Unaduwaa au unashupaa?

marcus rojo

JF-Expert Member
Mar 19, 2017
1,496
5,317
Na Cmn Mtega Kayoka

17 Phds at BoT

1. Kuna kitu tunaita Symbolic Power... ambacho huzalisha social capital... mtu mwenye symbolic power kubwa sana katika Jamii... Kama Rais au Askofu au CDF au IGP huwa na higher social capital kwa hiyo akisema jambo kwa mfano huweza kuchukuliwa ni sahihi kwa sababu mtaji wake wa kijamii social capital by virtue of his symbolic power yaani nguvu ambayo haihitaji polisi wala majeshi kufanya analosema likubalike Cheo Chake tu ni nguvu inayotosha hatahojiwa wala kuulizwa maswali social capital plus symbolic power.

2. Hiyo social capital ina sababisha yeye mwenye symbolic power aweze kufanya udhibiti wa matini discourse control na discourse control strategies ni kwa kutumia vitisho sheria kuweka ndani watu na kuwamyamazisha bila kuwapata fursa ya kujibu discourse silencing.

3. Zile PHD 17 hazijapewa nafasi kuzungumza discourse silencing ili tujue nini kiliwakwaza sheria maslahi binafsi iasa nyingi au uwezo dhaifu?

4. Zile PHD 17 zimeambiwa hazifanyikazi argumentum ad hominem hoja ya kashfa ukishakashifiwa na mtu mwenye symbolic power unashushwa hadhi na hoja yako haitakuwa na mashiko tena ukijitetea ndio maana watu wakaanza kusema wasomi ni wezi wasaliti hawatufai

5. Tuulizane ni nani aliyesema kuwa ili uwe na ubunge na ukuu wa mkoa unahitaji kujua kusoma na kuandika tu na hao ndio wanapitisha sheria mbovu za kufanyiwa kazi na wasomi wa PhD huko serikalini hao wanaojua kusoma na kuandika tu wanajua athari ya wanachokipitisha sheria hizo ni misahafu huwezi badili licha ya usomi wako.

6. Kila wizara ina vitengo vya Utafiti, je wametengewa shs ngapi za utafiti kila mwaka na watafiti wetu wanatumikaje na je tafiti zinazofanywa zinatumiwa na serikali kuboresha maamuzi na utendaji.

7. Je, wasomi wetu wa vyuo vikuu wanatumika kama washauri na kwa kiwango gani? Ni kiwango gani msomi anapomwambia mwanasiasa juu ya jambo fulani na mwanasiasa akaelewa na kufuata ushauri.

8. Idara za usalama zimejaa wasomi na wachambuzi waliobobea. Je, wanasiasa wanawasikiliza na kutekeleza mashauria yao?

9. Tuna tasnifu zimejaa huko vyuo vikuu ambazo zikisomwa upya unaweza ona jinsi wasomi walivyotoa majibu ya matatizo haya tunayoyazungumza leo kitambo kilichopita ila tuliwapuuza na hata katika utendaji katika baadhi ya maeneo wale wasomi wa kweli wasio na tabia ya ndio bwana ewallah mkuu callers of spade is a spade hawakubaliki hawachaguliwi.

10. Kwa kawaida ukiwa una symbolic power unahitaji ushauri mkubwa sana na wenye uangalifu because whatever you say it goes na hakuna anayeweza kubisha katika genetics kuna kitu kinaitwa meme vizalishi au visambazaji sasa hawa wenye social capital kwa vile wana hegemonic power huwaambukiza memes na wao memes huusambaza ujumbe ukabaki kuwa the only truth there is.

11. Dialogic approach ndio the only way forward demokrasia wananchi wakisema tukae chini tushauriane unapunguziwa mzigo wa kazi kwa zaidi ya nusu na lawama watazibeba wao kwa NIABA yako. Wasomi wa Afrika wanamezwa na Kabila la wanasiasa.

Unaduwaa au unashupaa?
 
Back
Top Bottom