Unajiona kabisa una sura mbaya yet unaenda kuzaa na mtu mwenye sura kama yako. Watoto wako watateseka sana kupata kazi na wenzi

Samia atosha tukutane2030

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
17,169
Reaction score
48,681
Hakuna mtu mwenye pesa zake, elimu yake au resources zake atakubali kuoa mke au kuolewa na mume mwenye sura mbaya.

Siku hizi wasomi wapo kila kaya, ili utoboe kupata kazi ya maana lazima connection au reception/ sura nzuri maana kazi zile za mabavu sasa haziko nyingi na kama zipo hazina maslahi.

Sura nzuri ni kigezo muhimu sana kwenye kupata fursa dunia ya leo.
Mtu mwenye sura nzuri automatically kila mwanadamu hupenda kuwa karibu naye bila kujali jinsia yake.

Pambana uoe mrembo au uolewe na handsome muzae watoto wazuri.
Kilichomfanya Potifa amnunue Yusuph na kumweka ndani na si mashambani kama watumwa wengine ni sura nzuri. Hata alipofungwa mkuu wa Magereza akampa nafasi nzuri (unyapara).

Mtoto mzuri hupewa upendeleo kuanzia chekechea mpaka university.
Wenye sura mbaya na hamtaki kutafuta wenzi wazuri myajitetea ooh sura sio akili.
Kila mtu ana akili , kuna msemo mmoja wa kijeshi unasema "Soldiers are made not born" kwamba mtu yeyote isipokuwa mlemavu tu ndiye hawezi kuwa mwanajeshi. Mwanajeshi bora huandaliwa na si kwamba kazaliwa na uanajeshi.
Kwahiyo mambo ya sura sio akili mara sura sio uchapakazi ni hoja mfu. Mtu yeyote anaweza kuwa mchapakazi au mvivu kulingana na maandalizi.
Sura ndiyo itaamua watu wakupe upendeleo au wakutreat vipi.
KABLA HATUJAANZA KUTUJAANZA KUTUKANANA NIJIBU HILI SWALI 👇
Una kampuni yako ya sales na kuna mabinti 2 wamekuja kuomba kazi, wote wana elimu sawa, wote ni fresh ndo kwanza wamemaliza chuo mmoja sura ya babu mmoja sura ya malkia. Yupi utaanza kumfikiria kumpa ajira?
 
Ni nani aangalie sura siku hyo ya haki.....siku ya hukumu,basi tenda wema kwani sura sio roho

Na akapita hivii
 
Sura nzuri sio kigezo cha kuwa mchapa kazi, ndio maana taifa hili linafeli
 
Yani unaweza ukazaa mtoto halafu akawa na akili duni kama hizi 🚮.



Mungu niepushe na janga kama hili!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…