Unafiki wa nchi za kiarabu ndio uliowezesha kuzingirwa kwa Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,194
10,929
Vita vinavyoendelea mpaka kufikia leo vimepitia hatua nyingi na za wazi.Kila mwenye kuelewa alielewa kilichopangwa kutokea.Hii ni kwa vile vita hivi kati ya Israel na wapalestina vimepiganwa katika namna za kisasa tofauti na vita vilivyotangulia vya mwaka 148 na vile vya Yom Kipur vya mwaka 1973.

Kipigo ilichopata Israel kutoka kwa Hamas oktoba 7 kilikuwa kiko wazi sambamba na hasira za Israel kama ilivyoonekana kupitia viongozi wao wa kisiasa.

Kingine kilichoonekana wazi ni makamio ya kulipiza kisasi na matayarisho yake.Kama ni umuhimu wa kutaka kuwatetea wapalestina basi ulionekana kwa mara nyengine kupitia uungwaji mkono wa makamio ya Israel kutoka kwa mataifa makubwa yenye mafungamano na taifa hilo.

Viongozi wa nchi kadhaa marafiki wa Israel walionekana kuhamanika kwa kwenda huku na huko kwa madhumuni mawili.Kwanz kuiunga mkono Israel kwa maneno na vitendo na upande wa pili kuwasisitiza waungaji mkono wa Palestina kwamba waiingilie katika vita hivyo kwa maelezo kuwa vita hivyo visije vikapanuka na kuwa vita vya eneo zima la mashariki ya kati.

Kwa mtu ambaye hana udhaifu wa kiakili na ambaye si mnafiki basi angekuwa makini kuweka masharti yake ya kujizuia kutoingilia kati huko kulikohimizwa na marafiki wa Israel.

Hayo yote yalikuwa ni maandalizi ya vita.Ilikuwa ni madogo kuliko yale yaliyoanza kuonekana mwanzoni mwa vita na mpaka kufikia leo.

Wakati waislamu wamehimizwa kuhurumiana na kujitolea kuwahami wale madhaifu wanaoonewa.Lakini inaonekana mafunzo hayo yanaingia sikio hili na kutokea sikio la pili.Watu wameuliwa kwa maelfu tena kwa njia mbaya ya kuporomoshewa majengo mazito au kuchomwa na moto wa mabomu.Hayo yote yamefanyika kwa watoto na wanawake zaidi na bado hakukuwatia huruma viongozi hao wa nchi za kiarabu.

Tukiangalia mifano na ukubwa wa unafiki huo tunauona kwa nchi tatu zaidi nazo ni Saudi Arabia,Misri na Jordan

Saudi Arabia : Ipo taarifa kuwa mwanmfalme Mohammed Suleiman mara baada ya kuchukua madaraka aliwahi kuwazodoa Hamas na wapalestina kwa jumla kuwa yanayowakuta ni shauri kwani wanatakiwa kukubaliana na mipango ya Israel

Tangu kuanza kwa vita hivi vya Oktoba 7 wamekuwa wako doro sana katika harakati zao za kuwaunga mkono Hamas katika nia ya kukomboa maeneo yao au angalau kuwakemea Israel wasitekeleze azma yao ya kupambana na Hamas

Katika kiwango cha juu cha unafiki wa Saudi Arabia ni kutungua kombora lililorushwa na Houth wa Yemen hapo juzi likielekea kusini ya Israel.

Jordan: Ni nchi yenye mafungamano ya kidugu zaidi na wapalestina kuliko nchi nyengine yoyote ile kwani 80% ya watu wake wana asili ya Palestina.Zaidi ni kuwa eneo la Jerusalem kwenye msikiti wa tatu kwa utakatifu wa Alaqsa,eneo hilo liliporwa kutoka kwao mwaka 1967.

Vita hivi ingekuwa ni fursa kwao kuwafungulia raia wake kuingia Jerusalem kwa namna yoyote wangeona inafaa.Wangefanya hivyo kama vile ambavyo wayahudi kwa kusaidiwa na jeshi la Israel limetumia fursa ya vita hivi vipya kuendelea kunyang'anya maeneo ya wapalesitna yaliyobaki huku wakiwauwa kwa visingizio mbali mbali na kuwaharibia mali zao.

