Unamkumbuka Crush wako wa utotoni? That was real and only unconditional love you will ever experience

Mimi crush wangu nilidate nae form 3 mpaka O level inaisha, wakati nilimpenda tangu form 1 naogopa kumwambia. Sikuwahi kuwa na crush mwingine zaidi yake mpaka leo. After graduation alinambia anataka tupate mtoto anahisi siku zake za kuishi ni chache, nikaogopa na kufanya nae matusi tena.

Tuliachana rasmi after form 6 aliponishutumu kuwa simpendi ninamcheat. Wapambe walikuwa wengi baina yetu maana couple ilikuwa maarufu, taarifa zake nilikuwa nazo ila zangu hana. Long distance ilituharibia tukaachana kwa vitisho. Sadly, kama alijua vile kwani sahivi hayuko sawa kwa afya ya akili na kupona 100% sidhani.

Nilimpenda na alinipenda. Kwanza nilimtongoza leo akakubali kesho, tangu hapo nikitongoza mtu akanizungusha kidogo naacha najua akikubali kwa kuchelewa analazimisha. Pili, alikuwa ananijua in and out hata nimfiche. Mapema kabisa nilijua mwanamke akikupenda sana anajua kusoma emotions zako kwa kukusikia, kukushika au kukutazama.
 
Mariamu la kwanza na la pili B akahama shule, Hadija la tatu mpaka la Saba B, akafata Judith,Kisha Zuhra advance. Chuo Rose! Sasa hivi naishi na niliyempa mimba!

Dunia haiko fair!
Mimi nilianza na mariamu shule ya msingi,akaja sauda o level, sasa naishi na niliyempa mimba yaani..daah
 
Siku ya kwanza kuanza darasa la kwanza macho yangu na moyo vinaangukia kwa bint mrembo alieitwa Mimash, nilimpenda sana na yeye alinipenda sana ila tuliogopana hadi kufikia darasa la 5 alihama yeye na familia yake na kuhamia Mombassa Kenya.

Tuliendeleza mawasiliano kwa njia ya Facebook messenger na yeye ndie alienitamkia kuwa ananipenda sana na hakuna kama mimi, ila baada ya miaka miwili yeye na familia yake wakahama tena na kurud kwao India, baada ya hapo hakukuwa na mawasiliano tena hadi leo hii.
Niliumia sana na ulinifanya nipitie maumivu yenye utamu wa kila nikikufikiria, na siachi kuzirudia zile sms tulizochat 12 years back.
 
Hehee nilikuwa namuelewa sana manzi mmoja hivi shule ya msingi Bunge mwaka 2002 alikuwa darasa la saba.
 
It took me 17yrs to be with her then i messed up kuja kushtuka kaolewa...siku nisipo muona usingizi ulikua hauji kabisa...nlipanga mafali kwenye ukuta wao nikimmis naenda kumchungulia...nisipomuona narusha mawe juu ya bati, akitoka nikamuona roho inatulia narudi home na amani tele...
 
Richie W. aka Richie Richie ( huyu tulipendana wote hadi tunamaliza lasaba B ila wote tulikuwa tunanata hakuna aliyetaka kumsemesha mwenzake. Tukawa tukasalimiana tuu na kupeana tabasamu basi). Sekondari tulipangiwa shule jirani tukawa tunaonana njiani saa ya kutoka au asubuhi kuingia shule.... alipopangiwa Minaki tukapotezana mazima hadi leo. Nilifatilia post za A level shule yao nikajua kapangiwa Minaki.... crush ya primary ikaishia hapo.)

Nkundwe ....( huyu hakujua kama nilimzimikia ila sababu alikuwa handsome waschana wengi walikuwa wanamsonga.... sikumbuki vizuri kama alihama tukiwa lasaba B au baada ya hapo alihamia ughaibuni.

Baada ya hapo nikawa mkaksi hadi nilipoingia chuo ndo nikaanza mahanjam 😋.
Kwa mara ya kwanza Nimepata mtu aliyetajwa humu naemfahamu, huyo nkundwe Ni mnyaki madam kasie, na amesharudi bongo ana mke wa kihaya na watoto wawili?????
 
Naamini waliokuwa wakipata tabu juu yangu Ni wengi mno, manake nilikuwaga karembo bhanaaaa😂 kapole Sana na kenye aibu nyingiiii, Kuna baadhi tukikutana wanataka watake advantage😂😂😂😂😂,

Mi nilimpenda mkaka flani tukiwa form 3 nae alinipenda nadhani manake alikuwa anaona sifa kweli kuwa karibu na mrembo wa shule🤩🤩, alikuwa anafanya poa class kunizidi nami nikaamza kukaza ili nimfikie nikampita na kumpita akaanza kunikunjia akawa anabana hata kunifundisha akaacha,, na kwa miluzi ilivyokuwa mingi nikampotezeaga, tulikutana 2015 ndipo kunitongoza nami nikamwambia nilimpendaga miaka hiyo,,, ila sio kwa utu uzimani tena, mi nikamuona km bado mdogo sana akili yangu iko mbele kuliko yake😤😤😤 na vile nimeolewa na mwanaume mkubwa karibu nusu ya umri wangu Basi wakaka niliosoma nao nawaonaga bado wavulana
 
Mimi crush wangu nilidate nae form 3 mpaka O level inaisha, wakati nilimpenda tangu form 1 naogopa kumwambia. Sikuwahi kuwa na crush mwingine zaidi yake mpaka leo. After graduation alinambia anataka tupate mtoto anahisi siku zake za kuishi ni chache, nikaogopa na kufanya nae matusi tena.

Tuliachana rasmi after form 6 aliponishutumu kuwa simpendi ninamcheat. Wapambe walikuwa wengi baina yetu maana couple ilikuwa maarufu, taarifa zake nilikuwa nazo ila zangu hana. Long distance ilituharibia tukaachana kwa vitisho. Sadly, kama alijua vile kwani sahivi hayuko sawa kwa afya ya akili na kupona 100% sidhani.

Nilimpenda na alinipenda. Kwanza nilimtongoza leo akakubali kesho, tangu hapo nikitongoza mtu akanizungusha kidogo naacha najua akikubali kwa kuchelewa analazimisha. Pili, alikuwa ananijua in and out hata nimfiche. Mapema kabisa nilijua mwanamke akikupenda sana anajua kusoma emotions zako kwa kukusikia, kukushika au kukutazama.
Sentensi ya mwisho ni elimu iliyojitosheleza .
 
Kuanzia darasa la 5 ndio nilikutana na bibie. Alikuwa mtu wa kupenda safari Sana,mwaka juzi kuna kibabu Cha Serbia kimemchukua moja kwa moja. Kaacha kutumia mitandao yote ya kijamii na account kafuta.
 
Kwa kweli my dear .Ila bado nahisi nitaenda kumwona siku moja .Uzuri alikuwa anajua one of his friend aliniambia akiwa mzima aliniulizia ila sasa sidhani kama angeendelea kuwa my crush .Ninachisikitika ni maisha yake ya sasa tu
Fanya hima ukamsalimie atafarijika sana, umsalimie kwa bashasha na hug kubwa ahisi kupona bibie
 
Back
Top Bottom