mchajikobe
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 2,652
- 1,238
Kuna jamaa yangu mmoja na ni mtu wangu wa karibu sana,anampenzi wake wa kike ambaye ameshamtambulisha hadi kwao,ila kunamambo ambayo yanamtokea jamaa huyu ambayo amejaribu kuniomba ushauri,na naomba wana JF wenzangu mumsaidie kwa ushauri,siku moja alimpigia simu huyo mpenzi wake na kujuliana hali,mpenzi wake akamwambia kuwa yupo nyumbani kwake(yaani kwa huyo mwanamke),baadae akakutana na huyo mwanaume wake mitaa ambayo wote sio yakwao,lakini huyo mwanamke alikuwa ameongozana na mwanaume mwingine,na mara alipomuona yule mwanaume wake ghafla alishtuka na kuzuga kwa kumuuliza vipi mbona upo mitaa hii,hatuagani?kipindi hicho yule mwanaume mwingine alendelea na kwenda kumsubiri yule mwanamke mbele,mwanamke akamwambia yule mtu wake nafika hapo mbele na kumfuata yule mwanaume bila ya kumtambulisha na kuendelea na safari.Siku nyingine wakati wamekaa pamoja ikaingia msg kwenye simu ya mwanamke,ikiwa imedisplay jina la aliyetuma na msg ilisomeka kuwa nakupenda sana,mwanaume alipo muuliza huyu ninani,binti akajibu simjui nilikutana naye tuu barabarani,sasa kama nikweli walikutana barabarani yanini alisave namba yake?Sasa juzi mwanamke kampigia simu huyo mpenzi wake kuwa anahitaji mpenzi wake aende kwake,jamaa kweli kaenda kwa huyo mwanamke alipofika akakuta huyo binti anaelekea maliwatoni,wakakaa takribani masaa matatu wakiendelea na mambo yao,baada ya kumaliza jamaa anataka kuondoka,hisia zikamtuma apige simu ya yule mwanamke ili kuona kama inaita,alipopiga akagundua kuwa yule mwanamama alikuwa ameweka zile namba za call barring,alipoulizwa uliziweka mda gani akasema nilipomaliza kuongea nawewe na ukasema unakuja,akimuuliza kwanini uliweka binti anasema aliamua tuu,jee hapa kunausalama kwa huyu jamaa yangu au?Naombeni ushauri wenu juu ya hili swala!!!