Unafiki wa mama yangu na dada zangu

Unafiki wa mama yangu na dada zangu

Pole yake atakayekuja kuolewa na huo MZIGO unaouita ndugu.

I guess una kawivu kidogo kwasababu mgeni anapewa royal treatment. Nakuhakikishia hata dada zako hawaEnjoy hizo shughuli.

Jitu halitandiki kitanda, halitoi sahani, eti kisa mwanaume! Naijua mimi MIZIGO ya hivi.
 
Kuna mawili, huyo jamaa ni babako wa kambo au shemeji yako.
 
Utaratibu wenu mbovu, yaani kila mtu akaoshe chombo chake kwenye sink ndo nn? Vyombo vinakusanywa vinaoshwa pamoja kwa usafi, hyo familia yako inawanawake watatu ukimtoa mama yako, sasa kwann mnashindwa kuorganise mambo madogo kama haya?
 
Duh! Kumbe na we una kazi nkajua bado uko sekondari,mana unavolalama kama vile ni fomu wani
 
Mi hata cjakuelewa unacho lalamika hapo zaidi ww roho yako itakua mbaya sana unaumizwa na vitu ambavyo havina msingi hasa ukiangalia ww hapo ni mpita njia tu
 
mmmh mmzazi wako anawezaje kuwa mnafiki?? khaa em rekebisha kauli yako kwanza !!!
 
Habarini wadau,kwa takribani wiki mbili sasa nipo nyumbani kwetu(kwa baba na mama) baada ya kuchukua likizo ya mwezi mmoja kazini.hapa nyumbani ninaye dada zangu wawili na dada wa kazi.

Moja kwa moja twende kwenye mada husika,siku mbili baada ya mimi kuwasili hapa home akaja ndugu yetu mmoja hiv wa kiume ambaye rika lake ni sawa na mimi tu.huyu ndugu siyo mara yake ya kwanza kuja hapa home kwa mujibu wa maelezo ya mama lakini kwa upande wangu tumeonana awamu hii.kwa maana hiyo huwa anawatembelea mara kwa mara mm nkiwa zangu mkoa mwingine kikazi.

Kinacho nishangaza kuhusu huyu ndugu anavoishi hapa home,yaani yeye ni mtu ambaye hajishugulishi na chochote,yaani yeye ni kama boss hapa home.Muda wa msos tunajumuika vizur tu,lakini chombo atakacho piga msos atakiacha hapohapo,hawa ndugu zangu ama mama huchukua jukumu la kumuoshea chombo chake.Hii hali imekuwa kero sasa kwa upande wangu,maana binafsi nikirud hapa home,nashiriki kila kitu muhimu cha hapa ikiwemo kuosha chombo changu ambacho nimepigia msosi.kiukweli imekuwa ni kero saana maana utakuta siku katoka,akirudi anakuta sisi tumeshakula na hivo msos ulio bakia ni kwa ajili yake tu..lakini ataishia kula na kuacha kila kitu hapo hapo mpaka glass aliyo nywea maji..dada zangu watakuja kuvitoa na kwenda kuviosha.

Huyu ndugu analala na mimi,hvo mida ya asubuh siku zingine huwa nawah kuamka kwa ajili ya michakato yangu.nikirud ile sa nne nakuta kaamka,kaoga kakaa sebuleni lakn kitanda hata hakijatandikwa.Binafsi sina maneno mengi,ninacho kifanya ni kutandika tu basi na kuendelea na mishe.



Nb..kinacho niuma zaidi mother anafahamu kila kitu lakin haongei lolote.yaani hata kikombe cha kunywea chai anakiacha hapohapo,hata kwenda tu kukisuuza ni kazi wadau.maana karo la kuoshea vyombo liko ndani humuhumu.Ingekuwa ni mara yake ya kwanza kuja hapa home nisingemlaumu kwa kufanya hivo,lkn wanadai ni mara nyingi tu huwa anakuja na anafanya hivohvo.


vp wadau,tatzo huwa ni nini? je,nimchane live ama nimpotezee? maana jamaa anaondoka kesho
Mbona na ww hujamweleza? Kwahiyo na ww ni mnafiki pia
 
Huyo jamaa yako atakuwa ana mzigo anauchukua hapo, eiri siyo bure. Fuatilia mkuu
 
Huyo ni mgeni wa familia.. Siyo mtumishi,hata angeviosha bado ungelalama anakula bure
 