Misri:Ndio nchi pekee ya kiarabu ambayo imepakana na Gaza.Watu huku wakiangamia kwa kuuliwa lakini pia wamekatiwa mahitajio muhimu ya kibinadamu kama chakula,maji na nishati za umeme na mafuta.

Katika hali hiyo huruma ya kibinadamu tu ingefanya nchi hiyo ifungue mpaka bila kushauriana na yoyote.
Kinyume chake viongozi wa nchi hiyo wamekuwa wakiilaumu Israel kwa kutokuingia kwa misaada iliyorundikana mpaka kama ndio sababu ya mahitaji hayo kutoingia Gaza.

Lawama hiyo imeonekana kama ni kula njama na Israel ili ifanikishe mipango yake kwani kituo cha mpaka wa Rafah hakiko Israel na upekuzi wa malori uliolalamikiwa hufanyika kilomita 62 ndani ya ardhi ya Misri.

Tukiendelea kupembua unafiki wa nchi hizo tunaweza kuwakuta Iran kwa kiasi kidogo na Syria. Mfano Pentagon ya Marekani imesema nchi hiyo iko mbioni kuwapelekea Hizbulah mifumo ya ulinzi wa anga. Kama ni kweli uamuzi huo utakuwa ni wa kushangaza kwani wenyewe wamekuwa wakipigwa na Israel wanavyopenda na bila kuwachokoza.Wangetumia mifumo hiyo kujilinda wenyewe kabla ya kufikiria kuipeleka Lebanon kwa Hizbulah.
 
Unalaumu nchi ambazo hazihusiki na ujinga wa Hamas. Hamas walichofanya walidhani majibu yake yangekuwa vipi?! Misri na Jordan walichapigana na Israeli na hawakumweza na hata sasa hatamweza.

Hizi nchi zimefanya vizuri, amalizane na msala wake. Hamas walidanganywa na Iran waanzishe vita, vikundi na nchi nyingine zitajiunga na vita, Israel alijua hili ndio maana alichelewa kuanza vita hadi US alipoweka meli vita pale ili Iran atulie alipo. Israeli ataifagia Gaza iwe nyeupe na hakuna wa kuingilia.

Iran amebakia kuzungumza kwa mafumbo kama waimba taarabu.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Unalaumu nchi ambazo hazihusiki na ujinga wa Hamas. Hamas walichofanya walidhani majibu yake yangekuwa vipi?! Misri na Jordan walichapigana na Israeli na hawakumweza na hata sasa hatamweza...
Umesema. Tusubiri kunaweza kukatokea msaada utakaoshangaza na Hamas kuibuka kidedea.Ushindi haupatikani kwa njia nyepesi.
 
Uchambuzi mzuri Ila umeegemea kutetea magaidi. Misri na saudia wanataka Amani ya mashariki ya Kati, Misri ilishawapokea wapalestina wengi, zaidi ya robo ya raia wa Misri ni wapalestina waliokimbia Vita zilizoyangulia, wawaongeze wengine? Hapana.

Lakini pia wakifungua mpaka wapalestina wengi watakimbia, hivyo Israel itainyakua Gaza Kama mikoa yake, dawa ni kuwalazimisha wapalestina wabaki sababu Israel hawezi kuwauwa wote, jumuia za kimataifa zitaingilia

Mwisho upinzani mkubwa wa Israel unatoka kwa vibaraka wa Irani yaani hauth, Hisbola na hamas. Unataka Saudia amuunge mkono adui yake Iran? Ambaye anatumia vikundi hivyohivyo kupambana na Saudia
 
Saudi Arabia na Jordan zinalindwa na Marekani. Mfalme wa kweli Saudia alikuwa ni Mfalme Faisal na wasaudia wenyewe wanalijua hili.

Abdel FAtteh Al Sisi amewekwa na Marekani baada ya kuondolewa kwa kuhukumiwa kifo Mohammed Morsi.

Morsi alipoingia madarakani alifungua mpaka uliyofungwa baina ya nchi yake na Palestina.

Maana yake kwa namna moja ama nyengine alianza kumsaidia Palestina. Usalama wa Israel ungekuwa mashakani. Kilichotokea unakifahamu.

Nchi ambayo kidogo inajaribu kutafuta suluhu angalau amani ipatikane ni Qatar.

