Unafurahia mahusiano yako?

Unafurahia mahusiano yako?

mimi najutia niko na mwanaume aliyetendwa sana na mkewe,mke alikuwa malaya wa kutupwa,anafanywa mpaka na wafanyakazi wenzake na huyo bwana,akiwa mzazi wa miezi 3 tu halali ndani mtoto anamwachia dada wa kazi,mume siku akarudi home saa 8 usiku ghafla alikuwa safari kakuta mtoto anachemka homa hafai akamkimbiza hosp piga simu ya mke haipokelewi asubh mke kaamkia job saa 5 asbh ndo anacall back simu ya mumewe kumbe mume yuko hosp na mtoto,ni mengi alimfanyia mumewe huyu mwanamke hadi kumchomea mumewe nyumba saiv wameachana na mume aliachiwa watoto 2 wadogo akahangaika nao hadi sasa wanakua huyo mdogo ana miaka 4,yani huyu mwanaume kajeruhika moyoni yani hayupo romantic kabisa yuko kama mnyama najitahidi kurudisha moyowake awe kawaida lakini inakuwa vigumu mno,namvumilia coz nampenda sitomchoka naamini utafika wakati ataamini tena ktk kupendwa na atakuwa tayari kupokea penzi ninalompa,nashangaa nampendea nn ila basi tu ndo nishampenda hvyohvyo bure acha niangalie nione mwisho wake wallah huyu bwana hana jema hata moja kiujumla sifurahii kabisa kuwa nae ila moyo ndo ushaganda kwake

Sent using Jamii Forums mobile app

Yaani huyo mke wake alikuwa Katili kupindukia
 
my dear kuhusu hili la nguvu wala sitothubutu kuongea naye mana kwanza namwogopa haongeagi na mimi kabisa nikisema ni mnyama namaanisha ni mnyama,akija kwangu ni dk 30 anaondoka na hataki story,tena huja usiku sana wala sijui huwa anawaza nn hadi kuja kwangu siwezi kuandika vituko vya huyu bwana hapa,niongee hata nilie hatojibu kitu ataniangalia tuu hata nilalamike vipi hatojibu neno atanitizama tuu,mwanzo sikumwelewa nikaona hanipendi nikaona mateso nikaamua kumwacha na kumblock akatumia simu ya rafiki yake akaniuliza mbona namwacha bure kakosa nn akaomba nimzoee ndivyo alivyo,sasa nikamweleza rafikiyake kuwa huyu bwana ana visa mimi cwezi zaidi nimechoka kwanza hapokei simuyangu haongei hanijibu msg yupo tu rafiki ananambia shemeji mvumilie huyu mtu mfariji tu kwa kipindi hiki akikaa sawa ndo umwache,ana hali mbaya mno,ndo huyo rafikiyake akanieleza mambo mengi yaliyompata ambayo hyu bwana hakuwahi hata kunigusia akanambia mvumilie ana shida

Sent using Jamii Forums mobile app

Sasa km Mwenyewe hajafunguka unawezaje kumsaidia?
 
hapo ndo panaponipa jakamoyo coz hata mambo yake nimeelezwa na rafikizake wa karibu yeye haongeagi chochote hata kumsaidia ni muhali mimi nimetulia naangalia tu nione mwishowake nduguyangu naamini kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho

Sent using Jamii Forums mobile app


Nachotaka kukushauri ni kuwa usipotoshwe na huruma yako kwake, ishi naye kama wewe.... Yaani usibadilishe tabia zako au maisha yako kwasababu yake,una haki ya kukasirika, kugomba, kucheka, kutania nk
Kwanini nasema hivi....

1. Itasaidia kukulinda wewe binafsi usije kuharibika kisaikolojia, msaada mwema ni ule usiokuwa na madhara kwako.

2. Huwezi kumsaidia kwa staili hiyo, kuna wakati hata naye anaweza akahisi unapretend.

3. Matatizo mengine yanatatulika kwa nguvu ya Mwenyezi Mungu tu, hivyo elekeza nguvu kwenye ibada pia.

4. Na km tatizo ni saikolojia imeharibika basi jua huna huo utaalamu wa kulimaliza, linahitaji wataalamu wa afya ya akili.
 
asante my dear namba 3 ina nguvu kuliko zote na ninajitahidi sana
Nachotaka kukushauri ni kuwa usipotoshwe na huruma yako kwake, ishi naye kama wewe.... Yaani usibadilishe tabia zako au maisha yako kwasababu yake,una haki ya kukasirika, kugomba, kucheka, kutania nk
Kwanini nasema hivi....

1. Itasaidia kukulinda wewe binafsi usije kuharibika kisaikolojia, msaada mwema ni ule usiokuwa na madhara kwako.

2. Huwezi kumsaidia kwa staili hiyo, kuna wakati hata naye anaweza akahisi unapretend.

3. Matatizo mengine yanatatulika kwa nguvu ya Mwenyezi Mungu tu, hivyo elekeza nguvu kwenye ibada pia.

4. Na km tatizo ni saikolojia imeharibika basi jua huna huo utaalamu wa kulimaliza, linahitaji wataalamu wa afya ya akili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera Dada.
Mimi nafurahia mahusiano yangu.
Siri pekee ni mimi na mpenzi wangu /Mume wangu ni marafiki. Muda mwingi tunataniana kama marafiki wa kawaida.

Mbali na kazi , Baadhi ya biashara tunafanya pamoja na kujikuta muda mwingi tunakuwa pamoja.

Siyo mkali na hapendi kutawala, ni msikivu na mwelewa na mwenye upendo. Hamna jukumu la mwanamke au la mwanaume ndani ya nyumba, chochote anakifanya na mimi pia ( isipokuwa hakifanyiki).

Hakuna siri za kuficha ficha hii ni pamoja na simu, password zake zote ninazo na wakati mwingine simu yake naitumia kama yangu na yangu kama yake ( isipokuwa simu za kazi).

Ni mwanaume ambaye ukiniuliza kwa sasa yupo wapi najua alipo na ana mipango gani najua kwa sababu kila kitu tunapanga pamoja.

Nampenda sana kwa sababu ni mahusiano ambayo nilikuwa nayatamani sana. Na mwisho kabisa ni HANDSOME NA GENTLEMAN.

Sitaki kuwaza kwamba anani cheat kwa sababu hiyo hainihusu, kinachonihusu ni kwamba ananipenda na nina mpenda na tunaheshimiana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom