Emc2
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 16,808
- 16,951
- Thread starter
- #141
Nadhani upo nje ya mada. Samahani lakini kwa kuandika maandishi meeengi ukiwa nje ya mada. Hapa tunaongelea ni namna gani Katiba ya chadema inavyo wanyima uhuru wabunge wake.Je, hivyo ndivyo unavyotafasiri sheria/kanuni?
Nafikiri kama lengo lako ni kuelimisha watu kuhusu mapungufu ya kisheria yaliyomo ndani ya Katiba ya CDM, ni bora ukafanya hivyo kwa kufanya uchambuzi bora na wenye kukidhi haja badala ya kukimbilia kuleta sensational quotations of the said party Constitution which may not bring your ill-intentions at home. Nimeendelea kusoma hoja zako nyingi, hakika sio uchambuzi wa kisheria kama unavyojidai kufanya, bali ni ujinga ndio unaoendelea kuandika.
Kwa taarifa yako, kila jambo linalotengenezwa na mwanadamu hapa duniani linaweza kufikia mwisho wake au kubadilisha kadri mwanadamu huyo atakavyoona inafaa, hata Katiba ya Tanzania, 1977 (as amended), inaweka masharti ya kuamua kufanya jambo fulani lifike ukomo wake au vinginevyo.
Mfano, ukisoma Ibara ya 98 ya Katiba utakuta maneno haya:
98.-(1) Bunge laweza kutunga Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii kwa kufuata Kanuni zifuatazo:-
(a) Muswada wa Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii (isipokuwa yale yanayohusika na
aya ya (b) ya ibara hii ndogo) au masharti yoyote ya sheria yoyote iliyotajwa katika Orodha ya Kwanza kwenye Nyongeza ya Pili utaungwa mkono kwa kura za Wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wabunge wote;
(b) Muswada wa Sheria kwa ajili ya kubadilisha masharti yoyote ya Katiba hii au masharti yoyote ya Sheria yoyote yanayohusika na jambo lolote kati ya mambo yaliyotajwa katika Orodha ya Pili kwenye Nyongeza ya Pili iliyoko mwishoni wa Katiba hii, utapitishwa tu iwapo utaungwa mkono kwa kura za Wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Zanzibar.
(2) Kwa madhumuni ya ufafanuzi wa masharti ya ibara ndogo ya (1) kubadilisha masharti ya Katiba hii au masharti ya sheria maana yake ifahamike kuwa ni pamoja na kurekebisha au kusahihisha masharti haya au kufuta na kuweka masharti mengine badala yake au kusisitiza au kubadilisha matumizi ya masharti hayo
Kwa msaada tu, mambo yaliyotajwa katika Nyongeza ya Pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo yanaweza kubadilishwa au kufutwa ni haya hapa:
ORODHA YA PILI
(Imetajwa katika ibara 98 (1) (b))
Mambo ambayo mabadiliko yake yahitaji kuungwa mkono na theluthi mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Visiwani.
1. Kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano.
2. Kuwapo kwa Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano.
3. Madaraka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
4. Kuwapo kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano.
5. Madaraka ya Serikali ya Zanzibar.
6. Mahakama Kuu ya Zanzibar.
7. Orodha ya Mambo ya Muungano.
8. Idadi ya Wabunge kutoka Zanzibar.
KWA HIYO, SIONI AJABU KAMA KATIBA YA CHAMA FULANI IKAAMUA KUWEKA MASHARTI YA KUVUNJA CHAMA CHAO, NA ZAIDI, BAADA YA KUSOMA HIVYO VIPENGELE VYA KATIBA YA CDM, NIMEGUNDUA WALICHOFANYA NI SAHIHI KWANI HUWEZI KUVUNJA CHAMA BILA KULIPA MADENI YA WATU, if any.
Let's learn to do impeccable arguments.
_____________
Hapa wewe naona kidogo umepotoka samahani lakini kama litakuwa hilo tusi kwako.