Usalama wa Israel, Marekani wameujenga kwa mahesabu na ndiyo maana mataifa ya pembeni yanaonekana ni dhaifu na Israel anaonekana shujaa anazungumza anavyotaka kwa majirani zako.
 
Hayo yoote ni kukosa uwezo wa kuwakabili Mayahudi yenye jeshi linaloshika no 3 Duniani!
Screenshot_20231007-215254.png
 
Hayo yoote ni kukosa uwezo wa kuwakabili Mayahudi yenye jeshi linaloshika no 3 Duniani!
Myahudi hana jeshi bora! Bali waliyonyuma yake wanaomlinda ni bora. Watu hawamhofii myahudi. Wanahofia waliyo nyuma yake. Wanahofia madhara watakayoyapata.

Ikiwa kama unamfuatilia Israel kwa jicho pevu utagundua ubora wa jeshi la Israel na udhaifu wake pia.
 
Saudi Arabia na Jordan zinalindwa na Marekani. Mfalme wa kweli Saudia alikuwa ni Mfalme Faisal na wasaudia wenyewe wanalijua hili.

Abdel FAtteh Al Sisi amewekwa na Marekani baada ya kuondolewa kwa kuhukumiwa kifo Mohammed Morsi.

Morsi alipoingia madarakani alifungua mpaka uliyofungwa baina ya nchi yake na Palestina.

Maana yake kwa namna moja ama nyengine alianza kumsaidia Palestina. Usalama wa Israel ungekuwa mashakani. Kilichotokea unakifahamu.

Nchi ambayo kidogo inajaribu kutafuta suluhu angalau amani ipatikane ni Qatar.

Usalama wa Israel, Marekani wameujenga kwa mahesabu na ndiyo maana mataifa ya pembeni yanaonekana ni dhaifu na Israel anaonekana shujaa anazungumza anavyotaka kwa majirani zako.
Sahihi
 
Wafalme na ma Rais wa nchi za kiarabu ndio balaa wao ndio wanafanya warabu waonekane mafala hata Natanyahau kawambia wandishi wa habari kuwa viongozi wa nchi za kiarabu ndio wanamuambia lazima awamalize Hamasi 😄

Wacha waote Natanyahau na Viongozi wa kiarabu na kina Joe, Hamasi pump kubwa hakuna anaye weza wamaliza.
 
Wafalme na ma Rais wa nchi za kiarabu ndio balaa wao ndio wanafanya warabu waonekane mafala hata Natanyahau kawambia wandishi wa habari kuwa viongozi wa nchi za kiarabu ndio wanamuambia lazima awamalize Hamasi

Wacha waote Natanyahau na Viongozi wa kiarabu na kina Joe, Hamasi pump kubwa hakuna anaye weza wamaliza.
Kuna siku na wao yatawafika tusubiri hapa ,marekani hana adui wala rafiki wa kudumu
 
Magaidi lazima yashughulikiwe kwa nguvu zote! Hata waarabu wenyewe wamechoka na mauaji ya kikatili yanayofanywa na hamas
 
Vita vinavyoendelea mpaka kufikia leo vimepitia hatua nyingi na za wazi.Kila mwenye kuelewa alielewa kilichopangwa kutokea.Hii ni kwa vile vita hivi kati ya Israel na wapalestina vimepiganwa katika namna za kisasa tofauti na vita vilivyotangulia vya mwaka 148 na vile vya Yom Kipur vya mwaka 1973.

Kipigo ilichopata Israel kutoka kwa Hamas oktoba 7 kilikuwa kiko wazi sambamba na hasira za Israel kama ilivyoonekana kupitia viongozi wao wa kisiasa.

Kingine kilichoonekana wazi ni makamio ya kulipiza kisasi na matayarisho yake.Kama ni umuhimu wa kutaka kuwatetea wapalestina basi ulionekana kwa mara nyengine kupitia uungwaji mkono wa makamio ya Israel kutoka kwa mataifa makubwa yenye mafungamano na taifa hilo.