Mhhh vijiba vya roho vingine mi siviwezagi aisee,ntaangalia umri wako ukiwa mkubwa sikugusi
Wengine ukiwa nyumbani shurti ushiriki shughuli kama wanafamilia wengine,
Huyo ni mkiamka asbh mnagawa kazi wewe fagia uwanja, osha vyombo,mwingine pika chai deki ndani mwingine safisha Choo,sebleni,mwingine aende sokoni nk nk
Mpangie kazi ya kufanya
Akimaliza kula mwambie calmly tu chief peleka vyombo hivo jikoni
Atazoea tu
It happens lakini makuzi tofauti na smtym kelele nyingi za nini
 
Kwahiyo katika familia yenu kila mtu akishakula anaenda kuosha chombo chake? Kweli kila familia na vituko vyake asee...mwe!
Zaidi ya vituko,sipatii picha mshua
Sijawahi muona kashika chombo aoshe aisee
 
Habarini wadau,

Kwa takribani wiki mbili sasa nipo nyumbani kwetu (kwa baba na mama) baada ya kuchukua likizo ya mwezi mmoja kazini, hapa nyumbani ninaye dada zangu wawili na dada wa kazi.

Moja kwa moja twende kwenye mada husika, siku mbili baada ya mimi kuwasili hapa nyumbani akaja ndugu yetu mmoja wa kiume ambaye rika lake ni sawa na mimi huyu ndugu siyo mara yake ya kwanza kuja hapa nyumbani, kwa mujibu wa maelezo ya mama lakini kwa upande wangu tumeonana awamu hii kwa maana hiyo huwa anawatembelea mara kwa mara mimi nikiwa zangu mkoa mwingine kikazi.

Kinachonishangaza kuhusu huyu ndugu anavoishi hapa home, yaani yeye ni mtu ambaye hajishugulishi na chochote,yaani yeye ni kama boss hapa home.Muda wa msosi tunajumuika vizuri tu, lakini chombo atakacho piga msosi atakiacha hapohapo,hawa ndugu zangu ama mama huchukua jukumu la kumuoshea chombo chake.Hii hali imekuwa kero sasa kwa upande wangu maana binafsi nikirudi hapa home,nashiriki kila kitu muhimu cha hapa ikiwemo kuosha chombo changu ambacho nimepigia msosi.

Kiukweli imekuwa ni kero sana maana utakuta siku katoka,akirudi anakuta sisi tumeshakula na hivo msosi ulio bakia ni kwa ajili yake tu lakini ataishia kula na kuacha kila kitu hapo hapo mpaka glass aliyo nywea maji dada zangu watakuja kuvitoa na kwenda kuviosha.

Huyu ndugu analala na mimi,hivo mida ya asubuhi siku zingine huwa nawahi kuamka kwa ajili ya michakato yangu. Nikirudi ile sa nne nakuta kaamka,kaoga kakaa sebuleni lakini kitanda hata hakijatandikwa.Binafsi sina maneno mengi,ninachokifanya ni kutandika tu basi na kuendelea na mishe.

Nb; kinacho niuma zaidi mother anafahamu kila kitu lakini haongei lolote yaani hata kikombe cha kunywea chai anakiacha hapohapo, hata kwenda tu kukisuuza ni kazi wadau, maana karo la kuoshea vyombo liko ndani humuhumu.Ingekuwa ni mara yake ya kwanza kuja hapa home nisingemlaumu kwa kufanya hivo, lakini wanadai ni mara nyingi tu huwa anakuja na anafanya hivyohivyo.

Vipi wadau, tatizo huwa ni nini? Je, nimchane live ama nimpotezee? Maana jamaa anaondoka kesho.
Hapo wewe ndie tatizo hupendi wageni halafu kuhusu kuosha vyombo ni utaratibu wa wapi huo kila mtu anaosha chombo chake ?mko boarding school au kambini?inaonesha familia yenu ni ya watu wabinafsi wenye choyo asante mama yako ni mwenye busara kakukalia kimya upuuzi wako.
Kijana badilika umesema mwenyewe huyo ni mgeni wenu basi mkarimu na hizo figisu za vyombo kwa maadili ya kiafrika dada zako wanastahili sana kuzifanya japo nitakuwa pamoja nawe suala la unadhifu wa kitanda .
 
Mie nasubiri mrejesho wa hii stori sababu hujajibu uhusiano wako na huyo jamaa, na kwanini unaogopa kumueleza yote uliyomwaga humu na kwanini uwaite nduguzo wanafiki wakati wewe ndo no. Moja?
 
Back
Top Bottom