Unamiliki silaha ili iweje?

Unamiliki silaha ili iweje?

Dunia ya leo mkuu wote tukiwa na mawazo kama yako mshana jr. Magaidi watatawala dunia na mauaji ya watu wasio na hatia yataongezeka
Hapana sijamaanisha hivyo nilichomaanisha ni ule umiliki wa mtu mmoja na sizungumzii majeshi wala vyombo vya usalama
 
Uwepo wa Mungu na kumiliki silaha hakufungamani wala kuleta conflict kama unayotaka kuelezea. Nitamuomba Mungu sawa, lakini wezi na wanyama wakali wanapokuvamia, utawakabili au utaanza maombi?

Huku tuendako, utasema tusijishughulishe kujifunza namna ya kuvuka barabara kwa kuwa Mungu atatulinda tusigongwe. Badala yake, ulipaswa kuwaasa watu wamuombe Mungu awape hekima ya matumizi ya silaha
Kuna mahali nimelijibu hili mimi mwenyewe binafsi ninazo silaha zangu ndani lakini sio mabunduki na mabastola
 
Hapana sijamaanisha hivyo nilichomaanisha ni ule umiliki wa mtu mmoja na sizungumzii majeshi wala vyombo vya usalama
Mkuu umeangalia matukio machache ambayo mimi naweza kuyaita ajali lakini hujaangalia matukio ya kuokolewa watu na Mali zao ambayo ndiyo mengi zaidi, ajali zipo hata kwenye majeshi na mifano ipo
 
siraha pesa, bunduki mzigo tu, kwan unaish kwa wasiwasi muda wote unawaza imekaa vzr ulipoihfadh nk.
 
Mshana hapa umekuwa upande mmoja, infact hata mm kuna wakat nilishawah kufikir hivyo kuwa silaha si muhimu, as long as usalama upo na mtu hujatengeza maadui wa kimaisha au kibiashara. Ila muda unavyoenda unagundua sio sahihi, panafika pahala inabid kuzuia vitu vinavyoweza kuepukika. Kuna vijana hawana ajira wanapiga vyuma, sijui karate na mazoezi mengine yenye nia mbaya kwa vijana na wananchi wengine, sasa ikiwa ww ni mtu uko bize huwez ku countereffect hayo mazoez, afterall hujui how intensive they are, njia pekee ni cha moto.
Kingine ni uvamiz wa mara kwa mara, boda boda, sijui misikitin, sema huwez kupambana na watu wenye silaha sababu ile ni timing.
 
3f51220ba9b2d06ad7ab32a687ff449d.jpg
916f4135e6f9b38818f3ce8551195bbb.jpg
Kuna jibu moja rahisi sana kwenye hili swali nalo ni kwa ajili ya ulinzi binafsi (pengine na familia)...lakini si kweli hata kidogo! Silaha unayo miliki ni kifo binafsi na si ulinzi binafsi , haina tija kwako haikusaidii kwa asilimia unazofikiri inakupa kujiamini kusiko halisi

Kama wewe ni mwamini wa Mungu mmoja unayeamini uwezo na ulinzi wako kwenye maisha yako kubeba silaha ni kujichanganya kiimani kwamba sasa unaamini katika ulinzi wa Mungu au silaha?

Silaha haina matokeo mema silaha chake ni kujeruhi kuua na kuangamiza, ni sahihi Kabisa kwamba tunapaswa kujihami tunapaswa kujilinda lakini kamwe si kwa mtindo huo wa kubeba silaha nzito nzito , kwani umekuwa askari wewe? Kwani ni mwanajeshi wewe? Your mind is the most lethal weapon and your faith to the Almighty creator

Silaha ni kwa ajili ya wasiojiamini silaha ni kwa ajili ya wasio waamini, silaha ni kwa ajili ya wenye rohombaya dhulmati na wanaoogopa kifo! Silaha ni kwa ajili ya maadui...kama unajiamini kama unaamini katika ulinzi wa Mungu kama huna roho mbaya sio dhulmati na huna maadui huna haja ya kubeba silaha

Wengi wamekufa wakiacha silaha zao bila kuzitumia hata siku moja...silaha ni biashara silaha ni uchumi wa watu ili wao waweze kuishi inabidi wauze silaha? Na ili wauze vizuri inabidi wakuandae kisaikolojia na wakuandalie mazingira ya woga na kutojiamini ili tu umiliki silaha ...ni aina fulani ya kucheza na akili za watu

Naamini kati yetu tutakaosoma hapa tuna berreta zetu kwenye makabati full loaded! Lakini mbona umeendelea kuugua? Mbona kuna mazingira mengi tu umeepushiwa kifo bila ya msaada wa hilo lichuma lako ulilolinunua kwa bei ghali sana?

