sana na haya mambo ya picha.
Lakini kama mtu antaka picha zaidi ninaweza kumtumia kwenye email au whatsapp halafu yeye aziweke.