Unakumbuka semina Elekezi?

Unakumbuka semina Elekezi?

Mashamba

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2011
Posts
418
Reaction score
103
Wadau wa jukwaa, wasalaaam.
Hiki ni kipindi cha lala salama kwa utawala wa JK na sio vibaya tukiangalia moja ya mbinu aliyoanza nayo, kulifanyika semina elekezi kwa ngazi nyingi za juu pale Ngurdoto hotel.Katika kujadili hili tuangalie ufanisi na changamoto zilizojitokeza katika utawala wake na mchango wa zile semina na nyingine nyingi, pia ikumbukwe huu ndio utawala uliopatwa na misukosuko mingi. Tujue kama walienda kutafuna kodi zetu au kuna kitu wametuengezea .

Karibuni,
Mashamba.
 
Mwendesha semina hizo kituko karibi mawaziri wote waliohudhuria kawafuta kazi kwa wizi, kifupi ulikuwa usanii wa hovyo kabisa
 
Wanajamvi nikumbusheni tarehe ya kura ya maoni ya katiba iliyopendekezwa ni lini nijiandae
 
Ni vema watanzania wakati mwingine tuwe waungwana si kila wakati kuwa hamnazo. Kama watu wamefanya vibaya katika wizara zao mlitaka waendelee kubaki serikalini halafu bdae tena mlalamike kuwa utawala mbovu huu fulani kaharaibu lakini bado yupo ofisini....la hasha ni vema sasa tuanze kubadilika na watu wasiotaka kubadilika ni wakupuuzwa.
 
So hapa tunafunga maesabu sasa , tatizo walikua mawaziri tu au hata ngazi za juu?
 
Wadau wa jukwaa, wasalaaam.
Hiki ni kipindi cha lala salama kwa utawala wa JK na sio vibaya tukiangalia moja ya mbinu aliyoanza nayo, kulifanyika semina elekezi kwa ngazi nyingi za juu pale Ngurdoto hotel.Katika kujadili hili tuangalie ufanisi na changamoto zilizojitokeza katika utawala wake na mchango wa zile semina na nyingine nyingi, pia ikumbukwe huu ndio utawala uliopatwa na misukosuko mingi. Tujue kama walienda kutafuna kodi zetu au kuna kitu wametuengezea .

Karibuni,
Mashamba.

Mkuu umesahau kidogo.

Kabla ya semina elekezi alizunguka kila wizara, akasikiliza matatizo yao na kutoa maelekezo, lakini sidhani kama alifuatilila tena utekelezaji wa maagizo yake....!!
 
Kwa ufupi haikuzaa matunda memea labda kujuana na kuoneana aibu tu na nchi kwenda ovyo
 
Mkuu umesahau kidogo.

Kabla ya semina elekezi alizunguka kila wizara, akasikiliza matatizo yao na kutoa maelekezo, lakini sidhani kama alifuatilila tena utekelezaji wa maagizo yake....!!

Itakua alikuja kuyasahau kutokana na haraka ya kwenda kujitambulisha nchi za ulaya na amerika mkuu
 
Itakua alikuja kuyasahau kutokana na haraka ya kwenda kujitambulisha nchi za ulaya na amerika mkuu

Inaelekea baada ya kutoa maelekezo alitoa amri ya nyuma geuka mbele tembea. Yeye naye akageuka nyuma na kupeana visogo na watendaji. Sasa wanarudi na ahadi za kutatua shida zilezile badala ya kutuambia wamefanya nini.
 
Back
Top Bottom