Mrudie Mola wako ukatubu na kuungama, kwa kutokuwa na imani thabiti juu ya ulinzi wake...! Maisha yako na mustakabali wako viko mikononi mwake na sio kwenye bunduki lako , ni yeye ajuaye kutoka kwako na kuingia wako sio bastola iliyoko kabatini chuma kisichosema

Eti hata fulani naye a nazo mbili? za nini?
Mungu wetu tunayemwamini ndio kila kitu kwenye maisha yetu
Duu nilidhani hii mada ni ya Kisayansi kumbe ni ya kiimani!! Nendeni mkahakiki siraha zenu jamani, tusimuachie kila kitu Mungu, jipiganie huku ukiomba sana msaada wa Mungu ndiyo maana hata Misikiti au Makanisa yana walinzi.
 
Mshana hapa umekuwa upande mmoja, infact hata mm kuna wakat nilishawah kufikir hivyo kuwa silaha si muhimu, as long as usalama upo na mtu hujatengeza maadui wa kimaisha au kibiashara. Ila muda unavyoenda unagundua sio sahihi, panafika pahala inabid kuzuia vitu vinavyoweza kuepukika. Kuna vijana hawana ajira wanapiga vyuma, sijui karate na mazoezi mengine yenye nia mbaya kwa vijana na wananchi wengine, sasa ikiwa ww ni mtu uko bize huwez ku countereffect hayo mazoez, afterall hujui how intensive they are, njia pekee ni cha moto.
Kingine ni uvamiz wa mara kwa mara, boda boda, sijui misikitin, sema huwez kupambana na watu wenye silaha sababu ile ni timing.
Kuna kitu nimeandika wengi hawakukizingatia nimesema your mind is the most powerful weapon....
 
Mkuu umeangalia matukio machache ambayo mimi naweza kuyaita ajali lakini hujaangalia matukio ya kuokolewa watu na Mali zao ambayo ndiyo mengi zaidi, ajali zipo hata kwenye majeshi na mifano ipo
Ila kuna point wengi hamkuizingatia kuhusu powerful mind..hebu tujaribu kuwa na mitazamo yote
 
Wengi wenye silaha Ni waoga na hawawezi kuzitumia wakati muafaka,ipo mifano mingi utakuta mmevamiwa mahali lakini mwenye bastola mkiambiwa Lala chini ye ndio wa kwanza anaogopa na anatetemeka hata kuishika hawezi,wengi wao Ni "mabitoz nyangema"
 
Mmh hapana hizo physical powers zinatokana na powerful mind
Ukikutana na mhalifu ni bora mtu moja mwenye Silaha ya kumdhibiti huyo mhalifu kuliko watu mia wenye powerful mind wasio na Silaha ya kumdhibiti huyo mhalifu
 
Ukikutana na mhalifu ni bora mtu moja mwenye Silaha ya kumdhibiti huyo mhalifu kuliko watu mia wenye powerful mind wasio na Silaha ya kumdhibiti huyo mhalifu
Powerful mind unajua ina uwezo wa ku neutralise any delicate or dangerous situation
 
Kwa anaeamini uwepo wa Mungu ni kweli kwamba kumtegemea Mungu ni jambo muhimu sana. Binadamu tuna matatizo mengi sana tunayopambana nayo katika maisha yetu. Kuna maradhi, maadui wetu wanaopatikana kutokana na sababu mbalimbali n.k. Wakati tunapopatwa na maradhi hatukai na kusema Mungu atatusaidia bila kwenda hospitali kupata matibabu (dawa).Vilevile katika kukabiliana na maadui hatupaswi kukaa tu na kusema Mungu yupo atatulinda bila kuchukua hatua stahiki. Ndiyo maana tunajenga nyumba, tunaweka milango na mageti na vifaa vingine vinavyotusaidia kwenye masuala ya usalama kama security lights, CCTV cameras n.k. Na hivi kwa hakika vimesaidia au kuokoa wengi. Kitu muhimu kwa anaeamini uwepo wa Mungu ni kujua kuwa pamoja na hayo yote hapo juu lakini hayawezi kufanikiwa bila nguvu ya Mungu.

