Yaani wewe Kama ni mke wangu nakuacha Mara mojawaswahili wenzangu hii tabia ya kwenda kwa mtu usiku bila taarifa yeyote alafu unayegemea ule,na mambo kama hayo hivi unategemea watu wajiandaeje sasa.
hivi kwa nini mnaendekeza hii tabia inayokera kupita maelezo.
kumbuka kupika chakula cha mtu mmoja ni gharama na pia inagharimu muda jamani.
kwa mfano ugali na wali kuupika inachukua karibia dakika 40 hadi lisaa
sisi wamama ukija kwetu hata bila taarifa inabidi upikiwe.
unamshtukiza mtu bila taarifa jamani
Kama mtu hajafundishwa toka nyumbani basi hata maadili ya dini hajui?
Mambo mengi tunajifunza tukiwa bado wadogo na tunakuwa nayo
Mimi sio mhubiri ila najua kuwa nyumbani kwa mtu ni private na mtu lazima awe na heshima
Nitakuja kwako kwq dharura au kukutembelea lakini kwa taarifa pia na siwezi kuja kwako mchana wala usiku na huo ndio utaratibu
Nenda kwa mtu ukiwa umeshiba au jizuie kuwakalifu wenzio kwani hujui nao wana hali gani
Sent from my SM-G570F using Tapatalk
mi kwa imani yangu kuna watu walipokea watu nyumbani kwao wakawafanyia ukarimu kwa kuwachinjia kondoo alienona kumbe wale watu ni malaika wakamwambia mambo mazuri yakaja timia....kuna watu walitoa kibaba cha mafuta ya mwisho yaliyobakia kwa wageni mafuta yakazidishwa....acheni uchoyo mnaelekea kubaya.mwanamke ukalalamike kupika ugali mara mbili kweli haipendezi kabisa....mie napika kwa furaha zote..sharp
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe utakuwa Muhaya.
Mie kwangu mtu aje tu, aje na taarifa asije na taarifa sawa tu, kwanza hizi taarifa ni kero wakat mwingine itabidi ujipange wee kama unataka kupika solo la harusini, akija bila taarifa ndio mpango kipo kinapikwa, hakipo atakunywa soda hata maji ya bomba pia, muhimu nafsi yako inatoaje, katika uislamu kuna hadithi inasema ina ammali bin niyatin, kila amali italipwa kwa nia, kuna mwingine anampikia mgeni wake vizur akiondoka huku nyuma anaanza kumsimanga kapika tu ili mradi, kuna mwingine anapika vizuri kwa sababu anajua tumeamrisjwa kuwakarimu vizur wagen wetu, kumkarimu vizuri ni kuna thawabu na mtu mwenda kumtembelea mtu kwake kuna thawabu zote ni ibada katika uislamu! So tufanye vitu kutoka moyoni kiroho safi sio kufanya kwa kuigiza, kaja kanikuta kuna sehemu nawahi namueleza ukweli kuwa hii ni saa 5 kamili, 5 na dk 20 nahitajika sehemu, kwanini tunafosi kuigiza maisha wajameni.. Kaja kuna samaki ndani na mie ninataka kusongewa ugali tutakula ugali, kakuta nagongewa mayai basi sawa tutatafuna, hakuna kitu kabisa hata glass ya maji sawa pia..
Sent using my nokia ya tochi
Mnazifukuza baraka kwa kutopenda wageni.
Hata kama ametokea Himo na amekuja kwako Sanawari huyo ni mgeni.Mpe karibisho la mgeni.Hawa wanaoongelewa si wageni, hawa ni wenyeji tusioishi nao...
VIIXCCCL GrandLodge,ARUSHA
Nakubaliana na wewe ingawa umeelekea kushoto sanaMkuu Ni maisha yako siyaingilii but Kuna kitu lazma ukitazame upya.
Mwaka 2015, nilikuwa meajiriwa wa KIA Kama mhandisi wa mifumo ya computer sikuwa nimeoa na nilikuwa nakaa na mpenzi wangu wa mda mrefu. Tulipanga nyumba nzima iliyokuwa na partition 2 hivyo partition nyingine alikuwa anaishi jamaa wa TRA .
Mimi kwetu ndo wa kwanza kuzaliwa na katika kunisomesha kwangu mpka Wazazi waliuza Rasilimali nyingi kwa sababu hawakuwa na uwezo mkubwa, nilivyomaliza chuo na kupata kazi ilikuwa ahueni kwa Wazazi ili niweze kuwasaidia wadogo zangu waliobaki. Sasa kwa sababu uwezo ulikuwepo niliwatafitia shule za bweni, na kwangu ndgu walikuwa hawakauki kuja karibia kila wiki na hata madogo wakiwa likizo nilikuwa nawatumia nauli waje..
Siku moja huyu jamaa yangu wa TRA kaniita ananiambia Kaka nataka nikupe ushauri " ukiataka kuishi vizuri na mkeo mpe uhuru, usiruhusu ndugu kuja Mara kwa Mara wanamnyima Uhuru, Hao ndgu waambie ushakuwa na maisha yako kwa hiyo Kama Kuna Jambo la kifamilia nendeni mkamalize Ila sio kufuatana fuatana kwako, mkeo hajisikii vizuri. Akaendelea " wewe SI unaona kwangu Niko mm tu na mke na maisha yetu Ni Raha kweli mm sitaki ndgu kwangu na nilishawaambia maana wananichonganisha na mke wangu, awe mama, baba, au wadogo Kama Kuna tatzo tupigiane simu tu".
Huyu jamaa nikamuitikia tu, kwa s'babu pale hata ndgu wa kike walikuwa wanakuja. Sasa huyu mpenzi wangu akaanza kubadilika na kufanya visa kwa ndgu nilipothibisha kwa asilimia 100, niliachana nae akarudi kwao.
Na sitarajii kuoa mpaka nione wadogo zangu wamesimama bila utegemezi na hata nikioa sharti kudumu kwenye lazma mwanamke apende familia yangu.
Hizi tabia sio za kisfrika huu Ni uchoyo, nowdays Kuna majiko ya gesi hata dk5 haiishi chakula kimeiva, unashindwaje kumuandalia ndgu, jamaa au rafiki?

naugua kabisaaa, sa namfikiria mtu ambaye ana njaa na uwezo wa kupata msosi hana! Wahaya walikufanyia kitu kibaya sana inaelekea???
Nikuombe msamaha kwa niaba yao wote
Sent using Jamii Forums mobile app