Viongozi wa nchi kadhaa marafiki wa Israel walionekana kuhamanika kwa kwenda huku na huko kwa madhumuni mawili.Kwanz kuiunga mkono Israel kwa maneno na vitendo na upande wa pili kuwasisitiza waungaji mkono wa Palestina kwamba waiingilie katika vita hivyo kwa maelezo kuwa vita hivyo visije vikapanuka na kuwa vita vya eneo zima la mashariki ya kati.

Kwa mtu ambaye hana udhaifu wa kiakili na ambaye si mnafiki basi angekuwa makini kuweka masharti yake ya kujizuia kutoingilia kati huko kulikohimizwa na marafiki wa Israel.

Hayo yote yalikuwa ni maandalizi ya vita.Ilikuwa ni madogo kuliko yale yaliyoanza kuonekana mwanzoni mwa vita na mpaka kufikia leo.

Wakati waislamu wamehimizwa kuhurumiana na kujitolea kuwahami wale madhaifu wanaoonewa.Lakini inaonekana mafunzo hayo yanaingia sikio hili na kutokea sikio la pili.Watu wameuliwa kwa maelfu tena kwa njia mbaya ya kuporomoshewa majengo mazito au kuchomwa na moto wa mabomu.Hayo yote yamefanyika kwa watoto na wanawake zaidi na bado hakukuwatia huruma viongozi hao wa nchi za kiarabu.

Tukiangalia mifano na ukubwa wa unafiki huo tunauona kwa nchi tatu zaidi nazo ni Saudi Arabia,Misri na Jordan

Saudi Arabia : Ipo taarifa kuwa mwanmfalme Mohammed Suleiman mara baada ya kuchukua madaraka aliwahi kuwazodoa Hamas na wapalestina kwa jumla kuwa yanayowakuta ni shauri kwani wanatakiwa kukubaliana na mipango ya Israel

Tangu kuanza kwa vita hivi vya Oktoba 7 wamekuwa wako doro sana katika harakati zao za kuwaunga mkono Hamas katika nia ya kukomboa maeneo yao au angalau kuwakemea Israel wasitekeleze azma yao ya kupambana na Hamas

Katika kiwango cha juu cha unafiki wa Saudi Arabia ni kutungua kombora lililorushwa na Houth wa Yemen hapo juzi likielekea kusini ya Israel.

Jordan: Ni nchi yenye mafungamano ya kidugu zaidi na wapalestina kuliko nchi nyengine yoyote ile kwani 80% ya watu wake wana asili ya Palestina.Zaidi ni kuwa eneo la Jerusalem kwenye msikiti wa tatu kwa utakatifu wa Alaqsa,eneo hilo liliporwa kutoka kwao mwaka 1967.

Vita hivi ingekuwa ni fursa kwao kuwafungulia raia wake kuingia Jerusalem kwa namna yoyote wangeona inafaa.Wangefanya hivyo kama vile ambavyo wayahudi kwa kusaidiwa na jeshi la Israel limetumia fursa ya vita hivi vipya kuendelea kunyang'anya maeneo ya wapalesitna yaliyobaki huku wakiwauwa kwa visingizio mbali mbali na kuwaharibia mali zao.

Misri:Ndio nchi pekee ya kiarabu ambayo imepakana na Gaza.Watu huku wakiangamia kwa kuuliwa lakini pia wamekatiwa mahitajio muhimu ya kibinadamu kama chakula,maji na nishati za umeme na mafuta.

Katika hali hiyo huruma ya kibinadamu tu ingefanya nchi hiyo ifungue mpaka bila kushauriana na yoyote.
Kinyume chake viongozi wa nchi hiyo wamekuwa wakiilaumu Israel kwa kutokuingia kwa misaada iliyorundikana mpaka kama ndio sababu ya mahitaji hayo kutoingia Gaza.

Lawama hiyo imeonekana kama ni kula njama na Israel ili ifanikishe mipango yake kwani kituo cha mpaka wa Rafah hakiko Israel na upekuzi wa malori uliolalamikiwa hufanyika kilomita 62 ndani ya ardhi ya Misri.