Nitoe mfano mmoja kutoka kwenye biblia. Kwa wasomaji wa biblia mnaelewa kisa cha Daudi (mwisraeli) aliyemuua mfilisti Goliathi kwa kutumia kombeo (sling) na mawe. Huyu Daudi alikwenda na kombeo na mawe ili kupambana na mfilisiti Goliathi ambaye alikuwa ni jitu kubwa na lenye nguvu sana lakini Daudi akiwa na silaha hiyo na mawe yake mfukoni alimwomba Mungu wake na kisha akaingia vitani na akaweza kumshinda adui yake Goliathi. Yaani Mungu aliweza kubariki silaha (kombeo na mawe) aliyokuwa nayo Daudi.

Ukiangalia huo mfano utaona kwamba kuwa na silaha kama bunduki (kombeo) na risasi ( mawe) siyo jambo baya na haimaanishi kuwa umiliki wake unaashiria kutomtegemea Mungu. Kitu muhimu ni kwamba umiliki wa hizo silaha uwe ni kwa kufuata sheria, silaha zitumike kwa malengo halali (kujilinda) na pia umiliki wa silaha usitufanye kuwa na kiburi na kudhani kuwa kwa vile tuna bunduki hizo basi Mungu hana nafasi tena juu ya maisha yetu na hizo silaha zetu. Hayo ndiyo mawazo yangu.
Huwezi kujilinda mwenyewe kwa silaha yako mkuu...labda umlinde mtu mwingine kwa silaha yako.ni wengi wenye silaha wanavamiwa na kuuawa bila kutumia silaha zao.
 
Wengi wenye silaha Ni waoga na hawawezi kuzitumia wakati muafaka,ipo mifano mingi utakuta mmevamiwa mahali lakini mwenye bastola mkiambiwa Lala chini ye ndio wa kwanza anaogopa na anatetemeka hata kuishika hawezi,wengi wao Ni "mabitoz nyangema"

Mkuu ukiwa na silaha mkafanyiwa timing, labda bar au popote kwenye kusanyiko, usije hata siku moja ukathubutu kutoa silaha hata kama unayo, the grave mistake tht even a trained commando would thnk twice, sababu hao majambazi wameweka kwenye plan yao kuwa upo uwezekano kukawepo na watu wenye silaha, bora ingekuwa raia tu mwenye silaha, lakin wanaogopa zaid kuwa anaweza kuwepo askar au polis au mjeda, au hata usalama na akawa pia na silaha so wanakuwa wanawa monitor wote.
Niliona pale mawela sinza jamaa walivamia, mlinz akijidai eti hawamuon akaanza kupiga simu, ww, hee jamaa alimtungua kutokea mbali kishenzi, wale jamaa nadhan huwa ni askari.
Me naongelea watu wachache wameingia sehem wana mapanga, au vibaka wale wa mtaani wanakuja na silaha ndogo ndogo.
 
Powerful mind unajua ina uwezo wa ku neutralise any delicate or dangerous situation
Mshana acha siasa kwenye ugaidi, hebu fikiria kilichotokea kwenye msikiti huko Mwanza kama angekuwepo mtu mmoja tu mwenye Silaha sasa hivi ingekuwa habari nyingine
 
Mshana acha siasa kwenye ugaidi, hebu fikiria kilichotokea kwenye msikiti huko Mwanza kama angekuwepo mtu mmoja tu mwenye Silaha sasa hivi ingekuwa habari nyingine
Kweli kabisa ndugu yangu hii sio siasa na vile vile iko beyond ugaidi tena hii kitu tuiweke pembeni maana wale walivamiwa it was a preplanned attack...kumbuka pale ni nyumba ya ibada wala sio bar huwezi hata kama una silaha yako ukaingia nayo pale..unajua powerful mind is beyond hizi illusions za silaha it's something very big natamani kuandika sana lakini niko mishemishe ngoja nitulie
 
Back
Top Bottom