sea emperor
JF-Expert Member
- Jan 21, 2016
- 250
- 116
Acha uchoyo Dogo hutaki wageni?
Huyo mtu ni nani kwenu..??Habarini wadau,kwa takribani wiki mbili sasa nipo nyumbani kwetu(kwa baba na mama) baada ya kuchukua likizo ya mwezi mmoja kazini.hapa nyumbani ninaye dada zangu wawili na dada wa kazi.
Moja kwa moja twende kwenye mada husika,siku mbili baada ya mimi kuwasili hapa home akaja ndugu yetu mmoja hiv wa kiume ambaye rika lake ni sawa na mimi tu.huyu ndugu siyo mara yake ya kwanza kuja hapa home kwa mujibu wa maelezo ya mama lakini kwa upande wangu tumeonana awamu hii.kwa maana hiyo huwa anawatembelea mara kwa mara mm nkiwa zangu mkoa mwingine kikazi.
Kinacho nishangaza kuhusu huyu ndugu anavoishi hapa home,yaani yeye ni mtu ambaye hajishugulishi na chochote,yaani yeye ni kama boss hapa home.Muda wa msos tunajumuika vizur tu,lakini chombo atakacho piga msos atakiacha hapohapo,hawa ndugu zangu ama mama huchukua jukumu la kumuoshea chombo chake.Hii hali imekuwa kero sasa kwa upande wangu,maana binafsi nikirud hapa home,nashiriki kila kitu muhimu cha hapa ikiwemo kuosha chombo changu ambacho nimepigia msosi.kiukweli imekuwa ni kero saana maana utakuta siku katoka,akirudi anakuta sisi tumeshakula na hivo msos ulio bakia ni kwa ajili yake tu..lakini ataishia kula na kuacha kila kitu hapo hapo mpaka glass aliyo nywea maji..dada zangu watakuja kuvitoa na kwenda kuviosha.
Huyu ndugu analala na mimi,hvo mida ya asubuh siku zingine huwa nawah kuamka kwa ajili ya michakato yangu.nikirud ile sa nne nakuta kaamka,kaoga kakaa sebuleni lakn kitanda hata hakijatandikwa.Binafsi sina maneno mengi,ninacho kifanya ni kutandika tu basi na kuendelea na mishe.
Nb..kinacho niuma zaidi mother anafahamu kila kitu lakin haongei lolote.yaani hata kikombe cha kunywea chai anakiacha hapohapo,hata kwenda tu kukisuuza ni kazi wadau.maana karo la kuoshea vyombo liko ndani humuhumu.Ingekuwa ni mara yake ya kwanza kuja hapa home nisingemlaumu kwa kufanya hivo,lkn wanadai ni mara nyingi tu huwa anakuja na anafanya hivohvo.
vp wadau,tatzo huwa ni nini? je,nimchane live ama nimpotezee? maana jamaa anaondoka kesho
Nimecheka sana HahahahahaHuyo nduguyo ana element halisi za kiume siyo wewe ulizoea kuchekacheka na kushinda na dada zako na Mama.
Kwa sisi wanaumme wa kanda ya ziwa hatuna hizo time kuosha vyombo wakati dada zangu wapo.
Hii familia ni kioja. Mimi naona familia nzima imejaa unafiki. Kijana anawaita mama na dada zake wanafiki. Sababu za kuwaita hivyo pengine ni kwa sababu hawamwambii kasoro zake huyo asiyeosha vyombo. Lakini wakati huo huo huyu kijana nae badala ya kumwambia kasoro zake huyo asiyeosha vyombo na kutandika kitanda au kushauriana na ndugu zake juu ya nini cha kufanya kuhusu huyo bwana, nae kwa unafiki anakuja kulalamika JF kiunafiki. Kiufupi familia inampiga majungu mgeni pembeni bila yeye kujua badala ya kuangalia ni yapi kati ya matendo yake yanyamaziwe na ni yapi wamweleze ili abadilike kitabia ukizingatia kuwa watu tunakulia katika mazingira tofauti tofauti na wakati mwingine unaweza kufanya jambo ukidhani uko sahihi kumbe sivyo. Hii ni ajabu sana. Mwisho hili la kila mtu kuosha chombo chake baada ya chakula ni mapinduzi makubwa katika jamii yetu ya kiafrika.Kweli kila familia ina taratibu zake..Yaani kila mtu baada ya kula anaenda kuosha chombo chake mwenyewe..Na hadi mgeni akija akishakula na yeye kwenye sink kuosha vyombo..