Epuka sana bar wanazokunywaWataalamu wa mambo waibuke watwambie tunawakwepaje wanasiasa
Ahsante, trick nzuri.Juzijuzi Bakhressa kapewa ma eka kibao, unafikiri yametoka wapi?
Ni hayo hayo ya "wazee wetu" wasio na hati miliki.
Kuna maeneo makubwa yamehodhiwa sehemu kubwa za makazi na hayo ndiyo yenye utata zaidi, watu wanataka kuishi mtu anazuwia eneo kubwa na haliendelezi. Maeneo ya maporini (mbali na makazi ya watu hayana atizo sana).
Na njia rahisi sana ya kuhodhi hata pori liwe kubwa vipi ni kueneza mizinga ya nyuki na kulifanya sehemu ya kufugia nyuki, kuwa na "documents" rasmi zinazoonesha kuwa ni mfugaji wa nyuki na kuwashirikisha mali asili. Hapo hutaguswa.
Wana SiasaAkina nani?
Ndio akina nani hao?Wana Siasa
Ndani ya kijiji kuna milk I binafsi za ardhi,mzee fulani ana shamba lake,huwezi kusema ni mali ya kijiji,mama Fulani ana shamba lake,huwezi kusema anamiliki kwa hisani ya kijijimkuu,ni kweli unayosema lakini ukiacha shamba lako bila kuliendeleza halafu halijapimwa akija mwekezaji uchwara "anapewa" na uongozi wa kijiji kwa maelezo kuwa ardhi ni mali ya kijiji.
yaani kwa sera ya ardhi iliyopo sasa hivi hakuna pa kukwepea.
kulikuwa na zoezi la hatimiliki za vijiji sijui liliishia wapi.
Hata kama una hati mwekezaji akitaka shamba lako anapewa we unalipwa fidia tena kwa kupangiwa beimkuu,ni kweli unayosema lakini ukiacha shamba lako bila kuliendeleza halafu halijapimwa akija mwekezaji uchwara "anapewa" na uongozi wa kijiji kwa maelezo kuwa ardhi ni mali ya kijiji.
yaani kwa sera ya ardhi iliyopo sasa hivi hakuna pa kukwepea.
kulikuwa na zoezi la hatimiliki za vijiji sijui liliishia wapi.
Lakini huwezi kufutiwa tuu hati jumla jumla,kama alivyofanyiwa sumaye,na shamba likarudishwa serikalini.Hata kama una hati mwekezaji akitaka shamba lako anapewa we unalipwa fidia tena kwa kupangiwa bei
kuna viongozi wengi wa vijiji hawajitambui wala hawaelewi mwisho wa mamlaka yao kuhusu ardhi.ndio maana migogoro ya ardhi ni mingi sana.Ndani ya kijiji kuna milk I binafsi za ardhi,mzee fulani ana shamba lake,huwezi kusema ni mali ya kijiji,mama Fulani ana shamba lake,huwezi kusema anamiliki kwa hisani ya kijiji
Ni lake peke yake
Kijiji kama serikali,kinatakiwa kiwe na maeneo yake pekee kwa ajili ya mipango yake ya baadae
Baada ya utafiti mdogo nilioufanya,nimegundua njia pekee itakayokufanya ukwepe makucha ya wanasiasa hasa pale unaponunua/unapomiliki shamba,ni kuacha kulipima na kupata hati miliki
Nina sababu zifuatazo.
MOJA:
Ukipimisha shamba ukapata hati,unajiweka chini ya kamishna wa Ardhi na Rais ambao watakuwa na mamlaka ya kutengua umiliki wako.
Angalia wale wazee wetu wa vijijini,wanamiliki mapori na mapori lakini umiliki wao hautenguliwi japo hawayaendelezi,kwa sababu hawana hati miliki,wangekuwa na hati miliki tayari wanasiasa wangewachongea,hati zao zikafutwa
MBILI
Ukipima shamba lako na kupata hati miliki,wanakupangia muda wa kumiliki,eti miaka 33,66,99.
Lakini ukiwa huna hati miliki ya shamba lako,umiliki wako ni wa milele,hupangiwi miaka,ni vizazi na vizazi
TATU
Usipopima shamba lako,unakuwa huna adha ya kulipishwa kodi ya shamba kila mwaka.
Ambaye kapima anahenyeshwa na mzigo wa kodi mpaka anakoma
NNE:
Kama shamba lako halijapimwa na mwingine limepimwa,kama serikali ikitaka kuyachukua,wote mnalipwa fidia sawa.
TANO.
Ukipima shamba lako na kupata hati unakuwa na hatari zaidi ya kunyanganywa kuliko ambaye hajapima
SITA
Wachache mno,karibu asilimia sifuri ndio hukopeshwa na mabenki kwa kutumia hati za mashamba
Ukisikia Fulani kafutiwa umiliki wa shamba,ujue iliyofutwa ni hati,ili uwe salama dhidi ya wanasiasa,epuka kupimisha shamba lako,weka mipaka ya asili tu kama miti,katani........
Nimetoa angalizo tu mkuu.Hahaha! Tuelekeza shamba lilipo tuje tuluchukue tuliendeleze .
Nimetoa angalizo tu mkuu.
Ukiwa na shamba halina hati lazima wahangaike kujua liko wapi
Kama lina hati,wanavuta droo yenye hati zote za nchi nzima wanakupata na wanajua liko wapi
Au kama wame computerise,wanaingiza jina lako kwenye computer wanalisoma mpaka lilipo
Ni vyema kubaki na kamkataba ka manunuzi tu,shahidi mzee chakubanga