Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

Unakumbuka wanyonya damu mashuleni?

Chemwali

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2011
Posts
397
Reaction score
178
Hivi jamani hili suala ni nani alikuwa analianzisha ?maana katika miaka yangu yote 7 ya primary school sijawahi kuwashuhudia though story zilikuwa haziishi..siku nyingine tunanusurika na kuumia kisa mmoja kalianzisha kaona wanyonya damu.je ni kweli walikuwepo ama ilikuwa ni imani tu
 
Hivi jamani hili suala ni nani alikuwa analianzisha ?maana katika miaka yangu yote 7 ya primary school sijawahi kuwashuhudia though story zilikuwa haziishi..siku nyingine tunanusurika na kuumia kisa mmoja kalianzisha kaona wanyonya damu.je ni kweli walikuwepo ama ilikuwa ni imani tu

Mi nadhani chanzo chake kilikuwa ni zile blood drives za asasi kama Red Cross. Sasa labda kutokana na ufinyu wa kampeni za kuwaelimisha watu kuhusu hilo watu wakaamua kuziba hilo ombwe kwa kuja na nadharia zao.

Nakumbuka siku moja wakati niko darasa la tano kuna jamaa mmoja aliropoka 'mumiani hao wanakuja' halafu huyo akatoka nduki. Basi darasani si kukanyagana kila mmoja akitaka kunusuru maisha yake kwa kukimbilia anapojua yeye.

Wengine mashapu shapu kaa sisi tulitokea dirishani. Baada ya kama dakika ishirini hivi hali ikatulia tukarudi tena darasani.
 
Mi nadhani chanzo chake kilikuwa ni zile blood drives za asasi kama Red Cross. Sasa labda kutokana na ufinyu wa kampeni za kuwaelimisha watu kuhusu hilo watu wakaamua kuziba hilo ombwe kwa kuja na nadharia zao.

Mi nakumbuka siku moja wakati niko darasa la tano kuna jamaa mmoja aliropoka 'mumiani hao wanakuja' halafu huyo akatoka nduki. Basi darasani si kukanyagana kila mmoja akitaka kunusuru maisha yake kwa kukimbilia anapojua yeye.

Wengine mashapu shapu kaa sisi tulitokea dirishani. Baada ya kama dakika ishirini hivi hali ikatulia tukarudi tena darasani.

hahah umenikumbusha jina lingine la mumiani hahahah yes chanzo iakuwa nadhani redcross maaana tulikuwa tunaambiwa magari yao yana msalaba
 
yes you are right nyani ngabu ila kwa kizazi cha Mulugo sidhani wamelisikia au kuliona.
 
Stori zalongi sana duh! tuliokuwa tunasoma shule za mbali unapita msituni unafika Shule roho uko mikononi, nilikua nakimbia kutoka nyumbani mpaka Shule
 
Stori zalongi sana duh! tuliokuwa tunasoma shule za mbali unapita msituni unafika Shule roho uko mikononi, nilikua nakimbia kutoka nyumbani mpaka Shule

Umesoma mlimani nini?maana dah msitu ulikuwa mkubwa..lazima tukimbizwe.
 
Mama alikuwa ananiuliza hao wanyonya damu,wanakuja kila siku maana ata kama kuna mwalimu mlangu autoshi tunavyokimbia..watoto wetu haya mambo wanayakosa mbona...
 
Ha ha ha hata mimi nimekumbuka mnyonya damu...aisee utoto raha hata nilikuwa sielewi maana yake nini nikisikia watu wakisema tu na mpaka sasa bado sielewi!!🙂
 
Wale waliokuwepo Iringa miaka 80 kuna jamaa aliogopeka sana kwa tuhuma hizo alikuwa akifahamika kama Sekeni
 
Heheheheh usinikumbushe
Wakati niko darasa la pili
Kida lilikuja gari jekundu sijui nani akatangaza kuwa ni la wanyonya damu

Ilikuwa patashika shule nzima
 
yaani mi nakumbuka kuna siku tupo shule mvua inanyesha mtu akaanzisha nyonya damuuuu,tuliruka madirishani hatukujali hata mvua kama begi hujafunga madaftari yote chini...unakimbia anayekukimbiza humuoni yaani acha tu
 
Dah! hii ni moja ya 'hoax' ambazo zilishika hatamu miaka hiyo tukiwa bado makinda...

Nakumbuka nikiwa Mbeya kuna jina la Msekwa(sio Pius Msekwa) lilikuwa maarufu sana...

Na kipindi kile mji haukuwa umejengwa sana kwani kulikuwa bado na ule uoto wa misitu ya mikaratusi...

Sasa ilikuwa inasemekana huyu bwana ni nyonya damu na anatembelea kibito chekundu na hakitoi mlio...

Suala la kwenda shule asubuhi na mapema au kurudi nyumbani kigiza kikiwa kimeingia ilikuwa tafrani sana...
 
yaani mi nakumbuka kuna siku tupo shule mvua inanyesha mtu akaanzisha nyonya damuuuu,tuliruka madirishani hatukujali hata mvua kama begi hujafunga madaftari yote chini...unakimbia anayekukimbiza humuoni yaani acha tu

Yani umetukumbusha mbali kweli..me mama alikuwa anielewi naacha kila kitu..kisa wanyonya damu..yani nimecheka kweli..utoto kweli raha.
 
Hahahaaaa ukikatiza kipori lazima mkojo ukubane ukihofia kukutana na masalo
Yani ilikuwa tabu kweli..tulikuwa kama tunakatiza kipori lazima tuwe wengi pale sheli..maana dah wale wajinga walikuwa wanatuvizia kweli..unakumbuka mpaka mama mmoja wa kihaya alianzisha daladala konda yeye ndio kama unaogopa kukatisha kipori anatubeba..ukichelewa inakula kwako.
 
mi nakumbuka kuna mtu alitutisha kuwa kakuta mbuzi anasoma gazeti chooni, dah watu tulikuwa tunarudi home na haja zetu kwa uoga. utoto bana!
 
Back
Top Bottom