Tukiendelea kupembua unafiki wa nchi hizo tunaweza kuwakuta Iran kwa kiasi kidogo na Syria. Mfano Pentagon ya Marekani imesema nchi hiyo iko mbioni kuwapelekea Hizbulah mifumo ya ulinzi wa anga. Kama ni kweli uamuzi huo utakuwa ni wa kushangaza kwani wenyewe wamekuwa wakipigwa na Israel wanavyopenda na bila kuwachokoza.Wangetumia mifumo hiyo kujilinda wenyewe kabla ya kufikiria kuipeleka Lebanon kwa Hizbulah.
Huyu ni muislam mjinga kuwahi kutokea Duniani, hivi huko madrasa uwa mnajifunza nini🤣🤣🤣
Sema una bahati ulikimbilia kuomba hifadhi Tanzania, nawe sahivi ungekuwa unaandika thread yako Jf ukiwa chini ya ardhi kama wenzako Gaza wanaoishi shimoni kama panya.
 
Vita vinavyoendelea mpaka kufikia leo vimepitia hatua nyingi na za wazi.Kila mwenye kuelewa alielewa kilichopangwa kutokea.Hii ni kwa vile vita hivi kati ya Israel na wapalestina vimepiganwa katika namna za kisasa tofauti na vita vilivyotangulia vya mwaka 148 na vile vya Yom Kipur vya mwaka 1973.

Kipigo ilichopata Israel kutoka kwa Hamas oktoba 7 kilikuwa kiko wazi sambamba na hasira za Israel kama ilivyoonekana kupitia viongozi wao wa kisiasa.

Kingine kilichoonekana wazi ni makamio ya kulipiza kisasi na matayarisho yake.Kama ni umuhimu wa kutaka kuwatetea wapalestina basi ulionekana kwa mara nyengine kupitia uungwaji mkono wa makamio ya Israel kutoka kwa mataifa makubwa yenye mafungamano na taifa hilo.

Viongozi wa nchi kadhaa marafiki wa Israel walionekana kuhamanika kwa kwenda huku na huko kwa madhumuni mawili.Kwanz kuiunga mkono Israel kwa maneno na vitendo na upande wa pili kuwasisitiza waungaji mkono wa Palestina kwamba waiingilie katika vita hivyo kwa maelezo kuwa vita hivyo visije vikapanuka na kuwa vita vya eneo zima la mashariki ya kati.

Kwa mtu ambaye hana udhaifu wa kiakili na ambaye si mnafiki basi angekuwa makini kuweka masharti yake ya kujizuia kutoingilia kati huko kulikohimizwa na marafiki wa Israel.

Hayo yote yalikuwa ni maandalizi ya vita.Ilikuwa ni madogo kuliko yale yaliyoanza kuonekana mwanzoni mwa vita na mpaka kufikia leo.

Wakati waislamu wamehimizwa kuhurumiana na kujitolea kuwahami wale madhaifu wanaoonewa.Lakini inaonekana mafunzo hayo yanaingia sikio hili na kutokea sikio la pili.Watu wameuliwa kwa maelfu tena kwa njia mbaya ya kuporomoshewa majengo mazito au kuchomwa na moto wa mabomu.Hayo yote yamefanyika kwa watoto na wanawake zaidi na bado hakukuwatia huruma viongozi hao wa nchi za kiarabu.

Tukiangalia mifano na ukubwa wa unafiki huo tunauona kwa nchi tatu zaidi nazo ni Saudi Arabia,Misri na Jordan

Saudi Arabia : Ipo taarifa kuwa mwanmfalme Mohammed Suleiman mara baada ya kuchukua madaraka aliwahi kuwazodoa Hamas na wapalestina kwa jumla kuwa yanayowakuta ni shauri kwani wanatakiwa kukubaliana na mipango ya Israel

Tangu kuanza kwa vita hivi vya Oktoba 7 wamekuwa wako doro sana katika harakati zao za kuwaunga mkono Hamas katika nia ya kukomboa maeneo yao au angalau kuwakemea Israel wasitekeleze azma yao ya kupambana na Hamas

Katika kiwango cha juu cha unafiki wa Saudi Arabia ni kutungua kombora lililorushwa na Houth wa Yemen hapo juzi likielekea kusini ya Israel.

Jordan: Ni nchi yenye mafungamano ya kidugu zaidi na wapalestina kuliko nchi nyengine yoyote ile kwani 80% ya watu wake wana asili ya Palestina.Zaidi ni kuwa eneo la Jerusalem kwenye msikiti wa tatu kwa utakatifu wa Alaqsa,eneo hilo liliporwa kutoka kwao mwaka 1967.

