Unadhani hawajisikii vibaya?

Unadhani hawajisikii vibaya?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,508
Reaction score
830,009
1475549728753.jpg

Ni asubuhi ya siku nyingine tena, harakati zimeshaanza na nyingi Zikiwa ni kuwahi kazini au mishemishe pamoja na uchovu wa jana lakini huna budi kuamka na kujiandaa ili uwahi kazini

Ni katika kipindi hiki kwenye hizi harakati za kuwahi kibaruani kuna mtu yuko kitandani muda huu si kwa kupenda la hasha! Anaumia hana kazi naye angetamani muda huu awe anapasi nguo za kazini au yuko barabarani kuwahi

1475549747204.jpg

Anaumia sana akikumbuka alivyosoma kwa tabu na sasa ni mwaka wa tatu huu hana ajira huku washkaji zake wakipeta(mawazo mabaya huanzia hapa)kwanini na si mimi?kwanini wao wapate na mimi nikose? Kwani tunatofautiana nini? INAUMIZA SANA

Huwezi kuendelea kulala siku nzima utaumwa unaamua kutoka uende kijiweni au ukajaribu bahati yako popote lakini du mfukoni huna hata mia!inauma sana.

Siku yako inapita hivyo hivyo kimungu Mungu na jioni inapokaribia unaanza kuwaona watu wakirudi toka makazini, kwenye magari yao na wengine kwenye usafiri wa jumuiya wengine wamechoka wengine wanapiga story inaumiza mno unatamani na wewe ungekuwa mmoja wao

Unavuta picha jinsi ulivyochomekea na tai yako jinsi ulivyohudumia wateja wako kazini changamoto ulizokutana nazo..unajikuta kabisa ukitumika na kuhudumia kwa furaha unapotelea kabisa mawazoni mpaka unatabasamu, na ghafla unashtuka kumbe uko kijiweni honi ya mshikaji uliyesoma naye inakushtua yuko kwenye altezza anatoka job INAUMIZA SANA
1475549719531.jpg


tatizo la ajira ni la dunia nzima lakini hii isiwe kisingizio cha serikali...kila mwaka vijana wetu wanamaliza elimu zao wakitegemea kupata ajira...na idadi inaongezeka kila mwaka.. ! Hili linapaswa kuangaliwa kwa umakini zaidi hali ni mbaya sana mitaani
 
Takwimu za kukua kwa uchumi
Takwimu za kuongezeka pato la Taifa
Takwimu za kuanza kulipa deni la Taifa
Habari za kuhakiki watumishi hewa
Habari za kusitisha ajira nknk
Haya mambo yote haya ni kizungumkuti kwa kijana graduate asiye na ajira na mwenye kutegemewa na wazazi pale kijijini achilia mbali changamoto zake mwenyewe
 
Nafikiri kuna watu watalengwa na machozi wakisoma hapa, natamani mtu wangu mmoja wa karibu asiisome kabisa hii post yako, ila asante kwa kuliona na kutushirikisha, na pia ni alarm kwa wale wenye 'kibarua' kwamba kazi yoyote ni mbaya ukiwa nayo, na pia pamoja na changamoto zilizopo kwenye kazi yako bado kuna wengi wanaitamani
 
Usemacho ni kweli, nafahamu watu kwa ukaribu ambao wanamaumivu kama hayo na baadhi yao wakipata pesa tuu hata ya kupewa au baada ya kufanya deiwaka au kibarua huinywe pombe yote.
Washakata tamaa na maisha. Kweli inaumiza.

Nawaombea heri wote walio kwenye kada hiyo.
 
Usemacho ni kweli, nafahamu watu kwa ukaribu ambao wanamaumivu kama hayo na baadhi yao wakipata pesa tuu hata ya kupewa au baada ya kufanya deiwaka au kibarua huinywe pombe yote.
Washakata tamaa na maisha. Kweli inaumiza.

Nawaombea heri wote walio kwenye kada hiyo.
Kasie ni kweli kabisa lakini hakuna kitu kibaya kama kukata tamaa nimewaona wengi waliokuwa na ndoto nyingi lakini frustrations za ajira zikazima ndoto zote na leo hii ni watu wa bangi na viroba inauma sana
 
Nafikiri kuna watu watalengwa na machozi wakisoma hapa, natamani mtu wangu mmoja wa karibu asiisome kabisa hii post yako, ila asante kwa kuliona na kutushirikisha, na pia ni alarm kwa wale wenye 'kibarua' kwamba kazi yoyote ni mbaya ukiwa nayo, na pia pamoja na changamoto zilizopo kwenye kazi yako bado kuna wengi wanaitamani
Leo hii ukitangaza nafasi kumi za kazi turnover ya waombaji inaweza kukushangaza
Nakukumbuka ajira za uhamiaji kipindi kile waliojitokeza walikuwa elfu kumi wakati nafasi zilikuwa 70 tu
Kwa maisha haya ya sasa ukifanikiwa kupata ajira ipende ilinde na iheshimu
 
dah! hata sijui nitype nini hapa. Asante kwa kuliongelea huku iraiyani ni zaidi ya machozi hasa ukiwaangalia marafiki zako wanavyorudi makazini jioni huku wakipiga hatua za kimaendeleo haraka dah uchungu hatari.
 
Haya yote yamesababishwa na ******** mmoja
Tuna shida kidogo kwenye vipaumbele vyetu kama kile cha kujenga reli kwenda Rwanda yenye watu milioni kumi badala ya kujenga reli kwenda DRC Congo yenye watu zaidi ya milioni mia moja
Ni wazi kuwa kila kimoja kina umuhimu wake lakini kwasasa nchi haina tatizo kubwa la usafiri wa anga! Pengine zile pesa za Bombardier zingetosha kujenga viwanda vidogo vidogo zaidi ya 20 na kuleta ajira zisizopungua 500...nina hakika ajira zitakazotokana na bombardier mbili haziwezi kuzidi miamoja nchi nzima
Vile vile ile project ya kuua upinzani nchini kupitia bwana yule na wengineo pesa yake ingetosha kujenga walau kiwanda kimoja cha matunda mkoani Tanga na kuzalisha ajira zisizopungua 100 kuanzia kukusanya kuuza kuprocess matangazo kutawanya na kuuza
Kwa njia hii tungewapunguzia vijana wengi stress za maisha bila ajira
 
Si mnaambiwa muwe wajasiriamali, kuweni wabunifu acheni kusubiri kuajiriwa
nimecheza anga zote mbili..jaribu kuanzisha biashara yako leo hii ili ujikwamue kimaisha baada ya kukosa ajira uone mziki wake
Kupata tu nyaraka za kukutambua kama mjasiriamali unaweza kukata tamaa na kurudi kijiweni ukavute bangi
Michakato migumu kuanzia kupata mtaji mpaka kusimamisha biashara imewashinda wengi
 
nimecheza anga zote mbili..jaribu kuanzisha biashara yako leo hii ili ujikwamue kimaisha baada ya kukosa ajira uone mziki wake
Kupata tu nyaraka za kukutambua kama mjasiriamali unaweza kukata tamaa na kurudi kijiweni ukavute bangi
Michakato migumu kuanzia kupata mtaji mpaka kusimamisha biashara imewashinda wengi
Ndiyo muisome namba
 
Back
Top Bottom