Vita hivi ingekuwa ni fursa kwao kuwafungulia raia wake kuingia Jerusalem kwa namna yoyote wangeona inafaa.Wangefanya hivyo kama vile ambavyo wayahudi kwa kusaidiwa na jeshi la Israel limetumia fursa ya vita hivi vipya kuendelea kunyang'anya maeneo ya wapalesitna yaliyobaki huku wakiwauwa kwa visingizio mbali mbali na kuwaharibia mali zao.

Misri:Ndio nchi pekee ya kiarabu ambayo imepakana na Gaza.Watu huku wakiangamia kwa kuuliwa lakini pia wamekatiwa mahitajio muhimu ya kibinadamu kama chakula,maji na nishati za umeme na mafuta.

Katika hali hiyo huruma ya kibinadamu tu ingefanya nchi hiyo ifungue mpaka bila kushauriana na yoyote.
Kinyume chake viongozi wa nchi hiyo wamekuwa wakiilaumu Israel kwa kutokuingia kwa misaada iliyorundikana mpaka kama ndio sababu ya mahitaji hayo kutoingia Gaza.

Lawama hiyo imeonekana kama ni kula njama na Israel ili ifanikishe mipango yake kwani kituo cha mpaka wa Rafah hakiko Israel na upekuzi wa malori uliolalamikiwa hufanyika kilomita 62 ndani ya ardhi ya Misri.

Tukiendelea kupembua unafiki wa nchi hizo tunaweza kuwakuta Iran kwa kiasi kidogo na Syria. Mfano Pentagon ya Marekani imesema nchi hiyo iko mbioni kuwapelekea Hizbulah mifumo ya ulinzi wa anga. Kama ni kweli uamuzi huo utakuwa ni wa kushangaza kwani wenyewe wamekuwa wakipigwa na Israel wanavyopenda na bila kuwachokoza.Wangetumia mifumo hiyo kujilinda wenyewe kabla ya kufikiria kuipeleka Lebanon kwa Hizbulah.
Wewe unongea maneno tu kama hao. Waarabu hawa wamejitambua ,siyo wale wa ndg katika imani.
Ukaue watoto wa wa watu na wanawake, uwachukue mateka, unapoanza kupigwa uwaite wengine waje kukupigania, hawataki ujinga huo tena.
Unadhani hawajui,wanajua na wanaona kinachotokea.
Kwa hatua iliyofikia hadi sasa , Gaza imezingirwa, walioko mashimoni hawawezi tena kupokea msaada, wa silaha, chakula wala dawa, maana yake nini ,akiba waliyonao huko mashimoni wataitumia na oxygen.ikiisha basi.,ama watoke wakiwa wamejisalimisha, au wafie humo.
Hata ikitokea kuna yeyote atashambulia ,atashambulia Israel na siyo walioko Gaza.
 
Wewe unongea maneno tu kama hao. Waarabu hawa wamejitambua ,siyo wale wa ndg katika imani.
Ukaue watoto wa wa watu na wanawake, uwachukue mateka, unapoanza kupigwa uwaite wengine waje kukupigania, hawataki ujinga huo tena.
Unadhani hawajui,wanajua na wanaona kinachotokea.
Kwa hatua iliyofikia hadi sasa , Gaza imezingirwa, walioko mashimoni hawawezi tena kupokea msaada, wa silaha, chakula wala dawa, maana yake nini ,akiba waliyonao huko mashimoni wataitumia na oxygen.ikiisha basi.,ama watoke wakiwa wamejisalimisha, au wafie humo.
Hata ikitokea kuna yeyote atashambulia ,atashambulia Israel na siyo walioko Gaza.
Mbona bado wako hai na wanaendelea kutoa vidio na takwimu za vita.Usicheze na Mwenyezi Mungu wewe.Mipango yake haiendi kama wanavyopenda watu.
Israel wamezoea kucheza ngumi za Tyson.
Tumezoea vita vya wiki moja na wiki 2.Sasa ni karibu mwezi na wametumbukia katikati ya shimo hawawezi kutoka tena.Na wao wamezingirwa na wanaona haya kama malaya aliyefumaniwa gesti na hawara yake.
 
Back
Top Bottom